Seventh-day Adventist® Church

PASTOR LETTA'S OFFICIAL WEBSITE

Menu

USOMAJI BILIA KWA MPANGO

USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: EZRA 6:1-22 JUMAPILI 26/02/2023

1 Ndipo mfalme Dario akatoa amri, na watu wakatafuta katika nyumba ya vyuo vya tarehe, hapo akiba zilipowekwa katika Babeli.
2 Na chuo kimoja kilipatikana huko Akmetha, katika nyumba ya mfalme iliyo katika wilaya ya Umedi, na ndani yake maneno haya yameandikwa ili yakumbukwe.
3 Katika mwaka wa kwanza wa mfalme Koreshi, mfalme Koreshi alitoa amri, Kwa habari ya nyumba ya Mungu huko Yerusalemu, nyumba hiyo na ijengwe, mahali watoapo dhabihu, na misingi yake ipigwe na kufanywa imara sana; kuinuka kwake kuwe mikono sitini, na upana wake mikono sitini;
4 ziwepo safu tatu za mawe makubwa, na safu moja ya miti mipya; gharama zake zitolewe katika nyumba ya mfalme.
5 Na vyombo vya dhahabu na fedha, vya nyumba ya Mungu, ambavyo mfalme Nebukadreza alivitoa katika nyumba ya Mungu, iliyoko Yerusalemu, akavileta mpaka Babeli, na virudishwe, vikaingizwe tena katika hekalu lililoko Yerusalemu, kila kimoja mahali pake, na wewe uvitie katika nyumba ya Mungu.
6 Basi sasa ninyi, Tatenai, liwali wa ng'ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na hao wenzi wenu wa Kiajemi, mlio ng'ambo ya Mto, jitengeni na mahali pale;
7 iacheni kazi hii ya nyumba ya Mungu, msiizuie; waacheni liwali wa Wayahudi, na wazee wa Wayahudi, waijenge nyumba hii ya Mungu mahali pake.
8 Tena, natoa amri kuwaagiza ninyi mtakayowatendea wazee hao wa Wayahudi, kwa kazi hii ya kuijenga nyumba ya Mungu; katika mali ya mfalme, yaani, katika kodi za nchi iliyo ng'ambo ya Mto, watu hao wapewe gharama zote kwa bidii, ili wasizuiliwe.
9 Na kila kitu wanachokihitaji, katika ng'ombe wachanga, na kondoo waume, na wana-kondoo, kwa sadaka za kuteketezwa watakazomtolea Mungu wa mbinguni, na ngano, na chumvi, na divai, na mafuta, kama makuhani walioko Yerusalemu watakavyosema, na wapewe vitu hivyo vyote siku kwa siku, msikose kuwapa;
10 wapate kumtolea Mungu wa mbinguni sadaka zenye harufu nzuri, na kumwombea mfalme, na wanawe, wapate uzima.
11 Pia nimetoa amri kwamba, mtu awaye yote atakayelibadili neno hili, boriti na itolewe katika nyumba yake, akainuliwe na kutungikwa juu yake; tena nyumba yake ikafanywe jaa kwa ajili ya neno hili.
12 Na Mungu huyu, aliyelifanya jina lake likae pale, na aangamize wafalme wote, na watu wote, watakaonyosha mikono yao kulibadili neno hili, na kuiharibu nyumba hii ya Mungu, iliyoko Yerusalemu. Mimi, Dario, nimetoa amri; na ifanyike kwa bidii nyingi.
13 Ndipo Tatenai, liwali wa ng'ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzi wao, wakafanya hayo kwa bidii, kwa sababu mfalme Dario alikuwa ametuma watu kwao.
14 Nao wazee wa Wayahudi wakajenga, wakafanikiwa, kwa msaada wa kuhubiri kwao Hagai nabii, na Zekaria mwana wa Ido. Wakajenga, wakaimaliza kazi yao, kwa maagizo ya Mungu wa Israeli, na kwa amri ya Koreshi, na Dario, na Artashasta mfalme wa Uajemi.
15 Nyumba hiyo ikamalizika siku ya tatu ya mwezi Adari, katika mwaka wa sita wa kutawala kwake mfalme Dario.
16 Na wana wa Israeli, na makuhani na Walawi, na watu wengine katika hao waliohamishwa, wakaiweka wakfu nyumba ya Mungu kwa furaha.
17 Na katika kuiweka wakfu nyumba ya Mungu, wakatoa sadaka, ng'ombe mia, na kondoo waume mia mbili, na wana-kondoo mia nne; tena wakatoa mbuzi waume kumi na wawili, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya Israeli wote, kwa hesabu ya kabila za Israeli.
18 Wakawaweka makuhani katika kura zao, wakawaweka na Walawi katika zamu zao, kwa ajili ya huduma ya Mungu, iliyokuwako Yerusalemu; vile vile kama vilivyoandikwa katika chuo cha Musa.
19 Kisha, wana wa uhamisho wakaifanya Pasaka, mwezi wa kwanza siku ya kumi na nne ya mwezi.
20 Kwa maana makuhani na Walawi walikuwa wamejitakasa wote pamoja; wote walikuwa hali ya tohara; wakachinja Pasaka kwa ajili ya wana wote wa uhamisho, na kwa ajili ya ndugu zao makuhani, na kwa ajili ya nafsi zao.
21 Wana wa Israeli wakaila, wale waliorudi kuitoka nchi ya uhamisho wao, na watu wote ambao pamoja nao wamejitenga na uchafu wa taifa za nchi, ili kumtaka Bwana, Mungu wa Israeli,
22 wakaifanya sikukuu ya mikate isiyotiwa chachu kwa furaha, kwa muda wa siku saba; kwa kuwa Bwana amewafurahisha, na kumgeuza moyo mfalme wa Ashuru, awaelekee, ili awatie nguvu mikono yao katika kazi hiyo ya nyumba ya Mungu, Mungu wa Israeli.

NILICHOGUNDUANAKUJIFUNZA:

1. Utaratibu wa kutunza kumbukumbu ulikuwepo tangu zamani. Mwanadamu ana kawaida ya kusahau. Kumbukumbu zilisaidia kubaini ukweli juu ya uhalali wa ujenzi uliokuwa ukiendelea Yerusalemu. Utunzaji wa kumbukumbu husaidia katika kutatua migogoro.
2. Haki ya mtu haiwezi kupotea lakini inaweza kucheleweshwa. Kuna wakati mchakato wa kutafuta haki huwa wa muhimu ili kupata ufumbuzi wa kudumu wa mgogoro uliodumu kwa muda mrefu. Utawala wa Babeli ulitaka kuonesha kuwa unathamini juhudi za watendaji wake katika kuutakia mema utawala wake na unajali pia haki za raia wake. Ubabe katika mazingira hayo usingeweza kuleta suluhu ya kweli.
3. Kuna wakati waliotuhumu hujikuta wakipewa majukumu ya kuwahudumia waliowatuhumu na kuhakikisha wanafanikisha majukumu yao bila kubugudhiwa. Huo ndiyo wakati waliokupiga kibuti hukupigia saluti.


USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: EZRA 5:1-17 JUMAMOSI 25/02/2023


1 Basi manabii, Hagai nabii, na Zekaria mwana wa Ido, wakawafanyia unabii Wayahudi waliokuwako Yerusalemu na Yuda; waliwafanyia unabii kwa jina la Mungu wa Israeli.
2 Ndipo akaondoka Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na Yoshua, mwana wa Yosadaki, wakaanza kuijenga nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu; na pamoja nao walikuwa manabii wa Mungu, wakiwasaidia.
3 Wakati ule ule Tatenai, liwali wa ng'ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzi wao, wakawajia, wakawaambia, Ni nani aliyewapa amri kuijenga nyumba hii, na kuumaliza ukuta huu?
4 Ndipo wakawauliza hivi, Majina ya watu wanaofanya ujenzi huu ni nani na nani?
5 Lakini jicho la Mungu lilikuwa likiwaelekea wazee wa Wayahudi, hao wasiwazuie, hata habari ile imfikilie Dario, ndipo jawabu litakapopatikana kwa waraka.
6 Hii ndiyo nakala ya waraka waliyompelekea mfalme Dario; na Tatenai, liwali wa ng'ambo ya Mto, na Shethar-Bozenai, na wenzake wa Kiajemi, waliokuwako huko ng'ambo ya Mto,
7 walimpelekea waraka nao; na maneno haya yakaandikwa ndani yake; Kwa Dario, mfalme; Salamu sana.
8 Na ajue mfalme ya kuwa sisi tuliingia nchi ya Yuda, tukafika kunako nyumba ya Mungu mkuu, iliyojengwa kwa mawe makubwa, na miti imetiwa katika kuta zake, na kazi hii inaendelea kwa bidii, na kusitawi katika mikono yao.
9 Ndipo tukawauliza wale wazee, tukawaambia hivi, Ni nani aliyewapa amri kuijenga nyumba hii, na kuumaliza ukuta huu?
10 Tukawauliza pia majina yao, ili kukuarifu wewe, tupate kuandika majina ya watu waliokuwa wakubwa wao.
11 Wakatujibu hivi, wakasema, Sisi tu watumishi wa Mungu wa mbingu na nchi, nasi tunaijenga nyumba iliyojengwa zamani sana, yapata miaka mingi, ambayo mfalme mkuu wa Israeli aliijenga na kuimaliza.
12 Lakini hapo baba zetu walipomkasirisha Mungu wa mbingu na nchi, hata akaghadhibika, akawatia katika mkono wa Nebukadreza, mfalme wa Babeli, Mkaldayo, naye ndiye aliyeiharibu nyumba hii, akawachukua watu mateka mpaka Babeli.
13 Lakini katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Babeli, Koreshi, mfalme, alitoa amri ijengwe tena nyumba ya Mungu.
14 Na vyombo vya dhahabu na fedha, vya nyumba ya Mungu, alivyovitoa Nebukadreza katika hekalu lililokuwako Yerusalemu, na kuviingiza katika hekalu la Babeli, vyombo hivyo mfalme Koreshi alivitoa katika hekalu la Babeli, akakabidhiwa mtu, jina lake Sheshbaza, ambaye alikuwa amemfanya liwali;
15 naye akamwambia, Chukua vyombo hivi, uende, ukavitie katika hekalu lililoko Yerusalemu, na nyumba ya Mungu na ijengwe mahali pake.
16 Ndipo ye yule Sheshbaza alipokuja, akaupiga msingi wa nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu; na tangu wakati ule hata leo imekuwa ikijengwa, wala bado haijamalizika.
17 Basi, sasa, mfalme akiona vema, watu na watafute katika nyumba ya hazina ya mfalme, iliyoko huko Babeli, kama ni kweli ya kuwa mfalme Koreshi alitoa amri kuijenga nyumba hiyo ya Mungu katika Yerusalemu, na mfalme akatuletee habari ya mapenzi yake katika jambo hili.

MASWALI YA KUJADILI:

1. Je ukijua haki yako ya kufanya unachofanya na kisha mtu asiye na mamlaka yoyote akakutishia uache kufanya utamsikiliza na kumtii? Je kuna nyakati katika maisha unastahili kuwa mbishi? Yesu aliposema akupigaye shavu la kuume mgeuzie la pili alimaanisha tuwe tayari kuonewa? Je viongozi wa Yuda na Yerusalemu waliposimamishwa kujenga kwa amri ya mfalme Artashasta walipaswa kufanya nini?
2. Viongozi wa kiroho kama manabii walifanya sahihi kuwatia moyo viongozi kuendelea na ujenzi wa hekalu licha ya kusitishwa na mfalme Artashasta? Je, unadhani kuna wakati woga umekwamisha kazi ya Mungu? Kwa nini ujenzi wa nyumba nyingi za ibada unachelewa kukamilika?
3. Waraka uliotumwa kwa mfalme Dario ulisaidia kueleza umuhimu na uhalali wa ujenzi wa hekalu unaoendelea Yerusalemu. Kama wanaoshitaki wanatambua nyumba inayojengwa Yerusalemu ni ya Mungu mkuu kwa nini wanahangaika kushindana naye? Je kuna wakati anayekuchongea hukusaidia kukusafishia njia?

USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: EZRA 4:1-24 IJUMAA 24/02/2023


1 Basi adui za Yuda na Benyamini, waliposikia ya kuwa wana wa uhamisho wanamjengea Bwana, Mungu wa Israeli, hekalu,
2 wakamkaribia Zerubabeli, na wakuu wa mbari za mababa, wakawaambia, Na tujenge sisi nasi pamoja nanyi; kwa maana tunamtafuta Mungu wenu kama ninyi, nasi twamtolea dhabihu tangu zamani za Esar-hadoni, mfalme wa Ashuru, aliyetupandisha mpaka hapa.
3 Lakini Zerubabeli, na Yoshua, na wakuu wengine wa mbari za mababa katika Israeli, wakawaambia, Ninyi haiwahusu kushirikiana nasi katika kumjengea Mungu wetu nyumba; bali sisi wenyewe peke yetu tutamjengea Bwana, Mungu wa Israeli, nyumba, kama mfalme Koreshi, mfalme wa Uajemi, alivyotuamuru.
4 Ndipo watu wa nchi wakaidhoofisha mikono ya watu wa Yuda, wakawasumbua, walipokuwa wakijenga.
5 Wakawaajiri washauri juu yao, ili kuwapinga kusudi lao, siku zote za Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata wakati wa kutawala kwake Dario, mfalme wa Uajemi.
6 Tena, wakati wa kutawala kwake Ahasuero, mwanzo wa kutawala kwake, watu wakaandika mashitaka juu ya wenyeji wa Yuda na Yerusalemu.
7 Na tena, katika siku za Artashasta, Mithredathi, na Tabeeli na mabaki ya wenziwe, wakimwandikia Artashasta, mfalme wa Uajemi, salamu za heri; na mwandiko wa waraka huo, ukaandikwa kwa herufi za Kiaramu, na kunenwa kwa lugha ya Kiaramu.
8 Nao Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, wakaandika waraka juu ya Yerusalemu kwa Artashasta, mfalme, kama hivi;
9 Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, na mabaki ya wenzao, makadhi wa Kiajemi na madiwani wa Kiajemi; na Waarkewi, Wababeli, Washushani, yaani, Waelami;
10 na mabaki ya mataifa, ambao Asur-bani-pali mkuu, mwenye heshima, aliwavusha, na kuwakalisha katika mji wa Samaria, na mahali penginepo, ng'ambo ya Mto; wakadhalika.
11 Hii ndiyo nakili ya waraka waliyompelekea mfalme Artashasta;watumishi wako,watu walio ng`ambo ya mto wakadhalika.
12 Ijulikane kwa mfalme ya kuwa Wayahudi, waliokwea kutoka kwako, wamefika kwetu Yerusalemu; nao wanaujenga ule mji mwasi, mbaya; wamemaliza kuta zake, na kuitengeneza misingi yake.
13 Basi, ijulikane kwa mfalme, ya kuwa mji huu ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hawatatoa kodi, wala ada, wala ushuru, na mwisho wake wafalme watapata hasara.
14 Na sisi, kwa kuwa tunakula chumvi ya nyumba ya mfalme, wala si wajibu wetu kumwona mfalme akivunjiwa heshima, basi tumetuma watu na kumwarifu mfalme.
15 Ili habari zitafutwe katika kitabu cha tarehe za baba zako; ndivyo utakavyopata kujua kwa kitabu cha tarehe ya kuwa mji huo ni mji mwasi, wenye kuwadhuru wafalme, na maliwali, na ya kuwa wenyeji wake wamefanya fitina katika mji huo zamani; ndiyo sababu mji huo ukaangamizwa.
16 Twamwarifu mfalme ya kuwa mji huo ukijengwa, na kuta zake zikimalizika, hutakuwa na sehemu ya nchi ng'ambo ya Mto.
17 Ndipo mfalme akapeleka majibu;Kwa Rehumu,Bwana shauri, na Shimshai,mwandishi na wenzao wengine waliokaa katika Samaria,na penginepo ng`ambo ya mto, Salamu; wakadharika.
18 Ule waraka mlionipelekea umesomwa mbele yangu, nami nikaelewa na maana yake.
19 Nikatoa amri, na watu wametafuta habari; ikaonekana ya kuwa mji huu zamani umefanya fitina juu ya wafalme, na ya kuwa uasi na fitina zimefanyika ndani yake.
20 Tena walikuwako wafalme wakuu juu ya Yerusalemu, waliotawala nchi yote iliyo ng'ambo ya Mto; wakapewa kodi, na ada, na ushuru.
21 Sasa toeni amri kuwakomesha watu hawa kazi yao, mji huu usijengwe, hata mimi nitakapotoa amri.
22 Tena jihadharini, msilegee katika jambo hili; kwa nini madhara yazidi, na wafalme wapate hasara?
23 Hata nakala ya waraka huo wa mfalme Artashasta uliposomwa mbele ya Rehumu, Bwana shauri, na Shimshai, mwandishi, na wenzao, wakaenda Yerusalemu upesi, kwa Wayahudi, wakawakomesha kwa nguvu na kwa kuwashurutisha.
24 Hivyo kazi ya nyumba ya Mungu iliyoko Yerusalemu ikakoma; nayo ikakoma hata mwaka wa pili wa kutawala kwake Dario, mfalme wa Uajemi.

MASWALI YA KUJADILI:

1. Kwa nini adui wa Yuda na Benyamini walitaka kushiriki kazi ya ujenzi wa hekalu la Yerusalemu? Kwa nini kazi hiyo wasiifanye wenyewe wakati Yuda na Benjamini wakiwa hawajarudi toka uhamishoni? Hiyo inakufundisha nini juu ya watu usiowajua wanaotaka kukusaidia? Je ni salama siku zote kuwakubalia watu kama hao?
2. Watu waliokuwa wamejitoa kusaidia kujenga hekalu waliwezaje kugeuka na kuanza kuwasumbua waliokuwa wanaendelea kujenga hata kuwadhoofisha? Mchumba anayegeuka kuwa adui mkubwa baada ya kukataliwa hiyo inaashiria alikuwa na upendo mwingi au hakuwa na upendo kabisa?
3. Walioandika mashtaka juu ya wenyeji wa Yuda na Yerusalemu kwa nini hawakufanya hivyo mara tu walipoanza kujenga lakini wakasubiri hadi ujenzi ulipokuwa umeanza kushika kasi? Walioshitaki kuwa mji wa Yerusalemu unaojengwa ni mji mwasi walisahau kwamba watawala hao wa Uajemi ndiyo walioamuru kwamba ujengwe?
4. Je haiwezekani kuwashawishi wengine kuwa wewe ni mtu mwema bila kwanza kuwapaka matope watu wengine? Tabia ya kujipendekeza kwa watawala na kuchongea wengine inatokana na nini? Ukipewa taarifa kuwa mtu fulani ni mbaya wako wajibu wako wa kwanza ni upi? Anayekwamisha kazi ya Mungu kwa tuhuma za uongo Mungu anamchukuliaje?


USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: EZRA 3:1-13 ALHAMISI 23/02/2023


1 Hata ulipowadia mwezi wa saba, na wana wa Israeli walipokuwa katika miji yao, watu wakakusanyika pamoja huko Yerusalemu kama mtu mmoja.
2 Ndipo akasimama Yoshua, mwana wa Yosadaki, na ndugu zake makuhani, na Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na ndugu zake, nao wakaijenga madhabahu ya Mungu wa Israeli, ili kutoa sadaka za kuteketezwa juu yake, kama ilivyoandikwa katika torati ya Musa, mtu wa Mungu.
3 Wakaiweka madhabahu juu ya msingi wake; maana hofu imewashika kwa sababu ya watu wa nchi; wakamtolea Bwana sadaka za kuteketezwa juu yake, sadaka za kuteketezwa za asubuhi na jioni.
4 Wakaishika Sikukuu ya Vibanda, kama ilivyoandikwa, wakatoa sadaka za kuteketezwa za kila siku kwa hesabu yake, kama ilivyoagizwa, kama ilivyopasa kila siku;
5 na baadaye sadaka ya kuteketezwa ya daima, na za mwandamo wa mwezi, na za sikukuu za Bwana, zilizoamriwa na kuwekwa wakfu, na za kila mtu aliyemtolea Bwana sadaka kwa hiari yake.
6 Tangu siku ya kwanza ya mwezi wa saba walianza kumtolea Bwana sadaka za kuteketezwa, lakini msingi wa hekalu la Bwana ulikuwa haujawekwa bado.
7 Tena waliwapa waashi na maseremala fedha; wakawapa watu wa Sidoni, na watu wa Tiro, chakula, na vinywaji, na mafuta, ili walete mierezi kutoka Lebanoni mpaka Yafa kwa njia ya bahari, kwa kadiri walivyopewa ruhusa na Koreshi, mfalme wa Uajemi.
8 Hata mwaka wa pili wa kufika kwao nyumbani kwa Mungu, huko Yerusalemu, mwezi wa pili, Zerubabeli, mwana wa Shealtieli, na Yoshua, mwana wa Yosadaki, na ndugu zao wengine, makuhani na Walawi, na watu wote, waliotoka katika uhamisho na kufika Yerusalemu, wakaanza; nao wakawaweka Walawi, hao wenye miaka ishirini na waliozidi, ili kuisimamia kazi ya nyumba ya Bwana.
9 Ndipo wakasimama Yeshua, na wanawe na ndugu zake, Kadmieli, na wanawe, wana wa Hodavia, pamoja, ili kuwasimamia hao wafanyao kazi katika nyumba ya Mungu; wana wa Henadadi, pamoja na wana wao, na ndugu zao, Walawi.
10 Hata wajenzi walipouweka msingi wa hekalu la Bwana, wakawaweka makuhani, wamevaa mavazi yao, wenye baragumu, na Walawi, wana wa Asafu, wenye matoazi, ili wamhimidi Bwana, kama alivyoagiza Daudi, mfalme wa Israeli.
11 Wakaimbiana, wakimhimidi Bwana, na kumshukuru, wakasema, Kwa kuwa ni mwema, kwa maana fadhili zake kwa Israeli ni za milele. Kisha watu wote wakapaza sauti zao, na kupiga kelele, walipomhimidi Bwana, kwa sababu msingi wa nyumba ya Bwana umekwisha kuwekwa.
12 Bali makuhani wengi, na Walawi, na wakuu wa mbari za mababa, waliokuwa wameiona nyumba ya kwanza, wakati msingi wa nyumba hii ulipowekwa mbele ya macho yao, walilia kwa sauti kuu; na watu wengi walipiga kelele za furaha;
13 hata watu wasiweze kupambanua kelele za furaha, na kelele za vilio vya watu; maana watu walipiga kelele kwa sauti kuu, na kelele zao zikasikilikana mbali sana.

MASWALI YA KUJADILI:

1. Kukusanyika pamoja kama mtu mmoja kunamaanisha nini? Unadhani ni nini kiliwashika hata wakakusanyika pamoja kama mtu mmoja? Kwa nini walitangulia kumtolea Bwana sadaka kabla hawajaweka msingi wa hekalu? Je ni kwa nini Koreshi aliendelea kuhusika na ujenzi wa hekalu la Yerusalemu?
2. Kwa nini waliotoka uhamishoni walianza kumtolea Bwana sadaka siku ya kwanza ya mwezi wa saba? Kwa nini Yerusalemu panaitwa nyumbani kwa Mungu? Kwa nini watakaokombolewa wanatambuliwa kama watu wa nyumbani mwake Mungu (Waefeso 2:19)? Kwa nini kazi ya usimamamizi wa nyumba ya Bwana ilihitaji Walawi wenye miaka ishirini au zaidi?
3. Kwa nini nyimbo za kusifu zinapatikana zaidi kwenye nyimbo zetu za vitabuni kuliko katika nyimbo za kwaya zetu za makanisani? Je kusifu kumepitwa na wakati? Kumhimidi Bwana kwa kupaza sauti na kupiga kelele kuna umuhimu gani katika uimbaji? Kwa nini kwenye ujenzi wa nyumba ya Mungu huwepo wale wenye kupaza sauti kwa furaha na wale wenye kupaza sauti kwa huzuni?

USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: EZRA 2:1-70 JUMATANO 21/02/2023

1 Basi hawa ndio wana wa wilaya, waliokwea kutoka katika ule uhamisho wa hao waliokuwa wamechukuliwa, ambao Nebukadneza, mfalme wa Babeli, aliwachukua mateka mpaka Babeli, nao wakarudi Yerusalemu na Yuda, kila mtu mjini kwake;
2 ndio hawa waliokuja pamoja na Zerubabeli, Yoshua, Nehemia, Seraya, Reelaya, Mordekai, Bilshani, Mispari, Bigwai, Rehumu, na Baana. Hii ndiyo hesabu ya wanaume wa watu wa Israeli;
3 wana wa Paroshi, elfu mbili mia moja sabini na wawili.
4 Wana wa Shefatia, mia tatu sabini na wawili.
5 Wana wa Ara, mia saba sabini na watano.
6 Wana wa Pahath-Moabu, wa wana wa Yeshua na Yoabu, elfu mbili mia nane na kumi na wawili.
7 Wana wa Elamu, elfu moja mia mbili hamsini na wanne.
8 Wana wa Zatu, mia kenda arobaini na watano.
9 Wana wa Zakai, mia saba na sitini.
10 Wana wa Binui, mia sita arobaini na wawili.
11 Wana wa Bebai, mia sita ishirini na watatu.
12 Wana wa Azgadi, elfu moja mia mbili ishirini na wawili.
13 Wana wa Adonikamu, mia sita sitini na sita.
14 Wana wa Bigwai, elfu mbili hamsini na sita.
15 Wana wa Adini, mia nne hamsini na wanne.
16 Wana wa Ateri, wa wana wa Hezekia, tisini na wanane.
17 Wana wa Besai, mia tatu ishirini na watatu.
18 Wana wa Harifu, mia moja na kumi na wawili.
19 Wana wa Hashumu, mia mbili ishirini na watatu.
20 Watu wa Gibeoni, tisini na watano.
21 Watu wa Bethlehemu, mia ishirini na watatu.
22 Watu wa Netofa, hamsini na sita.
23 Watu wa Anathothi, mia ishirini na wanane.
24 Watu wa Beth-Azmawethi, arobaini na wawili.
25 Watu wa Kiriath-yearimu, na Kefira, na Beerothi, mia saba arobaini na watatu.
26 Watu wa Rama na Geba, mia sita ishirini na mmoja.
27 Watu wa Mikmashi, mia moja ishirini na wawili.
28 Watu wa Betheli, na Ai, mia mbili ishirini na watatu.
29 Watu wa Nebo, hamsini na wawili.
30 Watu wa Magbishi, mia moja hamsini na sita.
31 Watu wa Elamu wa pili, elfu moja mia mbili hamsini na wanne.
32 Watu wa Harimu, mia tatu na ishirini.
33 Watu wa Lodi, na Hadidi, na Ono, mia saba ishirini na watano.
34 Watu wa Yeriko, mia tatu arobaini na watano.
35 Watu wa Senaa, elfu tatu mia sita na thelathini.
36 Makuhani; wana wa Yedaya, wa mbari ya Yeshua, mia kenda sabini na watatu.
37 Wana wa Imeri, elfu moja hamsini na wawili.
38 Wana wa Pashuri, elfu moja mia mbili arobaini na saba.
39 Wana wa Harimu, elfu moja na kumi na saba.
40 Walawi; wana wa Yeshua, na wana wa Kadmieli wa wana wa Hodavia, sabini na wanne.
41 Waimbaji; wana wa Asafu, mia moja ishirini na wanane.
42 Akina bawabu; wana wa Shalumu, wana wa Ateri, wana wa Talmoni, wana wa Akubu, wana wa Hatita, wana wa Shobai; jumla yao ni mia moja thelathini na kenda.
43 Wanethini; wana wa Siha, wana wa Hasufa, wana wa Tabaothi;
44 wana wa Kerosi, wana wa Siaha, wana wa Padoni;
45 wana wa Lebana, wana wa Hagaba, wana wa Akubu;
46 wana wa Hagabu, wana wa Salmai, wana wa Hanani;
47 wana wa Gideli, wana wa Gahari, wana wa Reaya;
48 wana wa Resini, wana wa Nekoda, wana wa Gazamu;
49 wana wa Uza, wana wa Pasea, wana wa Besai;
50 wana wa Asna, wana wa Meunimu, wana wa Nefusimu;
51 wana wa Bakbuki, wana wa Hakufa, wana wa Harhuri;
52 wana wa Basluthi, wana wa Mehida, wana wa Harsha;
53 wana wa Barkosi, wana wa Sisera, wana wa Tema;
54 wana wa Nesia, wana wa Hatifa.
55 Wa watumwa wa Sulemani; wana wa Sotai, wana wa Soferethi, wana wa Peruda;
56 wana wa Yaala, wana wa Darkoni, wana wa Gideli;
57 wana wa Shefatia, wana wa Hatili, wana wa Pokereth-Sebaimu, wana wa Amoni.
58 Wanethini wote, pamoja na watumwa wa Sulemani, walikuwa mia tatu tisini na wawili.
59 Na hawa ndio watu waliokwea kutoka Tel-mela, na Tel-harsha, na Kerubu, na Adani, na Imeri; walakini hawakuweza kuonyesha mbari za baba zao, wala kizazi chao, kwamba walikuwa wa Israeli;
60 wana wa Delaya, wana wa Tobia, wana wa Nekoda, mia sita hamsini na wawili.
61 Tena wa makuhani; wana wa Habaya, wana wa Hakosi, wana wa Barzilai, yule aliyeoa mmojawapo wa binti Barzilai, Mgileadi, akaitwa kwa jina lao.
62 Hao waliitafuta orodha yao miongoni mwa wale waliohesabiwa kwa nasaba, wasionekane; kwa hiyo walihesabiwa kuwa na unajisi.
63 Na huyo Tirshatha akawaambia wasile katika vitu vitakatifu sana ,hata atakaposimama kuhani mwenye urimu na Thumimu.
64 Basi hilo kusanyiko lote zima, jumla yake ilikuwa watu arobaini na mbili elfu na mia tatu na sitini,
65 tena, zaidi ya hao, kulikuwa na watumishi wao waume kwa wake, ambao walikuwa saba elfu, na mia tatu na thelathini na saba; nao walikuwa na waimbaji waume kwa wake mia mbili.
66 Farasi zao walikuwa mia saba thelathini na sita; nyumbu zao, mia mbili arobaini na watano;
67 ngamia zao, mia nne thelathini na watano; punda zao elfu sita, na mia saba na ishirini.
68 Na baadhi ya wakuu wa mbari za baba zao, hapo walipoifikilia nyumba ya Bwana, iliyoko Yerusalemu, walitoa mali kwa ukarimu kwa ajili ya nyumba ya Mungu, ili kuisimamisha mahali pake;
69 wakatoa kadiri walivyoweza, na kutia katika hazina ya kazi hiyo, darkoni za dhahabu sitini na moja elfu ,na nane za fedha elfu tano,na mavazi mia ya makuhani.
70 Hivyo makuhani, na Walawi, na baadhi ya watu, na waimbaji, na mabawabu, na Wanethini, wakakaa mijini mwao, naam, Israeli wote wakakaa mijini mwao.

MASWALI YA KUJADILI:

1. Unadhani Mungu aliruhusu Wayahudi waende utumwani Babeli ili wakafundishe au wakafundishwe au yote mawili? Unadhani wanadamu baada ya kukaa kwenye dunia ya dhambi kwa takribani miaka 1,000 tumekuwa bora zaidi kuliko tulivyokuwa kabla ya dhambi? Je Mungu alipata faida yoyote kwa Wayahudi kukaa uhamishoni Babeli? Je Mungu anawachukuliaje wale wanaowalea watu wake walio kwenye mazizi mengine (vikundi vya dini) yanayopotosha ukweli wake? (Yohana 10:16).
2. Unadhani kuhesabiwa kwa watu kulilenga kubaini wenye nasaba ya Yuda na wanaostahili kurudi Yuda? Kulikuwa na hatari gani kama wasingehesabiwa? Je mtu aweza kuwa na watumishi wa kike na wa kiume na hali yeye mwenyewe akiwa mtumwa? Kwa nini watumwa waliokuwako Babeli walianza kubaguana walipokuwa wanakaribia kurejea nyumbani? Unaona hiyo ikijitokeza kwenye kanisa lako?

USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: 2 NYAKATI 36:1-23 JUMATATU 20/02/2023

1 Watu wa nchi wakamtwaa Yehoahazi mwana wa Yosia, wakamtawaza awe mfalme katika Yerusalemu badala ya babaye.
2 Yehoahazi alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitatu alipoanza kutawala; akatawala huko Yerusalemu miezi mitatu.
3 Naye mfalme wa Misri akamwondoa katika Yerusalemu, akaitoza nchi talanta mia za fedha, na talanta moja ya dhahabu.
4 Mfalme wa Misri akamtawaza Eliakimu nduguye awe mfalme juu ya Yuda na Yerusalemu, akambadilisha jina lake kuwa Yehoyakimu. Neko akamtwaa Yehoahazi nduguye, akamchukua mpaka Misri.
5 Yehoyakimu alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka kumi na mmoja; akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, Mungu wake.
6 Juu yake akakwea Nebukadreza,
7 Nebukadreza akachukua baadhi ya vyombo vya nyumba ya Bwana mpaka Babeli, akavitia katika hekalu lake huko Babeli.
8 Basi mambo yote ya Yehoyakimu yaliyosalia, na machukizo yake aliyoyafanya, nayo yaliyoonekana kwake, tazama, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda; na Yekonia
9 Yekonia alikuwa na umri wa miaka kumi na minane alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miezi mitatu na siku kumi; akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana.
10 Mwaka ulipokwisha, Nebukadreza akatuma wajumbe, akamchukua mpaka Babeli; pamoja na vyombo vya thamani vya nyumba ya Bwana; akamtawaza Sedekia nduguye awe mfalme juu ya Yuda na Yerusalemu.
11 Sedekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mmoja, alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka kumi na mmoja;
12 akafanya yaliyo mabaya machoni pa Bwana, Mungu wake; wala hakujinyenyekesha mbele ya Yeremia nabii aliponena kwa kinywa cha Bwana.
13 Tena akamwasi mfalme Nebukadreza, aliyemwapisha kwa Mungu; lakini akajifanyia shingo ngumu, akajitia moyo nguvu asimgeukie Bwana, Mungu wa Israeli.
14 Na zaidi ya hayo wakuu wote wa makuhani, na watu, wakakosa mno sawasawa na machukizo yote ya mataifa; wakainajisi nyumba ya Bwana aliyoitakasa katika Yerusalemu.
15 Naye Bwana, Mungu wa baba zao, akatuma kwao kwa mikono ya wajumbe wake, akiondoka mapema, na kutuma; kwa sababu aliwahurumia watu wake, na makao yake;
16 lakini waliwadhihaki wajumbe wa Mungu, na kuyadharau maneno yake, na kuwacheka manabii wake, hata ilipozidi ghadhabu ya Bwana juu ya watu wake, hata kusiwe na kuponya.
17 Kwa hiyo akaleta juu yao mfalme wa Wakaldayo, aliyewaua vijana wao kwa upanga nyumbani mwa patakatifu pao, asiwahurumie kijana wala mwanamwali, mzee wala mkongwe; akawatia wote mkononi mwake.
18 Na vyombo vyote vya nyumba ya Mungu, vikubwa kwa vidogo, na hazina za nyumba ya Bwana, na hazina za mfalme, na za wakuu wake; vyote pia akavileta Babeli.
19 Wakaiteketeza nyumba ya Mungu, wakaubomoa ukuta wa Yerusalemu, wakayateketeza kwa moto majumba yake yote, wakaviharibu vyombo vyake vyote vya thamani.
20 Na wale waliookoka na upanga akawachukua mpaka Babeli; wakamtumikia yeye na wanawe hata kulipoingia milki ya Uajemi;
21 ili kulitimiza neno la Bwana kwa kinywa cha Yeremia, hata nchi itakapofurahia sabato zake; kwa maana siku zote ilipokaa ukiwa ilishika sabato, kutimiza miaka sabini.
22 Ikawa katika mwaka wa kwanza wa Koreshi, mfalme wa Uajemi, ili kwamba neno la Bwana alilolisema kwa kinywa cha Yeremia lipate kutimizwa, Bwana akamwamsha roho yake Koreshi, mfalme wa Uajemi, hata akapiga mbiu katika ufalme wake wote, akaiandika pia, akisema,
23 Koreshi, mfalme wa Uajemi asema hivi; Bwana, Mungu wa mbinguni, amenipa falme zote za dunia; naye ameniagiza nimjengee nyumba katika Yerusalemu, ulioko Yuda. Basi kila mtu katika ninyi nyote mlio watu wake, Bwana, Mungu wake, na awe pamoja naye, na akwee.

MASWALI YA KUJADILI:

1. Utawala wa Yehoahazi ulitawala kwa muda mfupi wa miezi mitatu ambapo Misri ilitumia udhaifu huo kujitwalia mali kwa njia ya kodi. Je iliwezekanaje Misri bara lililodhaniwa la giza liitawale Yuda taifa linaloongozwa na Mungu? Je kuna uwezekano leo kanisa likiongozwa na watu waliochomekwa na maadui zao?
2. Kwa nini Nebukadreza hakutamani fedha bali alilenga kuvichukua vyombo vya nyumba ya Bwana ili vikatumike kwenye hekalu lake huko Babeli? Wageni wanaweza kuvutiwa na jambo gani katika ibada yako wanachoweza kukipeleka kwenye ibada zao? Kwa nini uchukuaji wa vyombo haukufanyika kwa mara moja bali kwa awamu tatu?
3. Mfalme Sedekia hakujinyenyekeza mbele ya Yeremia nabii aliponena kwa kinywa cha Bwana. Unadhani anguko la wafalme wa Yuda lilitokana na kutowasikiliza manabii wa Mungu? Ni kwa kiasi gani kanisa leo limezingatia nuru iliyotolewa na mtumishi wa Mungu Ellen G. White? Je kuna mahali mtumishi huyo wa Mungu amelionya kanisa hilo la masalio au Laodikia kukutwa na hukumu ya Mungu lisipotii na kutubu?
4. Je kumwasi mfalme Nebukadreza kulikofanywa na mfalme Sedekia kulikuwa jambo sahihi? Machoni pa Mungu nani alikuwa bora zaidi kati ya Sedekia na Nebukadreza? Je Mungu aweza kumtumia mtawala wa kipagani kumtia adabu mtumishi anayeongoza taifa lake takatifu?
5. Je Mungu anaporuhusu watu wake kuchukuliwa utumwani na wengine kuuawa kama ilivyotokea kwenye utawala wa Sedekia huwa anakuwa na huruma nao? Mungu akijiridhisha kuwa mtu wake haonyeki huchukua hatua gani? Je ikiwa Mungu atagundua kuwa upendeleo aliokufanyia huuthamini aweza kuondoa huo upendeleo kwako na kuukabidhi kwa wengine? Je unadhani Yuda walitambua ukweli huo?
6. Kwa nini Mungu aliruhusu hekalu lake takatifu kuteketezwa na mfalme wa kipagani wa Wakaldayo? Je mtoto wako asipothamini mali ulizomrithisha waweza kumnyang'anya na kumpa mtu meingine?


USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: 2 NYAKATI 35:1-27 JUMAPILI 19/02/2023


1 Naye Yosia akamfanyia Bwana pasaka huko Yerusalemu; wakachinja pasaka siku ya kumi na nne ya mwezi wa kwanza.
2 Akawasimamisha makuhani katika malinzi yao, akawatia moyo kufanya utumishi wa nyumba ya Bwana.
3 Akawaambia Walawi, waliowafundisha Israeli wote, waliotakasika kwa Bwana, Wekeni sanduku takatifu katika nyumba aliyoijenga Sulemani, mwana wa Daudi, mfalme wa Israeli; hamtakuwa tena na mzigo mabegani; sasa mtumikieni Bwana, Mungu wenu, na watu wake Israeli.
4 Mkajiweke tayari kwa kadiri ya nyumba za baba zenu, kwa zamu zenu, kama alivyoandika Daudi mfalme wa Israeli, na kama alivyoandika Sulemani mwanawe.
5 Mkasimame katika patakatifu, kama walivyogawanyika ndugu zenu, wana wa watu, kufuata nyumba za mababa, kadiri ya mgawanyiko wa kila nyumba ya baba, ya Walawi.
6 Mkachinje pasaka, mkajitakase, mkawatengenezee ndugu zenu, kutenda sawasawa na neno la Bwana kwa mkono wa Musa.
7 Tena Yosia akawapa wana wa watu, matoleo ya makundi, wana-kondoo na wana-mbuzi, yote yawe kwa ajili ya matoleo ya pasaka, wote waliokuwako, wakipata thelathini elfu, na ng'ombe elfu tatu; hao walitoka katika mali za mfalme.
8 Na wakuu wake wakawapa watu, na makuhani na Walawi matoleo ya hiari. Hilkia na wana na Yehieli, wakubwa wa nyumba ya Mungu, wakawapa makuhani, kuwa matoleo ya pasaka, wana-kondoo elfu mbili na mia sita, na ng'ombe mia tatu.
9 Konania naye, na Shemaya, na Nethaneli, ndugu zake, na Hashabia, na Yeieli, na Yozabadi, wakuu wa Walawi, wakawapa Walawi, kuwa matoleo ya pasaka, wana-kondoo elfu tano, na ng'ombe mia tano.
10 Hivyo huduma ikatengenezwa, wakasimama makuhani mahali pao, na Walawi kwa zamu zao, kama alivyoamuru mfalme.
11 Wakachinja pasaka, nao makuhani wakamimina damu waliyopokea mikononi mwao, Walawi wakachuna.
12 Wakaziondoa sadaka za kuteketezwa, wawape wana wa watu, kama walivyogawanyika kufuata nyumba za mababa, ili wamtolee Bwana, kama ilivyoandikwa katika kitabu cha Musa. Nao ng'ombe wakawafanya vivyo hivyo.
13 Wakaioka moto pasaka kama ilivyo sheria; wakatokosa matoleo matakatifu vyunguni, na masufuriani, na makaangoni, wakawachukulia upesi wana wa watu wote.
14 Baadaye wakajiandalia wenyewe, na makuhani; kwa sababu makuhani, wana wa Haruni, walikuwa na kazi ya kutoa sadaka za kuteketezwa, na mafuta hata usiku; kwa hiyo Walawi wakajiandalia wenyewe, na makuhani, wana wa Haruni.
15 Nao waimbaji, wana wa Asafu wakasimama mahali pao, kama alivyoamuru Daudi, na Asafu, na Hemani, na Yeduthuni mwonaji wa mfalme; nao mabawabu walikuwa katika kila lango; hawakuhitaji kuondoka katika huduma yao, kwa kuwa ndugu zao Walawi wakawaandalia.
16 Basi huduma yote ya Bwana ikatengenezwa siku ile ile, kuifanya pasaka, na kutoa sadaka za kuteketezwa juu ya madhabahu ya Bwana, kama alivyoamuru mfalme Yosia.
17 Wana wa Israeli waliokuwapo wakafanya pasaka wakati ule, na sikukuu ya mikate isiyochachwa muda wa siku saba.
18 Wala haikufanyika pasaka kama ile katika Israeli tangu siku za nabii Samweli; wala wafalme wa Israeli hawakufanya hata mmoja wao pasaka kama ile Yosia aliyoifanya, pamoja na makuhani, na Walawi, na Yuda wote na Israeli waliokuwapo, na wenyeji wa Yerusalemu.
19 Katika mwaka wa kumi na nane wa kutawala kwake Yosia ikafanyika pasaka hiyo.
20 Baada ya hayo yote, alipokwisha Yosia kulitengeneza hekalu, Neko, mfalme wa Misri, akakwea ili kupigana Karkemishi karibu na Frati; naye Yosia akatoka juu yake.
21 Lakini yeye akatuma kwake wajumbe, kusema, Ni nini niliyo nayo mimi na wewe, Ee mfalme wa Yuda? Sikuja juu yako leo, lakini juu ya nyumba niliyo na vita nayo; naye Mungu ameniamuru nifanye haraka; acha basi kumpinga Mungu, aliye pamoja nami, asikuharibu.
22 Walakini Yosia hakukubali kumgeuzia uso mbali, akajibadilisha apate kupigana naye, asiyasikilize maneno ya Neko, yaliyotoka kinywani kwa Mungu, akaja kupigana bondeni mwa Megido.
23 Nao wapiga upinde wakampiga Yosia; naye mfalme akawaambia watumishi wake, Niondoeni; kwani nimejeruhiwa sana.
24 Basi watumishi wake wakamtoa garini, wakamtia katika gari la pili alilokuwa nalo, wakamleta Yerusalemu; naye akafa, akazikwa makaburini mwa babaze. Wakamlilia Yosia Yuda wote na Yerusalemu.
25 Naye Yeremia akamlilia Yosia; na waimbaji wote waume kwa wake wakamtaja Yosia katika maombolezo yao, hata leo; hata wakayafanya kuwa ada kwa Israeli; nayo, tazama, yameandikwa katika maombolezo.
26 Basi mambo yote ya Yosia yaliyosalia, na matendo yake mema, sawasawa na yote yaliyoandikwa katika torati ya Bwana,
27 na mambo yake, ya kwanza na ya mwisho, tazama, yameandikwa katika kitabu cha wafalme wa Israeli na Yuda.

MASWALI YA KUJADILI:

1. Mojawapo ya mambo muhimu aliyofanya Yosia ni kumfanyia Bwana Pasaka huko Yerusalemu. Pasaka ina umuhimu gani katika kufanya matengenezo ya kiroho? Pasaka inayotukumbusha kafara ya Yesu msalabani inasaidiaje kutupatia ushindi dhdi ya maadui zetu?
2. Je watumishi wa Mungu wanahitaji kutiwa moyo ili kutekeleza majukumu yao? Kwa nini watiwe moyo ikiwa wana wito wa kazi waifanyayo? Je na wale watumishi wa Mungu wanaolipwa nao wanahitaji kutiwa moyo? Ni madhara ya kazi pale kiongozi asipowatia moyo wasaidizi wake?
3. Mnatumia vigezo gani kanisani kwenu kutambu kuwa pasaka (Meza ya Bwana) mliyofanya ilikuwa ya mafanikio? Unadhani ni kwa nini baadhi ya watu wanapuuza kushiriki Meza ya Bwana. Kuna faida gani kanisa zima likishiriki Meza ya Bwana. Kufanikiwa kwa Meza ya Bwana kunatokana na juhudi za Mashemasi au Wazee wa Kanisa na Mchungaji? Je Meza ya Bwana kanisani kwenu imewasaidia washiriki kuwa wanyenyekevu na wenye mshikamano zaidi?
4. Kwaya zina mchango gani katika kuifanya Meza ya Bwana kuwa ya kipekee. Uimbaji wa kicho unaovuta hisia za waabuduo kwa Mungu aliye juu umekuwa wa kawaida kanisani kwako?
5. Unadhani kuvaa majoho kunawatambulisha waimbaji kama wahudumu wa ibada kuliko ilivyo kwa mavazi mengine yasiyo majoho? Mwonekano wa majoho unawapunguziaje majaribu waimbaji na watazamaji wao?


USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: 2 NYAKATI 34:1-25 JUMAMOSI 18/02/2023


1 Yosia alikuwa na umri wa miaka minane alipoanza kutawala; akatawala miaka thelathini na mmoja huko Yerusalemu.
2 Akafanya yaliyo mema machoni pa Bwana, akaziendea njia za Daudi babaye, asigeuke kwa kuume wala kwa kushoto.
3 Kwa kuwa katika mwaka wa nane wa kutawala kwake, naye akali mchanga, alianza kumtafuta Mungu wa Daudi babaye; hata katika mwaka wa kumi na mbili akaanza kusafisha Yuda na Yerusalemu kwa kuondoa mahali pa juu, na kwa kuondoa maashera, na sanamu za kuchora, nazo za kusubu.
4 Wakazibomoa madhabahu za mabaali machoni pake; na sanamu za jua, zilizoinuliwa juu yake, akazikata-kata; na maashera, na sanamu za kuchonga, nazo za kusubu, akazivunja-vunja, akaziponda kuwa mavumbi, akayamimina juu ya makaburi ya hao waliozichinjia dhabihu.
5 Akaiteketeza mifupa ya makuhani madhabahuni mwao, akasafisha Yuda na Yerusalemu.
6 Na katika miji ya Manase, na Efraimu, na Simeoni, mpaka Naftali, akafanya vile vile; na katika maganjo yake pande zote.
7 Akazibomoa madhabahu, akaponda-ponda maashera na sanamu kuwa mavumbi, akazikata-kata sanamu zote za jua katika nchi yote ya Israeli, kisha akarejea Yerusalemu.
8 Hata katika mwaka wa kumi na nane wa kutawala kwake, alipokwisha kuisafisha nchi, na nyumba, akamtuma Shafani, mwana wa Azalia, na Maaseya, akida wa mji, na Yoa, mwana wa Yoahazi, mwandishi wa tarehe, waitengeneze nyumba ya Bwana, Mungu wake.
9 Wakamjia Hilkia kuhani mkuu, wakampa fedha, iliyoletwa nyumbani mwa Mungu, waliyoikusanya Walawi, wangoje mlango, mikononi mwa Manase na Efraimu, na mabaki yote ya Israeli, na Yuda yote na Benyamini, na wenyeji wa Yerusalemu.
10 Wakaitia mikononi mwa watenda kazi walioisimamia nyumba ya Bwana; na hao mafundi waliotenda kazi nyumbani mwa Bwana wakaitoa kwa kuitengeneza na kuifanya upya nyumba;
11 wakawapa maseremala na waashi, ili wanunue mawe ya kuchonga, na miti ya kuungia, na kuifanyiza boriti kwa nyumba zile walizoziharibu wafalme wa Yuda.
12 Nao watu wakatenda kazi kwa uaminifu; na wasimamizi wao walikuwa Yahathi na Obadia, Walawi, wa wana wa Merari; na Zekaria na Meshulamu, wa wana wa Wakohathi, ili kuihimiza kazi; na wengine katika Walawi, wote waliokuwa wastadi wa kupiga vinanda.
13 Tena walikuwa juu ya wachukuzi wa mizigo, wakawahimiza wote waliotenda kazi ya huduma yo yote; na miongoni mwa Walawi kulikuwa na waandishi, na wasimamizi, na mabawabu.
14 Nao walipotoa ile fedha iliyoletwa nyumbani mwa Bwana, Hilkia kuhani akakiona kitabu cha torati ya Bwana iliyotolewa kwa mkono wa Musa.
15 Akajibu Hilkia akamwambia Shafani mwandishi, Kitabu cha torati nimekiona nyumbani mwa Bwana. Hilkia akampa Shafani kile kitabu.
16 Shafani akampelekea mfalme hicho kitabu, tena akampasha mfalme habari, akisema, Yote waliyokabidhiwa watumishi wako, wayafanya.
17 Nao wameimimina fedha iliyoonekana nyumbani mwa Bwana, nayo wameitia mikononi mwa wasimamizi, na mikononi mwa watenda kazi.
18 Shafani mwandishi akamweleza mfalme, akisema, Hilkia kuhani amenipa kitabu. Shafani akasoma ndani yake mbele ya mfalme.
19 Ikawa, mfalme alipoyasikia maneno ya torati, aliyararua mavazi yake.
20 Mfalme akawaamuru Hilkia, na Ahikamu, mwana wa Shafani, na Abdoni, mwana wa Mika, na Shafani mwandishi, na Asaya, mtumishi wa mfalme, kusema,
21 Nendeni, mkamwulize Bwana kwa ajili yangu, na kwa hao waliosalia wa Israeli na wa Yuda, katika habari za maneno ya kitabu kilichoonekana; maana ghadhabu ya Bwana ni nyingi iliyomwagika juu yetu, kwa sababu baba zetu hawakulishika neno la Bwana, kutenda sawasawa na yote yaliyoandikwa kitabuni humo.
22 Basi Hilkia, na hao waliotumwa na mfalme, wakamwendea Hulda nabii mke, mkewe Shalumu, mwana wa Tohathi, mwana wa Hasra, mtunza mavazi; (naye alikuwa akikaa Yerusalemu katika mtaa wa pili); wakasema naye kama hayo.
23 Akawaambia, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi; Mwambieni mtu huyo aliyewatuma kwangu,
24 Bwana asema hivi, Angalia, nitaleta mabaya juu ya mahali hapa, na juu ya wakaao, laana zote zilizoandikwa katika kitabu hicho walichokisoma mbele ya mfalme wa Yuda;
25 kwa sababu wameniacha mimi, na kuifukizia uvumba miungu mingine, ili wanikasirishe mimi kwa matendo yote ya mikono yao; kwa hiyo ghadhabu yangu imemwagika juu ya mahali hapa, wala isizimike.
26 Lakini mfalme wa Yuda, aliyewatuma kumwuliza Bwana, mtamwambia hivi, Bwana, Mungu wa Israeli, asema hivi; Kwa habari ya maneno uliyoyasikia,
27 kwa kuwa moyo wako ulikuwa mwororo, nawe umejinyenyekeza mbele ya Mungu, uliposikia maneno yake juu ya mahali hapa, na juu ya wakaao, ukajinyenyekeza mbele zangu, na kuyararua mavazi yako, na kulia mbele zangu; mimi nami nimekusikia, asema Bwana.
28 Tazama, nitakukusanya kwa baba zako, nawe utawekwa kaburini mwako kwa amani, wala macho yako hayataona mabaya yote nitakayoyaleta juu ya mahali hapa, na juu ya wakaao. Basi wakamrudishia mfalme habari.
29 Ndipo mfalme akapeleka wajumbe, akawakusanya wazee wote wa Yuda na Yerusalemu.
30 Akapanda mfalme nyumbani kwa Bwana, na watu wote wa Yuda, na wenyeji wa Yerusalemu, na makuhani na Walawi, na watu wote, wakubwa kwa wadogo; naye akasoma masikioni mwao maneno yote ya kitabu cha agano kilichoonekana nyumbani mwa Bwana.
31 Akasimama mfalme mahali pake, akafanya agano mbele za Bwana, kumfuata Bwana, na kuzishika amri zake, na shuhuda zake, na sheria zake, kwa moyo wake wote, na kwa roho yake yote, kuyatenda maneno ya agano yaliyoandikwa kitabuni humo.
32 Akawafanya wote walioonekana katika Yerusalemu na Benyamini walikubali. Na wenyeji wa Yerusalemu wakafanya sawasawa na agano la Mungu, Mungu wa baba zao.
33 Naye Yosia akayaondolea mbali machukizo yote katika nchi zote zilizokuwa milki ya wana wa Israeli, akawafanya wote walioonekana katika Israeli kutumika, naam, wamtumikie Bwana, Mungu wao. Siku zake zote hawakuacha kumfuata Bwana, Mungu wa baba zao.

NILICHOGUNDUA NA KUJIFUNZA:

1. Umri mdogo wa mfalme Yosia haukuwa kikwazo cha yeye kushindwa kufanya vizuri katika majukumu yake. Hoja zinazotolewa na baadhi yetu juu ya kushindwa kwao kunakosababishwa na umri wao mdogo kazini zinathibitishwa na Yosia kuwa hazina mashiko. Katika uchanga wake wa umri na kazi alianza kumtafuta Mungu. Umri haumzuii Roho Mtakatifu kukufanya mkamilifu na uliyekomaa.
2. Kutokwenda kushoto wala kulia ni kusimamia kanuni na miongozo iliyopo bila kuyumba. Taasisi nyingi zinaanguka kwa kukosa wasimamizi thabiti kama Yosia. Mungu anajua wakati atakaowaleta viongozi wa aina hiyo kuongoza kazi yake. Tumwombe Bwana wa mavuno atume watendakazi shambani mwake.
3. Kubomoa machafu yaliyokuwepo kwenye uongozi uliotangulia kabla yako ni jambo linalohitaji ujasiri. Wengine hatua kama hiyo huilinganisha na kufukua makaburi hivyo huiepuka. Mambo yanayohitaji kubomolewa yanaweza yasionekane katika sura ya ubaya lakini ambayo yamerudisha nyuma kasi ya ukuaji wa kazi. Mipango mibovu na watu waliokuwa kwenye ajira kimakosa na kusababisha hasara kwa taasisi ni miongoni mwa mambo yanayohitaji kubomolewa. Ubomoaji huu ingawa huleta maumivu huzaa matumaini mapya ya maendeleo.
4. Utawala mpya unapoingia mara nyingi hukutana na uhaba wa fedha za kugharamia uendeshaji. Katika hali hiyo mikakati ya upatikanaji wa fedha kwa haraka kukidhi mahitaji huwa ni ya lazima. Uongozi usio na mkakati endelevu wa vyanzo vya mapato vya kuaminika una uwezekano wa kushindwa kabla haujaanza. Kama kuna eneo linalohitaji umakini mkubwa kulisimamia ni utunzaji wa mali na fedha. Matengenezo ya kweli ni lazima yaguse usimamizi wa fedha.
5. Jamii inayojiepusha na maonyo na makatazo ya Mwenyezi Mungu inatembea gizani kwa kuwa itakuwa na upungufu mkubwa katika mambo yahusuyo maadili. Mafanikio ya taifa, taasisi au mtu binafsi yanategemea inavyolipatia kipaumbele swala la usomaji wa Neno la Mungu na uinjilisti. Neno la Mungu linapswa kulindwa kwa gharama yoyote wakati wowote (Yoshua 1:8; Wakolosai 3:16).


USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: 2 NYAKATI 33:1-25 17/02/2023


1 Manase alikuwa na umri wa miaka kumi na miwili alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka hamsini na mitano.
2 Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, sawasawa na machukizo yote ya mataifa, aliowafukuza Bwana mbele ya wana wa Israeli.
3 Kwa maana akapajenga tena mahali pa juu alipopabomoa Hezekia babaye; akazisimamisha madhabahu za mabaali, akafanya na sanamu za maashera, akaabudu jeshi lote la mbinguni, na kulitumikia.
4 Akajenga madhabahu katika nyumba ya Bwana, napo ndipo alipopanena Bwana, Katika Yerusalemu litakuwako jina langu milele.
5 Akajenga madhabahu kwa ajili ya jeshi lote la mbinguni katika nyua mbili za nyumba ya Bwana.
6 Tena akawapitisha wanawe motoni katika bonde la mwana wa Hinomu; akatazama bao, akabashiri, akafanya uganga, akajishughulisha na hao wenye pepo wa utambuzi, na wachawi; akafanya mabaya mengi machoni pa Bwana, hata kumkasirisha.
7 Akaiweka sanamu ya kuchonga aliyoifanya, katika nyumba ya Mungu ambayo Mungu alimwambia Daudi, na Sulemani mwanawe, Katika nyumba hii, na katika Yerusalemu, niliouchagua miongoni mwa kabila zote za Israeli, nitaliweka jina langu milele;
8 wala sitawaondoshea miguu tena Israeli katika nchi niliyowaagizia baba zenu; wakiangalia tu kutenda yote niliyowaamuru, yaani, torati yote, na sheria, na maagizo, niliyowaamuru kwa mkono wa Musa.
9 Basi Manase akawakosesha Yuda na wenyeji wa Yerusalemu, hata wakazidi kufanya mabaya kuliko mataifa, aliowaharibu Bwana mbele ya wana wa Israeli.
10 Naye Bwana akasema na Manase, na watu wake; wala wasiangalie.
11 Kwa hiyo Bwana akaleta juu yao maakida wa jeshi la mfalme wa Ashuru, waliomkamata Manase kwa minyororo, wakamfunga kwa pingu, wakamchukua mpaka Babeli.
12 Hata alipokuwa katika taabu, akamsihi Bwana, Mungu wake, akajinyenyekeza sana mbele za Mungu wa baba zake.
13 Akamwomba; naye akamtakabali, akayasikia maombi yake; akamrudisha tena Yerusalemu katika ufalme wake. Ndipo Manase akajua ya kwamba Bwana ndiye Mungu.
14 Hata baada ya hayo akaujengea mji wa Daudi ukuta wa nje, upande wa magharibi wa Gihoni, bondeni, hata kufika maingilio ya lango la samaki; akauzungusha Ofeli, akauinua juu sana; akaweka maakida mashujaa katika miji yote ya Yuda yenye maboma.
15 Akaiondoa miungu migeni, na hiyo sanamu nyumbani mwa Bwana, na madhabahu zote alizozijenga katika mlima wa nyumba ya Bwana, na Yerusalemu, akazitupa nje ya mji.
16 Akaijenga madhabahu ya Bwana, akatoa juu yake dhabihu za sadaka za amani, na za shukrani, akawaamuru Yuda wamtumikie Bwana, Mungu wa Israeli.
17 Lakini watu wakaendelea kutoa dhabihu katika mahali pa juu, ila wakamtolea Bwana, Mungu wao tu.
18 Basi mambo yote ya Manase yaliyosalia, na maombi yake kwa Mungu wake, na maneno ya waonaji walionena naye kwa jina la Bwana, Mungu wa Israeli, tazama, yameandikwa kati ya mambo ya wafalme wa Israeli.
19 Sala yake pia, na jinsi Mungu alivyomtakabali, na dhambi yake yote, na kosa lake, na mahali alipopajenga mahali pa juu, na kupasimamishia maashera na sanamu za kuchonga, kabla ya kujinyenyekeza; tazama, hayo yameandikwa katika tarehe ya Hozai.
20 Basi Manase akalala na babaze, wakamzika nyumbani mwake; na Amoni mwanawe akatawala mahali pake.
21 Amoni alikuwa na umri wa miaka ishirini na miwili alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka miwili.
22 Akafanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, kama alivyofanya Manase babaye; Amoni akazitolea dhabihu sanamu zote alizozifanya Manase babaye, akazitumikia.
23 Wala hakujinyenyekeza mbele za Bwana, kama Manase babaye alivyojinyenyekeza; lakini huyo Amoni akaongeza makosa juu ya makosa.
24 Wakamfanyia fitina watumishi wake, wakamwua katika nyumba yake mwenyewe.
25 Lakini watu wa nchi wakawaua wote waliomfanyia fitina mfalme Amoni; watu wa nchi wakamfanya Yosia mwanawe awe mfalme badala yake.

MASWALI YA KUJADILI:

1. Je anayeanza kutawala akiwa na miaka 12 anapata wapi uzoefu wa kuongoza watu? Je ni nani alikuwa anaamua wawe viongo? Je, ni wao wenyewe na mfumo wa utawala uliopo au wanawekwa na wananchi? Wapo wanaodhani mfumo wa kidemokrasia haufai katika kuongoza nchi changa. Unaichukuliaje hoja hiyo ukifananisha na mfumo usio wa kidemokrasia uliokuwa ukiongoza Yuda na Israeli zamani hizo?
2. Je watawala wanahitaji kuwekewa masharti wasiyopaswa kukiuka mara waingiapo madarakani? Kwa nini hapakuwa na mwendelezo wa yale mema yaliyofanywa na watawala wa vipindi vya nyuma? Je kiongozi akiasi ni lazima wafuasi wake wote waasi?
3. Mungu ana uwezo wa kubashiri na kufanya uganga lakini Manase alitaka huduma hizo kutoka vyanzo vilivyopigwa marufuku? Inakuwaje mwanadamu anapoteza imani kwa Mungu na kuweka matumaini yake kwa mwanadamu mwenzake?
4. Namna pekee kwa baadhi ya watu yakuwafanya watambue kuwa Mungu ni Bwana ni kwa kuwaingiza kwenye tanuru la mateso. Kwa nini ni vigumu kwa mwanadamu kuwa mnyenyekevu hadi ateswe kwanza?
5. Kiongozi aliyeasi akitubu anaweza kurejeshwa kwenye nafasi yake ya awali? Kwa nini Mungu alimrejeshea nafasi yake ya ufalme baada ya kutubu? Je, Shetani angetubu kama Manase angerudishiwa nafasi yake mbinguni?
6. Manase, tofauti na wafalme wengi waliomtangulia, alianza vibaya na kumaliza vizuri. Iliwezekanaje kwa mfalme kunyenyekea na kuanza matengezo ya toba bila kuona kuwa tendo hilo ni la kujidhalilisha? Je unaweza kumwita Manase shujaa kwa kitendo chake hicho? Kwa nini Manase anasemwa kwa mabaya zaidi kuliko kwa mazuri?


USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: 2 NYAKATI 32:1-29 ALHAMISI 16/02/2023


1 :Ikawa, baada ya mambo hayo, na uaminifu huo, Senakeribu, mfalme wa Ashuru, akaja, akaingia katika Yuda, akafanya marago juu ya miji yenye maboma, akadhania kwamba ataipata iwe yake.
2 Basi Hezekia, alipoona ya kuwa Senakeribu amekuja, na kuazimia kupigana na Yerusalemu,
3 akafanya shauri na wakuu wake, na mashujaa wake, kuzuia maji ya chemchemi zilizokuwa nje ya mji; nao wakamsaidia.
4 Wakakusanyika watu wengi, wakazizuia chemchemi zote, na kijito kilichopita kati ya nchi, wakisema, Kwa nini, wakifika wafalme wa Ashuru, waone maji mengi?
5 Akapiga moyo konde, akaujenga ukuta wote uliobomoka, akauinua sawa na minara, na ukuta wa pili nje, akaongeza nguvu ya Milo, katika mji wa Daudi, akafanya silaha na ngao tele.
6 Akaweka maakida wa vita juu ya watu, akawakusanya kwake uwandani penye lango la mji, akawafurahisha mioyo; akisema,
7 Iweni hodari, na wa moyo mkuu, msiogope, wala msifadhaike kwa sababu ya mfalme wa Ashuru, wala kwa majeshi yote walio pamoja naye; kwa maana yupo mkuu pamoja nasi kuliko aliye pamoja naye;
8 kwake upo mkono wa mwili; ila kwetu yupo Bwana, Mungu wetu, kutusaidia, na kutupigania mapigano yetu. Na watu wakayategemea maneno ya Hezekia, mfalme wa Yuda.
9 Na baada ya hayo Senakeribu mfalme wa Ashuru, akatuma watumishi wake waende Yerusalemu, (naye alikuwapo mbele ya Lakishi, na uwezo wake wote pamoja naye,) kwa Hezekia, mfalme wa Yuda, na kwa Yuda wote waliokuwako Yerusalemu, kusema,
10 Senakeribu, mfalme wa Ashuru, asema hivi, Mwatumainia nini hata mkae mkihusuriwa katika Yerusalemu?
11 Siye Hezekia anayewashawishi, mtolewe kufa kwa njaa na kwa kiu, akisema, Bwana, Mungu wetu, atatuokoa na mkono wa mfalme wa Ashuru?
12 Si yeye Hezekia huyo aliyeondoa mahali pake pa juu, na madhabahu zake, akawaamuru Yuda na Yerusalemu, akisema, Abuduni mbele ya madhabahu moja, na juu yake mtafukiza uvumba?
13 Je! Ninyi hamjui mimi na baba zangu tuliyowafanyia watu wote wa nchi? Je! Miungu ya mataifa wa nchi iliweza kuokoa kwa lo lote nchi zao na mkono wangu?
14 Ni yupi miongoni mwa miungu ya mataifa wale walioharibiwa kabisa na baba zangu, aliyeweza kuwaokoa watu wake na mkono wangu, hata Mungu wenu aweze kuwaokoa ninyi na mkono wangu?
15 Basi sasa asiwadanganye Hezekia, wala asiwashawishi kwa hayo, wala msimwamini; kwa kuwa hapana mungu wa taifa lo lote, wala wa ufalme wo wote, aliyeweza kuwaokoa watu wake na mkono wangu, au na mkono wa baba zangu; sembuse Mungu wenu atawaokoaje ninyi na mkono wangu?
16 Na watumishi wake wakazidi kusema juu ya Bwana Mungu, na juu ya Hezekia, mtumishi wake.
17 Tena akaandika waraka, kumtukana Bwana, Mungu wa Israeli, na kumwambia, akisema, Kama vile miungu ya mataifa wa nchi isivyowaokoa watu wao na mkono wangu, vivyo hivyo Mungu wa Hezekia hatawaokoa watu wake na mkono wangu.
18 Wakawalilia kwa sauti kuu, kwa lugha ya Kiyahudi, watu wa Yerusalemu waliokuwako ukutani ili kuwaogofisha, na kuwafadhaisha; hata wapate kuutwaa mji.
19 Wakamnenea Mungu wa Yerusalemu, kana kwamba kuitaja miungu ya mataifa wa nchi, iliyo kazi ya mikono ya watu.
20 Na kwa ajili ya hayo Hezekia mfalme, na Isaya nabii, mwana wa Amozi, wakaomba, wakalia hata mbinguni.
21 Naye Bwana akatuma malaika aliyewakatia mbali mashujaa wote, na majemadari, na maakida, matuoni mwa mfalme wa Ashuru. Basi akarudia nchi yake mwenye haya ya uso. Naye alipoingia nyumbani mwa mungu wake, wale waliotoka viunoni mwake mwenyewe wakamwangamiza humo kwa upanga.
22 Ndivyo Bwana alivyomwokoa Hezekia, na wenyeji wa Yerusalemu, na mkono wa Senakeribu, mfalme wa Ashuru, na mikononi mwa wote, akawaongoza pande zote.
23 Watu wengi walimletea Bwana zawadi huko Yerusalemu, na vitu vya thamani kwa Hezekia, mfalme wa Yuda; hata yeye akatukuka tangu wakati ule machoni pa mataifa yote.
24 Katika siku hizo Hezekia akaugua akawa katika hatari ya kufa; akamwomba Bwana; naye akasema naye, akampa ishara.
25 Walakini kadiri alivyofadhiliwa Hezekia hakumrudishia vivyo; kwa kuwa moyo wake ulitukuka; kwa hiyo ikawako hasira juu yake, na juu ya Yuda na Yerusalemu.
26 Hata hivyo Hezekia akajinyenyekeza kwa ajili ya huku kutukuka kwa moyo wake, yeye na wenyeji wa Yerusalemu, hata haikuwajia hasira ya Bwana siku za Hezekia.
27 Naye Hezekia akawa na mali nyingi mno na heshima; akajifanyizia hazina za fedha, na za dhahabu, na za vito, na za manukato, na za ngao, na za namna zote za vyombo vya thamani;
28 ghala pia za mazao ya nafaka na mvinyo na mafuta; na malisho ya wanyama wa namna zote, na makundi mazizini.
29 Tena akajifanyizia miji, na mali za kondoo na ng'ombe kwa wingi; maana Mungu alimtajirisha sana sana.
30 Naye huyo Hezekia ndiye aliyezuia chemchemi ya juu ya maji ya Gihoni, akayaleta chini moja kwa moja upande wa magharibi wa mji wa Daudi. Akafanikiwa Hezekia katika kazi zake zote.
31 Walakini kwa habari ya wajumbe wa wakuu wa Babeli, waliotuma kwake kuuliza ajabu iliyofanywa katika nchi, Mungu akamwacha, ili amjaribu, ili kwamba ayajue yote yaliyokuwamo moyoni mwake.
32 Basi mambo yote ya Hezekia yaliyosalia, na matendo yake mema, tazama, yameandikwa katika maono ya Isaya nabii, mwana wa Amozi, katika kitabu cha wafalme wa Yuda na Israeli.
33 Hezekia akalala na babaze, wakamzika mahali pa kupandia makaburi ya wana wa Daudi; nao Yuda wote na wenyeji wa Yerusalemu wakamfanyia heshima alipokufa. Na Manase mwanawe akatawala mahali pake.

NILICHOGUNDUA NA KUJIFUNZA:

1. Ni muhimu kuzuia mianya ambayo adui anaweza kuitumia ili kukushinda. Kutojiandaa kushinda ni kujiandaa kushindwa. Ushindi hupatikana katika hatua za maandalizi. Unakusanya taarifa za kutosha za adui. Unapima uwezo wako. Kisha unabuni mkakati wa kumsambaratisha adui yako
2. Hamasa kwa wapambanaji wa mstari wa mbele ni ya muhimu. Wapambanaji hujengewa uwezo kwa kutiwa moyo na kutendewa wanavyostahili. Vitendea kazi si muhimu kuliko upendo wanaooneshwa. Ni lazima wajione kuwa bora na muhimu. Ni lazima wafurahishwe mioyo yao.
3. Lazima sisi tulio wapambanaji tutambue kuwa tunapigana kwa ajili ya nani na kwa nini? Ni lazima tutambue tumepata upendeleo kuwemo kwenye taasisi tuliyopo. Tutambue kuwa aliye upande wetu ni mkuu kuliko aliye upande wa adui. Tutambue kuwa katika mapambano haya hakuna kushindwa. Aliye upande wetu hajawahi kushindwa.
4. Tambo katika vita ya kiroho na katika vita yeyote ile ni za muhimu (1 Wafalme 18:27). Kuzomea adui na kushangilia timu yako ni mambo yasiyoweza kutenganishwa. Hakuna namna ya kutukuza uwezo wa adui. Uwezo wa adui unapotukuzwa na unapoongelewa sana una kawaida ya kupunguza kiwango cha ujasiri.
5. Historia ya ushindi ina nafasi katika kuandaa mazingira ya ushindi. Lakini siyo kila ushindi wa siku za nyuma wa adui waweza kuwa kigezo cha kumhofia. Ushindi wake waweza kuwa umetokana na kuwashinda wenye viwango vya chini. Adui wa kuhofiwa ni yule aliyewashinda watu wa kiwango chako au walio zaidi yako. Hata hivyo ushindi hautegemei sana historia. Hutegemea hali ya mshindani wako ilivyo siku ya tukio. Ushindi wa adui yako katika siku za nyuma hauwezi kuwa sababu ya wewe kushindwa. Hata Goliati mwenye historia ya kushinda alipigwa na kijana mdogo Daudi (1 Samweli 17:4-51).
6. Wale wanaowashutumu watumishi wa Mungu kwa kuwasingizia uongo wanajitafutia maangamizo. Hawawadhalilishi viongozi na taasisi wanayoisimamia tu bali wanamdhalilisha Mungu mwenyewe pia. Kulilinganisha kanisa la Mungu lenye kufuata misingi ya Maandiko na makanisa yenye kubeba mapokeo ya wanadamu ni udhalilishaji kama ule uliofanywa na Senakerubi. Wanaotambua heshima ya Mungu watakapoomba wadhalilishaji hao watajikuta mahali pabaya.
7. Kuna uwezekano wa Mungu kumtajirisha sana sana mwanadamu. Mungu hapendi tuwe maskini. Umaskini wetu waweza kuwa umetokana na sisi kutomtumainia au kushindwa kuitawala ile mali. Mungu hutajirisha utajiri udumuo na usio na majuto (Yakobo 1:17; Kumb. 8:18; Mithali 8:18; 2 Kor. 9:8). Tatizo la watu ni kutafuta utajiri kwa kutegemea akili zao wenyewe (Mithali 23:4; Wafilipi 4:19), na kuitumainia hiyo mali (1Timotheo 6:17; 1Timotheo 6:10).

USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: 2 NYAKATI 31:1-21 JUMATANO 15/02/2023


1 Basi hayo yote yalipokwisha, wakatoka Israeli wote waliokuwako waende miji ya Yuda, wakazivunja-vunja nguzo, wakayakata-kata maashera, wakabomoa mahali pa juu na madhabahu katika Yuda yote na Benyamini, katika Efraimu pia na Manase, hata walipokwisha kuviharibu vyote. Ndipo wana wa Israeli wote wakarudi, kila mtu kwa milki yake, mijini kwao.
2 Hezekia akaziweka zamu za makuhani na Walawi kwa zamu zao, kila mtu kwa kadiri ya huduma yake, makuhani na Walawi pia, kwa sadaka za kuteketezwa na kwa sadaka za amani, kutumika, na kushukuru, na kusifu, malangoni mwa matuo ya Bwana.
3 Tena akaweka sehemu ya mfalme ya mali zake kwa sadaka za kuteketezwa, yaani, sadaka za kuteketezwa za asubuhi na jioni, na sadaka za kuteketezwa za sabato, na za mwezi mpya, na sikukuu, kama ilivyoandikwa katika torati ya Bwana.
4 Tena akawaamuru watu waliokaa Yerusalemu, watoe sehemu ya makuhani na Walawi, ili hao wajibidiishe katika torati ya Bwana.
5 Mara ilipotangaa amri, wana wa Israeli wakatoa kwa wingi malimbuko ya nafaka, na divai, na mafuta, na asali, na mazao yote ya mashamba; na zaka za vitu vyote wakazileta nyingi.
6 Nao wana wa Israeli na Yuda, waliokaa mijini mwa Yuda, wakaleta pia zaka za ng'ombe na kondoo, na zaka za vitu vilivyowekwa wakfu, alivyowekewa Bwana, Mungu wao, wakaviweka chungu chungu.
7 Katika mwezi wa tatu wakaanza kuweka misingi ya hizo chungu, wakazimaliza katika mwezi wa saba.
8 Hata walipokuja Hezekia na wakuu, na kuziona zile chungu, wakamhimidi Bwana, na watu wake Israeli.
9 Ndipo Hezekia akaulizana na makuhani na Walawi katika habari ya hizo chungu.
10 Azaria kuhani mkuu, wa nyumba ya Sadoki, akamjibu, akasema, Tangu watu walipoanza kuleta matoleo nyumbani kwa Bwana, tumekula na kushiba, na kusaza tele; kwa kuwa Bwana amewabariki watu wake; na kilichosalia ndiyo akiba hii kubwa.
11 Ndipo Hezekia akaamuru kutengeneza vyumba nyumbani mwa Bwana; wakavitengeneza.
12 Wakayaingiza matoleo na zaka na vitu vilivyowekwa wakfu, kwa uaminifu; na juu yake Konania Mlawi alikuwa mkuu, na wa pili ni Shimei nduguye.
13 Na Yehieli, na Azaria, na Nahathi, na Asaheli, na Yerimothi, na Yozabadi, na Elieli, na Ismakia, na Mahathi, na Benaya, walikuwa wasimamizi chini ya mkono wa Konania na Shimei nduguye, kwa amri ya Hezekia mfalme, na Azaria mkuu wa nyumba ya Mungu.
14 Na Kore, mwana wa Imna, Mlawi, bawabu wa mlango wa mashariki, alizisimamia sadaka za hiari za Mungu; ili kugawa matoleo ya Bwana, navyo vitu vilivyokuwa vitakatifu sana.
15 Na chini yake walikuwa Edeni, na Minyamini, na Yeshua, na Shemaya, na Amaria, na Shekania, mijini mwa makuhani, kwa walivyoaminiwa, ili kuwagawia ndugu zao kwa zamu, wakuu na wadogo sawasawa;
16 zaidi ya wale waliohesabiwa kwa nasaba ya wanaume, wenye miaka mitatu na zaidi, kila mmoja aliyeingia nyumbani mwa Bwana, kama ilivyopasa kazi ya kila siku, kwa huduma zao katika malinzi yao, kwa kadiri ya zamu zao;
17 na wale waliohesabiwa kwa nasaba ya makuhani kufuata nyumba za baba zao, na Walawi, wenye umri wa miaka ishirini na zaidi, katika malinzi yao, kwa kadiri ya zamu zao;
18 na wale waliohesabiwa kwa nasaba ya wadogo wao wote, wake zao, na wana wao, na binti zao, katika kusanyiko lote; kwani kwa vile walivyoaminiwa, wakajitakasa katika utakatifu;
19 tena kwa ajili ya wana wa Haruni makuhani, waliokuwamo mashambani mwa malisho ya miji yao, mji kwa mji, kulikuwa na watu waliotajwa majina yao, ili kuwagawia sehemu wanaume wote miongoni mwa makuhani, na wote waliohesabiwa kwa nasaba miongoni mwa Walawi.
20 Na hivyo ndivyo alivyofanya Hezekia katika Yuda yote; akatenda yaliyo mema, na ya adili, na uaminifu, mbele za Bwana, Mungu wake.
21 Na katika kila kazi aliyoanza kwa utumishi wa nyumba ya Mungu, na kwa torati, na kwa amri, ili kumtafuta Mungu wake, aliifanya kwa moyo wake wote, akafanikiwa.

NILICHOGUNDUANAKUJIFUNZA:

1. Kama watu wangeleta matoleo nyumbani mwa Bwana, wangekula na kushiba, na kusaza tele, kwa kuwa Bwana angewabariki watu wake. Kuzuia mali ya Mungu kumetuzuilia mibaraka (Mithali 11:24). Mungu ameweka utaratibu wa matoleo ili atunufaishe sisi (Mithali 28:25).


USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: 2 NYAKATI 29:1-36 JUMATATU 13/02/2023


1 Hezekia alikuwa na umri wa miaka ishirini na mitano alipoanza kutawala; akatawala katika Yerusalemu miaka ishirini na kenda; na jina la mamaye aliitwa Abiya binti Zekaria.
2 Akafanya yaliyo ya adili machoni pa Bwana, sawasawa na yote aliyoyafanya Daudi babaye.
3 Yeye, katika mwaka wa kwanza wa kutawala kwake, katika mwezi wa kwanza, aliifungua milango ya nyumba ya Bwana, akaitengeneza.
4 Akawaingiza makuhani na Walawi, akawakusanya uwandani upande wa mashariki,
5 akawaambia, Nisikieni, enyi Walawi; jitakaseni nafsi zenu sasa, mkaitakase na nyumba ya Bwana, Mungu wa baba zenu, mkautoe uchafu katika patakatifu.
6 Kwa maana baba zetu wameasi, na kufanya yaliyo maovu machoni pa Bwana, Mungu wetu, wamemwacha, na kugeuzia mbali nyuso zao na makao ya Bwana, na kumpa maungo.
7 Tena wameifunga milango ya ukumbi, na kuzizima taa, wala hawakufukiza uvumba, wala hawakumtolea Mungu wa Israeli sadaka za kuteketezwa katika patakatifu.
8 Kwa hiyo hasira ya Bwana imekuwa juu ya Yuda na Yerusalemu, naye amewatoa kuwa matetemeko, wawe ushangao, na mazomeo, kama mwonavyo kwa macho yenu.
9 Kwa kuwa, tazama, baba zetu wameangamia kwa upanga, na wana wetu, na binti zetu, na wake zetu wametekwa kwa ajili ya hayo.
10 Basi nia yangu ni kufanya agano na Bwana, Mungu wa Israeli, ili kwamba hasira yake kali itugeukie mbali.
11 Basi wanangu, msijipurukushe sasa, kwa kuwa Bwana amewachagua ninyi msimame mbele yake, kumhudumia, nanyi mpate kuwa watumishi wake, mkafukize uvumba.
12 Ndipo wakaondoka Walawi, Mahathi mwana wa Amasai, na Yoeli mwana wa Azaria, wa wana wa Wakohathi; na wa wana wa Merari, Kishi mwana wa Abdi, na Azaria mwana wa Yehaleleli; na wa Wagershoni, Yoa mwana wa Zima na Edeni mwana wa Yoa;
13 na wa wana wa Elisafani, Shimri na Yeueli; na wa wana wa Asafu, Zekaria na Matania;
14 na wa wana wa Hemani, Yehueli na Shimei; na wa wana wa Yeduthuni, Shemaya na Uzieli.
15 Wakawakusanya ndugu zao, wakajitakasa, wakaingia, kama alivyoamuru mfalme kwa maneno ya Bwana, ili waisafishe nyumba ya Bwana.
16 Nao makuhani wakaingia nyumbani mwa Bwana, katika mahali pa ndani, ili waisafishe, wakatoa uchafu wote waliouona hekaluni mwa Bwana, wakautupa nje uani mwa nyumba ya Bwana. Walawi wakautwaa, ili wauchukue nje mpaka kijito cha Kidroni.
17 Basi wakaanza kutakasa siku ya kwanza ya mwezi wa kwanza, hata siku ya nane ya mwezi wakafika katika ukumbi wa Bwana; wakaitakasa nyumba ya Bwana katika muda wa siku nane; wakamaliza siku ya kumi na sita ya mwezi wa kwanza.
18 Wakaingia ndani kwa Hezekia mfalme, wakasema, Tumeisafisha nyumba yote ya Bwana, na madhabahu ya sadaka ya kuteketezwa, pamoja na vyombo vyake vyote, na meza ya mikate ya wonyesho, pamoja na vyombo vyake vyote.
19 Tena vyombo vyote alivyovitupa mfalme Ahazi alipotawala, hapo alipoasi, tumevitengeza na kuvitakasa; navyo, tazama, vipo mbele ya madhabahu ya Bwana.
20 Ndipo Hezekia mfalme akaamka mapema, akakusanya wakuu wa mji, akapanda nyumbani kwa Bwana.
21 Wakaleta ng'ombe waume saba, na kondoo waume saba, na wana-kondoo saba, na mabeberu saba, kuwa sadaka ya dhambi kwa ajili ya ufalme, na kwa ajili ya patakatifu, na kwa ajili ya Yuda. Akaamuru makuhani, wana wa Haruni, wawatoe madhabahuni pa Bwana.
22 Basi wakawachinja ng'ombe, na makuhani wakaipokea damu, wakainyunyiza madhabahuni; wakawachinja kondoo waume, na kuinyunyiza damu madhabahuni; wakawachinja na wana-kondoo, na kuinyunyiza damu madhabahuni.
23 Wakawaleta karibu mabeberu wa sadaka ya dhambi mbele ya mfalme na kusanyiko; wakawawekea mikono yao;
24 na makuhani wakawachinja, wakaitoa damu yao kuwa sadaka ya dhambi madhabahuni, ili kuwafanyia Israeli wote upatanisho; maana mfalme aliamuru Israeli wote wafanyiwe sadaka ya kuteketezwa na sadaka ya dhambi.
25 Akawasimamisha Walawi nyumbani mwa Bwana wenye matoazi, wenye vinanda, na wenye vinubi, kama alivyoamuru Daudi, na Gadi mwonaji wa mfalme, na Nathani nabii; kwani Bwana aliamuru hivi kwa manabii wake.
26 Wakasimama Walawi wenye vinanda vya Daudi, na makuhani wenye mapanda.
27 Hezekia akaamuru kutoa sadaka ya kuteketezwa madhabahuni. Na wakati ilipoanza sadaka hiyo ya kuteketezwa, ukaanza na huo wimbo wa Bwana, na mapanda, pamoja na vinanda vya Daudi mfalme wa Israeli.
28 Na kusanyiko lote wakaabudu, waimbaji wakaimba, wenye mapanda wakapiga; haya yote yakaendelea hata ilipomalizika sadaka ya kuteketezwa.
29 Hata walipokwisha kutoa sadaka, mfalme, na hao wote waliokuwapo naye, wakasujudia, wakaabudu.
30 Tena Hezekia mfalme na wakuu wakawaamuru Walawi, wamwimbie Bwana sifa kwa maneno ya Daudi, na ya Asafu mwonaji. Wakaimba sifa kwa furaha, wakainama vichwa, wakaabudu.
31 Ndipo Hezekia akajibu, akasema, Sasa mmejifanya wakfu kwa Bwana, karibuni mkalete dhabihu na matoleo ya shukrani nyumbani mwa Bwana. Basi kusanyiko wakaleta dhabihu na matoleo ya shukrani; na wote wenye moyo wa ukarimu, wakaleta sadaka za kuteketezwa.
32 Na hesabu ya sadaka hizo za kuteketezwa walizozileta kusanyiko ikawa ng'ombe waume sabini, kondoo waume mia, na wana-kondoo mia mbili; hao wote walikuwa ni sadaka ya kuteketezwa kwa Bwana.
33 Na vitu vitakatifu vilikuwa ng'ombe mia sita, na kondoo elfu tatu.
34 Lakini makuhani walikuwa wachache, wasiweze kuchuna sadaka zote za kuteketezwa; basi ndugu zao Walawi wakawasaidia, hata ilipokwisha kazi, na hata makuhani walipojitakasa; kwa kuwa Walawi walikuwa wenye mioyo ya adili kwa kujitakasa kuliko makuhani.
35 Na tena sadaka za kuteketezwa nazo zilikuwa nyingi, pamoja na mafuta ya sadaka za amani, na sadaka za kinywaji kwa kila sadaka ya kuteketezwa. Hivyo ikatengezeka huduma ya nyumba ya Bwana.
36 Akafurahi Hezekia, na watu wote, kwa sababu ya hayo Mungu aliyowatengenezea watu; maana jambo hilo likawa kwa ghafula.

NILICHOGUNDUA NA KUJIFUNZA:

1. Hezekia alianza kipindi cha utawala wake kwa kuwarejesha watu madhabahuni. Huduma zilizokuwa zimekoma zikafufuliwa. Matengenezo ya kweli huanza na ibada. Ibada iliyokoma nyumbani kwako huu ndiyo wakati wa kuifufua. Nunua Biblia, Nunua kitabu cha Nyimbo, nunua na Mwongozo wa Kujifunza Biblia.
2. Kuna nyakati ambazo watu hugeuzia mbali nyuso zao na makao ya Bwana kumpa maungo tu. Wengine huwapeleka watoto wao kanisani wenyewe wakibaki nyumbani. Na wengine huja ibadani bila sadaka. Mambo hayo yanahitaji matengenezo. Mungu anawatarajie watu hao watambue umuhimu wake maishani mwao. Mungu akiwa wa kwanza maishani mwako atavifanya vingine vyote kushika nafasi ya kwanza.
3. Wale ambao Mungu amewachagua kuwa viongozi wa kiroho wameitwa ili kumtumikia Mungu. Kila wakifanyacho wahesabu kuwa wanakifanya kwa Mungu na si kwa wanadamu. Wanamtumikia Mungu aliyeziumba mbingu na nchi. Hii ndiyo heshima ya juu zaidi awezayo kupewa mwanadamu.
4. Upo wakati wa kuweka upya agano lako na Mungu. Unapoona mambo yako hayaendi kama ilivyotarajiwa. Wakati mikosi inapokuandama. Huu ndiyo wakati wa kujitathmini na kujitakasa. Kujidhili kwa namna hiyo kwaweza kuepusha mabaya mengi na kufungua ukurasa mpya wa maisha.
 
 


USOMAJI BIBLIA KWA MPANGO: MATHAYO 9:1-38 IJUMAA, 07/05/2021
 1 Akapanda chomboni, akavuka, akafika mjini kwao.
 2 Na tazama, wakamletea mtu mwenye kupooza, amelala kitandani; naye Yesu, alipoiona imani yao, alimwambia yule mwenye kupooza, Jipe moyo mkuu, mwanangu, umesamehewa dhambi zako.
 3 Na tazama, baadhi ya waandishi wakasema nafsini mwao, Huyu anakufuru.
 4 Naye Yesu, hali akijua mawazo yao, akasema, Mbona mnawaza maovu mioyoni mwenu?
 5 Kwa maana rahisi ni lipi, ni kusema, Umesamehewa dhambi zako, au ni kusema, Ondoka, uende?
 6 Lakini mpate kujua ya kwamba Mwana wa Adamu anayo amri duniani ya kusamehe dhambi, (amwambia yule mwenye kupooza) Ondoka, ujitwike kitanda chako, uende nyumbani kwako.
 7 Akaondoka, akaenda zake nyumbani kwake.
 8 Makutano walipomwona, walishikwa na hofu, wakamtukuza Mungu, aliyewapa watu amri ya namna hii.
 9 Naye Yesu alipokuwa akipita kutoka huko aliona mtu ameketi forodhani, aitwaye Mathayo, akamwambia, Nifuate. Akaondoka, akamfuata.
 10 Ikawa alipoketi nyumbani ale chakula, tazama, watoza ushuru wengi na wenye dhambi walikuja wakaketi pamoja na Yesu na wanafunzi wake.
 11 Mafarisayo walipoona, waliwaambia wanafunzi wake, Mbona mwalimu wenu anakula pamoja na watoza ushuru na wenye dhambi?
 12 Naye aliposikia, aliwaambia, Wenye afya hawahitaji tabibu, bali walio hawawezi.
 13 Lakini nendeni, mkajifunze maana yake maneno haya, Nataka rehema, wala si sadaka; kwa maana sikuja kuwaita wenye haki, bali wenye dhambi.
 14 Wakati ule wanafunzi wake Yohana wakamwendea, wakasema, Kwa nini sisi na Mafarisayo twafunga, bali wanafunzi wako hawafungi?
 15 Yesu akawaambia, Walioalikwa arusini wawezaje kuomboleza, muda bwana arusi akiwapo pamoja nao? Lakini siku zitakuja watakapoondolewa bwana arusi; ndipo watakapofunga.
 16 Hakuna mtu atiaye kiraka cha nguo mpya katika vazi kuukuu; maana kile kilichotiwa huondoa kipande cha lile vazi, na pale palipotatuka huzidi.
 17 Wala watu hawatii divai mpya katika viriba vikuukuu; na kama wakitia, vile viriba hupasuka, divai ikamwagika, na viriba vikaharibika; bali hutia divai mpya katika viriba vipya, vikahifadhika vyote.
 18 Alipokuwa akiwaambia hayo, tazama, akaja jumbe mmoja, akamsujudia, akisema, Binti yangu sasa hivi amekufa; lakini njoo, uweke mkono wako juu yake, naye ataishi.
 19 Akaondoka Yesu, akamfuata, pamoja na wanafunzi wake.
 20 Na tazama, mwanamke aliyekuwa na ugonjwa wa kutoka damu muda wa miaka kumi na miwili, alikuja kwa nyuma, akaugusa upindo wa vazi lake.
 21 Kwa maana alisema moyoni mwake, Nikigusa tu upindo wa vazi lake nitapona.
 22 Yesu akageuka, akamwona, akamwambia, Jipe moyo mkuu, binti yangu; imani yako imekuponya. Yule mwanamke akapona tangu saa ile.
 23 Yesu alipofika nyumbani kwa yule jumbe, aliona wapiga filimbi, na makutano wakifanya maombolezo,
 24 akawaambia, Ondokeni; kwa maana kijana hakufa, amelala tu. Wakamcheka sana.
 25 Lakini makutano walipoondoshwa, aliingia, akamshika mkono; yule kijana akasimama.
 26 Zikaenea habari hizi katika nchi ile yote.
 27 Yesu alipokuwa akipita kutoka huko, vipofu wawili wakamfuata wakipaza sauti, wakisema, Uturehemu, Mwana wa Daudi.
 28 Naye alipofika nyumbani, wale vipofu walimwendea; Yesu akawaambia, Mnaamini kwamba naweza kufanya hili? Wakamwambia, Naam, Bwana.
 29 Ndipo alipowagusa macho, akasema, Kwa kadiri ya imani yenu mpate.
 30 Macho yao yakafumbuka. Naye Yesu akawaagiza kwa nguvu, akisema, Angalieni hata mtu mmoja asijue.
 31 Lakini wakatoka, wakaeneza habari zake katika nchi ile yote.
 32 Hata hao walipokuwa wakitoka, tazama, walimletea mtu bubu mwenye pepo.
 33 Na pepo alipotolewa, yule bubu alinena, makutano wakastajabu, wakasema, Haijaonekana hivi katika Israeli wakati wo wote.
 34 Lakini Mafarisayo wakasema, Kwa nguvu za mkuu wa pepo atoa pepo.
 35 Naye Yesu alikuwa akizunguka katika miji yote na vijiji, akifundisha katika masinagogi yao, na kuihubiri habari njema ya ufalme, na kuponya magonjwa yote na udhaifu wa kila aina.
 36 Na alipowaona makutano, aliwahurumia, kwa sababu walikuwa wamechoka na kutawanyika kama kondoo wasio na mchungaji.
 37 Ndipo alipowaambia wanafunzi wake, Mavuno ni mengi, lakini watenda kazi ni wachache.
 38 Basi mwombeni Bwana wa mavuno, apeleke watenda kazi katika mavuno yake.

 MASWALI YA KUJADILI:

1. Je Yesu anapaswa kushauriana na nani ili akusamehe dhambi? Kwa nini tangu mwanzo Yesu hakuonekana kuwa na hadhi ya Mungu? (Isaya 53:3)

2. "Jipe moyo mwanangu" na "Jipe moyo binti yangu" ni maneno aliyoyatumia Yesu kabla ya kuwaponya wagonjwa aliokutana nao. Jambo hili linakupa hisia gani kuhusu tabia ya Yesu kwa watu wanaopitia changamoto?