USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: EZRA 6:1-22 JUMAPILI 26/02/2023
1 Ndipo mfalme Dario akatoa amri, na watu wakatafuta katika nyumba ya vyuo vya tarehe, hapo akiba zilipowekwa katika Babeli.
2 Na chuo kimoja kilipatikana huko Akmetha, katika nyumba ya mfalme iliyo katika wilaya ya Umedi, na ndani yake maneno haya yameandikwa ili yakumbukwe.
3 Katika mwaka wa kwanza wa mfalme Koreshi, mfalme Koreshi alitoa amri, Kwa habari ya nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, nyumba hiyo na ijengwe, mahali watoapo dhabihu, na misingi yake ipigwe na kufanywa imara sana; kuinuka kwake kuwe mikono sitini, na upana wake mikono sitini;
4 ziwepo safu tatu za mawe makubwa, na safu moja ya miti mipya; gharama zake zitolewe katika nyumba ya mfalme.
5 Na vyombo vya dhahabu na fedha, vya nyumba ya Mungu, ambavyo mfalme Nebukadreza alivitoa katika nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu, akavileta mpaka Babeli, na virudishwe, vikaingizwe tena katika hekalu lililoko Yerusalemu, kila kimoja mahali pake, na wewe uvitie katika nyumba ya Mungu.
6 Basi sasa ninyi, Tatenai, liwali wa ng'ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na hao wenzi wenu wa Kiajemi, mlio ng'ambo ya Mto, jitengeni na mahali pale;
7 iacheni kazi hii ya nyumba ya Mungu, msiizuie; waacheni liwali wa Wayahudi, na wazee wa Wayahudi, waijenge nyumba hii ya Mungu mahali pake.
8 Tena, natoa amri kuwaagiza ninyi mtakayowatendea wazee hao wa Wayahudi, kwa kazi hii ya kuijenga nyumba ya Mungu; katika mali ya mfalme, yaani, katika kodi za nchi iliyo ng'ambo ya Mto, watu hao wapewe gharama zote kwa bidii, ili wasizuiliwe.
9 Na kila kitu wanachokihitaji, katika ng'ombe wachanga, na kondoo waume, na wana-kondoo, kwa sadaka za kuteketezwa watakazomtolea Mungu wa mbinguni, na ngano, na chumvi, na divai, na mafuta, kama makuhani walioko Yerusalemu watakavyosema, na wapewe vitu hivyo vyote siku kwa siku, msikose kuwapa;
10 wapate kumtolea Mungu wa mbinguni sadaka zenye harufu nzuri, na kumwombea mfalme, na wanawe, wapate uzima.
11 Pia nimetoa amri kwamba, mtu awaye yote atakayelibadili neno hili, boriti na itolewe katika nyumba yake, akainuliwe na kutungikwa juu yake; tena nyumba yake ikafanywe jaa kwa ajili ya neno hili.
12 Na Mungu huyu, aliyelifanya jina lake likae pale, na aangamize wafalme wote, na watu wote, watakaonyosha mikono yao kulibadili neno hili, na kuiharibu nyumba hii ya Mungu, iliyoko Yerusalemu. Mimi, Dario, nimetoa amri; na ifanyike kwa bidii nyingi.
13 Ndipo Tatenai, liwali wa ng'ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzi wao, wakafanya hayo kwa bidii, kwa sababu mfalme Dario alikuwa ametuma watu kwao.
14 Nao wazee wa Wayahudi wakajenga, wakafanikiwa, kwa msaada wa kuhubiri kwao Hagai nabii, na Zekaria mwana wa Ido. Wakajenga, wakaimaliza kazi yao, kwa maagizo ya Mungu wa Israeli, na kwa amri ya Koreshi, na Dario, na Artashasta mfalme wa Uajemi.
15 Nyumba hiyo ikamalizika siku ya tatu ya mwezi Adari, katika mwaka wa sita wa kutawala kwake mfalme Dario.
16 Na wana wa Israeli, na makuhani na Walawi, na watu wengine katika hao waliohamishwa, wakaiweka wakfu nyumba ya Mungu kwa furaha.
17 Na katika kuiweka wakfu nyumba ya Mungu, wakatoa sadaka, ng'ombe mia, na kondoo waume mia mbili, na wana-kondoo mia nne; tena wakatoa mbuzi waume kumi na wawili, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli wote, kwa hesabu ya kabila za Israeli.
18 Wakawaweka makuhani katika kura zao, wakawaweka na Walawi katika zamu zao, kwa ajili ya huduma ya Mungu, iliyokuwako Yerusalemu; vile vile kama vilivyoandikwa katika chuo cha Musa.
19 Kisha, wana wa uhamisho wakaifanya Pasaka, mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne ya mwezi.
20 Kwa maana makuhani na Walawi walikuwa wamejitakasa wote pamoja; wote walikuwa hali ya tohara; wakachinja Pasaka kwa ajili ya wana wote wa uhamisho, na kwa ajili ya ndugu zao makuhani, na kwa ajili ya nafsi zao.
21 Wana wa Israeli wakaila, wale waliorudi kuitoka nchi ya uhamisho wao, na watu wote ambao pamoja nao wamejitenga na uchafu wa taifa za nchi, ili kumtaka Bwana, Mungu wa Israeli,
22 wakaifanya sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu kwa furaha, kwa muda wa siku saba; kwa kuwa Bwana amewafurahisha, na kumgeuza moyo mfalme wa Ashuru, awaelekee, ili awatie nguvu mikono yao katika kazi hiyo ya nyumba ya Mungu, Mungu wa Israeli.
NILICHOGUNDUANAKUJIFUNZA:
1. Utaratibu wa kutunza kumbukumbu ulikuwepo tangu zamani. Mwanadamu ana kawaida ya kusahau. Kumbukumbu zilisaidia kubaini ukweli juu ya uhalali wa ujenzi uliokuwa ukiendelea Yerusalemu. Utunzaji wa kumbukumbu husaidia katika kutatua migogoro.
2. Haki ya mtu haiwezi kupotea lakini inaweza kucheleweshwa. Kuna wakati mchakato wa kutafuta haki huwa wa muhimu ili kupata ufumbuzi wa kudumu wa mgogoro uliodumu kwa muda mrefu. Utawala wa Babeli ulitaka kuonesha kuwa unathamini juhudi za watendaji wake katika kuutakia mema utawala wake na unajali pia haki za raia wake. Ubabe katika mazingira hayo usingeweza kuleta suluhu ya kweli.
3. Kuna wakati waliotuhumu hujikuta wakipewa majukumu ya kuwahudumia waliowatuhumu na kuhakikisha wanafanikisha majukumu yao bila kubugudhiwa. Huo ndiyo wakati waliokupiga kibuti hukupigia saluti.
USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: EZRA 5:1-17 JUMAMOSI 25/02/2023
1 Basi manabii, Hagai nabii, na Zekaria mwana wa Ido, wakawafanyia unabii Wayahudi waliokuwako Yerusalemu na Yuda; waliwafanyia unabii kwa jina la Mungu wa Israeli.
2 Ndipo akaondoka Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na Yoshua, mwana wa Yosadaki, wakaanza kuijenga nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu; na pamoja nao walikuwa manabii wa Mungu, wakiwasaidia.
3 Wakati ule ule Tatenai, liwali wa ng'ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzi wao, wakawajia, wakawaambia, Ni nani aliyewapa amri kuijenga nyumba hii, na kuumaliza ukuta huu?
4 Ndipo wakawauliza hivi, Majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani na nani?
5 Lakini jicho la Mungu lilikuwa likiwaelekea wazee wa Wayahudi, hao wasiwazuie, hata habari ile imfikilie Dario, ndipo jawabu litakapopatikana kwa waraka.
6 Hii ndiyo nakala ya waraka waliyompelekea mfalme Dario; na Tatenai, liwali wa ng'ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzake wa Kiajemi, waliokuwako huko ng'ambo ya Mto,
7 walimpelekea waraka nao; na maneno haya yakaandikwa ndani yake; Kwa Dario, mfalme; Salamu sana.
8 Na ajue mfalme ya kuwa sisi tuliingia nchi ya Yuda, tukafika kunako nyumba ya Mungu mkuu, iliyojengwa kwa mawe makubwa, na miti imetiwa katika kuta zake, na kazi hii inaendelea kwa bidii, na kusitawi katika mikono yao.
9 Ndipo tukawauliza wale wazee, tukawaambia hivi, Ni nani aliyewapa amri kuijenga nyumba hii, na kuumaliza ukuta huu?
10 Tukawauliza pia majina yao, ili kukuarifu wewe, tupate kuandika majina ya watu waliokuwa wakubwa wao.
11 Wakatujibu hivi, wakasema, Sisi tu watumishi wa Mungu wa mbingu na nchi, nasi tunaijenga nyumba iliyojengwa zamani sana, yapata miaka mingi, ambayo mfalme mkuu wa Israeli aliijenga na kuimaliza.
12 Lakini hapo baba zetu walipomkasirisha Mungu wa mbingu na nchi, hata akaghadhibika, akawatia katika mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, Mkaldayo, naye ndiye aliyeiharibu nyumba hii, akawachukua watu mateka mpaka Babeli.
13 Lakini katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Babeli, Koreshi, mfalme, alitoa amri ijengwe tena nyumba ya Mungu.
14 Na vyombo vya dhahabu na fedha, vya nyumba ya Mungu, alivyovitoa Nebukadreza katika hekalu lililokuwako Yerusalemu, na kuviingiza katika hekalu la Babeli, vyombo hivyo mfalme Koreshi alivitoa katika hekalu la Babeli, akakabidhiwa mtu, jina lake Sheshbaza, ambaye alikuwa amemfanya liwali;
15 naye akamwambia, Chukua vyombo hivi, uende, ukavitie katika hekalu lililoko Yerusalemu, na nyumba ya Mungu na ijengwe mahali pake.
16 Ndipo ye yule Sheshbaza alipokuja, akaupiga msingi wa nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu; na tangu wakati ule hata leo imekuwa ikijengwa, wala bado haijamalizika.
17 Basi, sasa, mfalme akiona vema, watu na watafute katika nyumba ya hazina ya mfalme, iliyoko huko Babeli, kama ni kweli ya kuwa mfalme Koreshi alitoa amri kuijenga nyumba hiyo ya Mungu katika Yerusalemu, na mfalme akatuletee habari ya mapenzi yake katika jambo hili.
1. Je ukijua haki yako ya kufanya unachofanya na kisha mtu asiye na mamlaka yoyote akakutishia uache kufanya utamsikiliza na kumtii? Je kuna nyakati katika maisha unastahili kuwa mbishi? Yesu aliposema akupigaye shavu la kuume mgeuzie la pili alimaanisha tuwe tayari kuonewa? Je viongozi wa Yuda na Yerusalemu waliposimamishwa kujenga kwa amri ya mfalme Artashasta walipaswa kufanya nini?
2. Viongozi wa kiroho kama manabii walifanya sahihi kuwatia moyo viongozi kuendelea na ujenzi wa hekalu licha ya kusitishwa na mfalme Artashasta? Je, unadhani kuna wakati woga umekwamisha kazi ya Mungu? Kwa nini ujenzi wa nyumba nyingi za ibada unachelewa kukamilika?
3. Waraka uliotumwa kwa mfalme Dario ulisaidia kueleza umuhimu na uhalali wa ujenzi wa hekalu unaoendelea Yerusalemu. Kama wanaoshitaki wanatambua nyumba inayojengwa Yerusalemu ni ya Mungu mkuu kwa nini wanahangaika kushindana naye? Je kuna wakati anayekuchongea hukusaidia kukusafishia njia?
USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: EZRA 4:1-24 IJUMAA 24/02/2023
1 Basi adui za Yuda na Benyamini, waliposikia ya kuwa wana wa uhamisho wanamjengea Bwana, Mungu wa Israeli, hekalu,
2 wakamkaribia Zerubabeli, na wakuu wa mbari za mababa, wakawaambia, Na tujenge sisi nasi pamoja nanyi; kwa maana tunamtafuta Mungu wenu kama ninyi, nasi twamtolea dhabihu tangu zamani za Esar-hadoni, mfalme wa Ashuru, aliyetupandisha mpaka hapa.
3 Lakini Zerubabeli, na Yoshua, na wakuu wengine wa mbari za mababa katika Israeli, wakawaambia, Ninyi haiwahusu kushirikiana nasi katika kumjengea Mungu wetu nyumba; bali sisi wenyewe peke yetu tutamjengea Bwana, Mungu wa Israeli, nyumba, kama mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi, alivyotuamuru.
4 Ndipo watu wa nchi wakaidhoofisha mikono ya watu wa Yuda, wakawasumbua, walipokuwa wakijenga.
5 Wakawaajiri washauri juu yao, ili kuwapinga kusudi lao, siku zote za Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata wakati wa kutawala kwake Dario, mfalme wa Uajemi.
6 Tena, wakati wa kutawala kwake Ahasuero, mwanzo wa kutawala kwake, watu wakaandika mashitaka juu ya wenyeji wa Yuda na Yerusalemu.
7 Na tena, katika siku za Artashasta, Mithredathi, na Tabeeli na mabaki ya wenziwe, wakimwandikia Artashasta, mfalme wa Uajemi, salamu za heri; na mwandiko wa waraka huo, ukaandikwa kwa herufi za Kiaramu, na kunenwa kwa lugha ya Kiaramu.
8 Nao Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, wakaandika waraka juu ya Yerusalemu kwa Artashasta, mfalme, kama hivi;
9 Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, na mabaki ya wenzao, makadhi wa Kiajemi na madiwani wa Kiajemi; na Waarkewi, Wababeli, Washushani, yaani, Waelami;
10 na mabaki ya mataifa, ambao Asur-bani-pali mkuu, mwenye heshima, aliwavusha, na kuwakalisha katika mji wa Samaria, na mahali penginepo, ng'ambo ya Mto; wakadhalika.
11 Hii ndiyo nakili ya waraka waliyompelekea mfalme Artashasta;watumishi wako,watu walio ng`ambo ya mto wakadhalika.
12 Ijulikane kwa mfalme ya kuwa Wayahudi, waliokwea kutoka kwako, wamefika kwetu Yerusalemu; nao wanaujenga ule mji mwasi, mbaya; wamemaliza kuta zake, na kuitengeneza misingi yake.
13 Basi, ijulikane kwa mfalme, ya kuwa mji huu ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hawatatoa kodi, wala ada, wala ushuru, na mwisho wake wafalme watapata hasara.
14 Na sisi, kwa kuwa tunakula chumvi ya nyumba ya mfalme, wala si wajibu wetu kumwona mfalme akivunjiwa heshima, basi tumetuma watu na kumwarifu mfalme.
15 Ili habari zitafutwe katika kitabu cha tarehe za baba zako; ndivyo utakavyopata kujua kwa kitabu cha tarehe ya kuwa mji huo ni mji mwasi, wenye kuwadhuru wafalme, na maliwali, na ya kuwa wenyeji wake wamefanya fitina katika mji huo zamani; ndiyo sababu mji huo ukaangamizwa.
16 Twamwarifu mfalme ya kuwa mji huo ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hutakuwa na sehemu ya nchi ng'ambo ya Mto.
17 Ndipo mfalme akapeleka majibu;Kwa Rehumu,Bwana shauri, na Shimshai,mwandishi na wenzao wengine waliokaa katika Samaria,na penginepo ng`ambo ya mto, Salamu; wakadharika.
18 Ule waraka mlionipelekea umesomwa mbele yangu, nami nikaelewa na maana yake.
19 Nikatoa amri, na watu wametafuta habari; ikaonekana ya kuwa mji huu zamani umefanya fitina juu ya wafalme, na ya kuwa uasi na fitina zimefanyika ndani yake.
20 Tena walikuwako wafalme wakuu juu ya Yerusalemu, waliotawala nchi yote iliyo ng'ambo ya Mto; wakapewa kodi, na ada, na ushuru.
21 Sasa toeni amri kuwakomesha watu hawa kazi yao, mji huu usijengwe, hata mimi nitakapotoa amri.
22 Tena jihadharini, msilegee katika jambo hili; kwa nini madhara yazidi, na wafalme wapate hasara?
23 Hata nakala ya waraka huo wa mfalme Artashasta uliposomwa mbele ya Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, na wenzao, wakaenda Yerusalemu upesi, kwa Wayahudi, wakawakomesha kwa nguvu na kwa kuwashurutisha.
24 Hivyo kazi ya nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu ikakoma; nayo ikakoma hata mwaka wa pili wa kutawala kwake Dario, mfalme wa Uajemi.
1. Kwa nini adui wa Yuda na Benyamini walitaka kushiriki kazi ya ujenzi wa hekalu la Yerusalemu? Kwa nini kazi hiyo wasiifanye wenyewe wakati Yuda na Benjamini wakiwa hawajarudi toka uhamishoni? Hiyo inakufundisha nini juu ya watu usiowajua wanaotaka kukusaidia? Je ni salama siku zote kuwakubalia watu kama hao?
2. Watu waliokuwa wamejitoa kusaidia kujenga hekalu waliwezaje kugeuka na kuanza kuwasumbua waliokuwa wanaendelea kujenga hata kuwadhoofisha? Mchumba anayegeuka kuwa adui mkubwa baada ya kukataliwa hiyo inaashiria alikuwa na upendo mwingi au hakuwa na upendo kabisa?
3. Walioandika mashtaka juu ya wenyeji wa Yuda na Yerusalemu kwa nini hawakufanya hivyo mara tu walipoanza kujenga lakini wakasubiri hadi ujenzi ulipokuwa umeanza kushika kasi? Walioshitaki kuwa mji wa Yerusalemu unaojengwa ni mji mwasi walisahau kwamba watawala hao wa Uajemi ndiyo walioamuru kwamba ujengwe?
4. Je haiwezekani kuwashawishi wengine kuwa wewe ni mtu mwema bila kwanza kuwapaka matope watu wengine? Tabia ya kujipendekeza kwa watawala na kuchongea wengine inatokana na nini? Ukipewa taarifa kuwa mtu fulani ni mbaya wako wajibu wako wa kwanza ni upi? Anayekwamisha kazi ya Mungu kwa tuhuma za uongo Mungu anamchukuliaje?
USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: EZRA 3:1-13 ALHAMISI 23/02/2023
1 Hata ulipowadia mwezi wa saba, na wana wa Israeli walipokuwa katika miji yao, watu wakakusanyika pamoja huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
2 Ndipo akasimama Yoshua, mwana wa Yosadaki, na ndugu zake makuhani, na Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na ndugu zake, nao wakaijenga madhabahu ya Mungu wa Israeli, ili kutoa sadaka za kuteketezwa juu yake, kama ilivyoandikwa katika torati ya Musa, mtu wa Mungu.
3 Wakaiweka madhabahu juu ya msingi wake; maana hofu imewashika kwa sababu ya watu wa nchi; wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa juu yake, sadaka za kuteketezwa za asubuhi na jioni.
4 Wakaishika Sikukuu ya Vibanda, kama ilivyoandikwa, wakatoa sadaka za kuteketezwa za kila siku kwa hesabu yake, kama ilivyoagizwa, kama ilivyopasa kila siku;
5 na baadaye sadaka ya kuteketezwa ya daima, na za mwandamo wa mwezi, na za sikukuu za Bwana, zilizoamriwa na kuwekwa wakfu, na za kila mtu aliyemtolea Bwana sadaka kwa hiari yake.
6 Tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba walianza kumtolea Bwana sadaka za kuteketezwa, lakini msingi wa hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa bado.
7 Tena waliwapa waashi na maseremala fedha; wakawapa watu wa Sidoni, na watu wa Tiro, chakula, na vinywaji, na mafuta, ili walete mierezi kutoka Lebanoni mpaka Yafa kwa njia ya bahari, kwa kadiri walivyopewa ruhusa na Koreshi, mfalme wa Uajemi.
8 Hata mwaka wa pili wa kufika kwao nyumbani kwa Mungu, huko Yerusalemu, mwezi wa pili, Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na Yoshua, mwana wa Yosadaki, na ndugu zao wengine, makuhani na Walawi, na watu wote, waliotoka katika uhamisho na kufika Yerusalemu, wakaanza; nao wakawaweka Walawi, hao wenye miaka ishirini na waliozidi, ili kuisimamia kazi ya nyumba ya Bwana.
9 Ndipo wakasimama Yeshua, na wanawe na ndugu zake, Kadmieli, na wanawe, wana wa Hodavia, pamoja, ili kuwasimamia hao wafanyao kazi katika nyumba ya Mungu; wana wa Henadadi, pamoja na wana wao, na ndugu zao, Walawi.
10 Hata wajenzi walipouweka msingi wa hekalu la Bwana, wakawaweka makuhani, wamevaa mavazi yao, wenye baragumu, na Walawi, wana wa Asafu, wenye matoazi, ili wamhimidi Bwana, kama alivyoagiza Daudi, mfalme wa Israeli.
11 Wakaimbiana, wakimhimidi Bwana, na kumshukuru, wakasema, Kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake kwa Israeli ni za milele. Kisha watu wote wakapaza sauti zao, na kupiga kelele, walipomhimidi Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana umekwisha kuwekwa.
12 Bali makuhani wengi, na Walawi, na wakuu wa mbari za mababa, waliokuwa wameiona nyumba ya kwanza, wakati msingi wa nyumba hii ulipowekwa mbele ya macho yao, walilia kwa sauti kuu; na watu wengi walipiga kelele za furaha;
13 hata watu wasiweze kupambanua kelele za furaha, na kelele za vilio vya watu; maana watu walipiga kelele kwa sauti kuu, na kelele zao zikasikilikana mbali sana.
1. Kukusanyika pamoja kama mtu mmoja kunamaanisha nini? Unadhani ni nini kiliwashika hata wakakusanyika pamoja kama mtu mmoja? Kwa nini walitangulia kumtolea Bwana sadaka kabla hawajaweka msingi wa hekalu? Je ni kwa nini Koreshi aliendelea kuhusika na ujenzi wa hekalu la Yerusalemu?
2. Kwa nini waliotoka uhamishoni walianza kumtolea Bwana sadaka siku ya kwanza ya mwezi wa saba? Kwa nini Yerusalemu panaitwa nyumbani kwa Mungu? Kwa nini watakaokombolewa wanatambuliwa kama watu wa nyumbani mwake Mungu (Waefeso 2:19)? Kwa nini kazi ya usimamamizi wa nyumba ya Bwana ilihitaji Walawi wenye miaka ishirini au zaidi?
3. Kwa nini nyimbo za kusifu zinapatikana zaidi kwenye nyimbo zetu za vitabuni kuliko katika nyimbo za kwaya zetu za makanisani? Je kusifu kumepitwa na wakati? Kumhimidi Bwana kwa kupaza sauti na kupiga kelele kuna umuhimu gani katika uimbaji? Kwa nini kwenye ujenzi wa nyumba ya Mungu huwepo wale wenye kupaza sauti kwa furaha na wale wenye kupaza sauti kwa huzuni?
USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: EZRA 2:1-70 JUMATANO 21/02/2023
1 Basi hawa ndio wana wa wilaya, waliokwea kutoka katika ule uhamisho wa hao waliokuwa wamechukuliwa, ambao Nebukadneza, mfalme wa Babeli, aliwachukua mateka mpaka Babeli, nao wakarudi Yerusalemu na Yuda, kila mtu mjini kwake;
2 ndio hawa waliokuja pamoja na Zerubabeli, Yoshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu, na Baana. Hii ndiyo hesabu ya wanaume wa watu wa Israeli;
3 wana wa Paroshi, elfu mbili mia moja sabini na wawili.
4 Wana wa Shefatia, mia tatu sabini na wawili.
5 Wana wa Ara, mia saba sabini na watano.
6 Wana wa Pahath-Moabu, wa wana wa Yeshua na Yoabu, elfu mbili mia nane na kumi na wawili.
7 Wana wa Elamu, elfu moja mia mbili hamsini na wanne.
8 Wana wa Zatu, mia kenda arobaini na watano.
9 Wana wa Zakai, mia saba na sitini.
10 Wana wa Binui, mia sita arobaini na wawili.
11 Wana wa Bebai, mia sita ishirini na watatu.
12 Wana wa Azgadi, elfu moja mia mbili ishirini na wawili.
13 Wana wa Adonikamu, mia sita sitini na sita.
14 Wana wa Bigwai, elfu mbili hamsini na sita.
15 Wana wa Adini, mia nne hamsini na wanne.
16 Wana wa Ateri, wa wana wa Hezekia, tisini na wanane.
17 Wana wa Besai, mia tatu ishirini na watatu.
18 Wana wa Harifu, mia moja na kumi na wawili.
19 Wana wa Hashumu, mia mbili ishirini na watatu.
20 Watu wa Gibeoni, tisini na watano.
21 Watu wa Bethlehemu, mia ishirini na watatu.
22 Watu wa Netofa, hamsini na sita.
23 Watu wa Anathothi, mia ishirini na wanane.
24 Watu wa Beth-Azmawethi, arobaini na wawili.
25 Watu wa Kiriath-yearimu, na Kefira, na Beerothi, mia saba arobaini na watatu.
26 Watu wa Rama na Geba, mia sita ishirini na mmoja.
27 Watu wa Mikmashi, mia moja ishirini na wawili.
28 Watu wa Betheli, na Ai, mia mbili ishirini na watatu.
29 Watu wa Nebo, hamsini na wawili.
30 Watu wa Magbishi, mia moja hamsini na sita.
31 Watu wa Elamu wa pili, elfu moja mia mbili hamsini na wanne.
32 Watu wa Harimu, mia tatu na ishirini.
33 Watu wa Lodi, na Hadidi, na Ono, mia saba ishirini na watano.
34 Watu wa Yeriko, mia tatu arobaini na watano.
35 Watu wa Senaa, elfu tatu mia sita na thelathini.
36 Makuhani; wana wa Yedaya, wa mbari ya Yeshua, mia kenda sabini na watatu.
37 Wana wa Imeri, elfu moja hamsini na wawili.
38 Wana wa Pashuri, elfu moja mia mbili arobaini na saba.
39 Wana wa Harimu, elfu moja na kumi na saba.
40 Walawi; wana wa Yeshua, na wana wa Kadmieli wa wana wa Hodavia, sabini na wanne.
41 Waimbaji; wana wa Asafu, mia moja ishirini na wanane.
42 Akina bawabu; wana wa Shalumu, wana wa Ateri, wana wa Talmoni, wana wa Akubu, wana wa Hatita, wana wa Shobai; jumla yao ni mia moja thelathini na kenda.
43 Wanethini; wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi;
44 wana wa Kerosi, wana wa Siaha, wana wa Padoni;
45 wana wa Lebana, wana wa Hagaba, wana wa Akubu;
46 wana wa Hagabu, wana wa Salmai, wana wa Hanani;
47 wana wa Gideli, wana wa Gahari, wana wa Reaya;
48 wana wa Resini, wana wa Nekoda, wana wa Gazamu;
49 wana wa Uza, wana wa Pasea, wana wa Besai;
50 wana wa Asna, wana wa Meunimu, wana wa Nefusimu;
51 wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri;
52 wana wa Basluthi, wana wa Mehida, wana wa Harsha;
53 wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema;
54 wana wa Nesia, wana wa Hatifa.
55 Wa watumwa wa Sulemani; wana wa Sotai, wana wa Soferethi, wana wa Peruda;
56 wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli;
57 wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokereth-Sebaimu, wana wa Amoni.
58 Wanethini wote, pamoja na watumwa wa Sulemani, walikuwa mia tatu tisini na wawili.
59 Na hawa ndio watu waliokwea kutoka Tel-mela, na Tel-harsha, na Kerubu, na Adani, na Imeri; walakini hawakuweza kuonyesha mbari za baba zao, wala kizazi chao, kwamba walikuwa wa Israeli;
60 wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda, mia sita hamsini na wawili.
61 Tena wa makuhani; wana wa Habaya, wana wa Hakosi, wana wa Barzilai, yule aliyeoa mmojawapo wa binti Barzilai, Mgileadi, akaitwa kwa jina lao.
62 Hao waliitafuta orodha yao miongoni mwa wale waliohesabiwa kwa nasaba, wasionekane; kwa hiyo walihesabiwa kuwa na unajisi.
63 Na huyo Tirshatha akawaambia wasile katika vitu vitakatifu sana ,hata atakaposimama kuhani mwenye urimu na Thumimu.
64 Basi hilo kusanyiko lote zima, jumla yake ilikuwa watu arobaini na mbili elfu na mia tatu na sitini,
65 tena, zaidi ya hao, kulikuwa na watumishi wao waume kwa wake, ambao walikuwa saba elfu, na mia tatu na thelathini na saba; nao walikuwa na waimbaji waume kwa wake mia mbili.
66 Farasi zao walikuwa mia saba thelathini na sita; nyumbu zao, mia mbili arobaini na watano;
67 ngamia zao, mia nne thelathini na watano; punda zao elfu sita, na mia saba na ishirini.
68 Na baadhi ya wakuu wa mbari za baba zao, hapo walipoifikilia nyumba ya Bwana, iliyoko Yerusalemu, walitoa mali kwa ukarimu kwa ajili ya nyumba ya Mungu, ili kuisimamisha mahali pake;
69 wakatoa kadiri walivyoweza, na kutia katika hazina ya kazi hiyo, darkoni za dhahabu sitini na moja elfu ,na nane za fedha elfu tano,na mavazi mia ya makuhani.
70 Hivyo makuhani, na Walawi, na baadhi ya watu, na waimbaji, na mabawabu, na Wanethini, wakakaa mijini mwao, naam, Israeli wote wakakaa mijini mwao.
1. Unadhani Mungu aliruhusu Wayahudi waende utumwani Babeli ili wakafundishe au wakafundishwe au yote mawili? Unadhani wanadamu baada ya kukaa kwenye dunia ya dhambi kwa takribani miaka 1,000 tumekuwa bora zaidi kuliko tulivyokuwa kabla ya dhambi? Je Mungu alipata faida yoyote kwa Wayahudi kukaa uhamishoni Babeli? Je Mungu anawachukuliaje wale wanaowalea watu wake walio kwenye mazizi mengine (vikundi vya dini) yanayopotosha ukweli wake? (Yohana 10:16).
2. Unadhani kuhesabiwa kwa watu kulilenga kubaini wenye nasaba ya Yuda na wanaostahili kurudi Yuda? Kulikuwa na hatari gani kama wasingehesabiwa? Je mtu aweza kuwa na watumishi wa kike na wa kiume na hali yeye mwenyewe akiwa mtumwa? Kwa nini watumwa waliokuwako Babeli walianza kubaguana walipokuwa wanakaribia kurejea nyumbani? Unaona hiyo ikijitokeza kwenye kanisa lako?
USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: 2 NYAKATI 36:1-23 JUMATATU 20/02/2023