Seventh-day Adventist® Church

PASTOR LETTA'S OFFICIAL WEBSITE

Menu

SIKU 10 ZA MAOMBI


SIKU 10 ZA MAOMBI MWAKA 2020 (08 - 18/01/2020)


KUTAFUTA ROHO WA MUNGU

MWONGOZO WA KIONGOZI


Karibu katika Siku Kumi za Maombi 2020! Tuna shukrani sana kwamba tunaweza kuanza mwaka huu kwa maombi. Mungu ametenda miujiza mingi katika miaka iliyopita kadri tulivyokuwa tukimtafuta katika maombi na kufunga. Roho Mtakatifu amewezesha uamsho, mabadiliko, hisia za uinjilisti zilizojengwa upya, na mahusiano yaliyoponywa. Kwa kweli, katika maombi ndipo mahali uamsho unapozaliwa!

Tunaamini kwamba maisha yako na ya wale unaowaombea, yatabadilishwa kadri unavyojumuika na washiriki wenzako katika maombi kwa ajili ya umwagwaji wa Roho Mtakatifu, ambaye Baba aliahidi kuwapatia wale watakaomuomba. Hapa kuna baadhi ya shuhuda tatu tu kutoka kwa wale walioshiriki katika Siku Kumi za Maombi za mwaka uliopita.

N.K. kutoka Zambia

Katika siku ya tatu ya kipindi cha Siku Kumi za Maombi, nilikuwa nikiomba mbele ya kusanyiko nilipoombwa kuomba kwa ajili ya uingiliaji kati wa Mungu ulio mtakatifu. “Kuna mtu yupo katika mchakato wa kusitisha maisha yake,” niliomba. “Baba mpendwa, tafadhali usimruhusu kufanikiwa. Tafadhali ingilia kati.” Siku iliyofuata nilishtuka kugundua kwamba shangazi yangu alijaribu kujiua. Lakini kwa sababu ya maombi yetu, Mungu aliingilia kati na kuokoa maisha yake. Ninapoandika ushuhuda huu, shangazi yangu ni mzima na Mungu anatenda kazi katika maisha yake. Sote tunamsifu Bwana kwa jibu lake la muujiza kwa ombi letu.

J.J. kutoka North Carolina, Marekani:

Wakati wa Siku Kumi za Maombi mwaka 2018, rafiki yangu Alicia aliomba kwa ajili ya watu watano mahususi ili waje kwa Kristo. Mungu alijibu maombi yake mengi, lakini bado jina moja kwenye orodha yake, jina la dada yake, halikuitikia. Hata hivyo, mwaka huu katika Siku Kumi za Maombi, dada yake Alicia alikuja katika mikutano ya maombi na kujisalimisha kwa Yesu. Hivi sasa anajifunza Masomo ya Biblia na anajiandaa kwa ajili ya ubatizo. Pia, watu wengine wawili waliohudhuria katika mikutano ya Siku Kumi za Maombi wamejitoa kwa ajili ya ubatizo. Tunamsifu Mungu kwa kazi yake na kwa huduma ya Siku Kumi za Maombi. Kwa kweli sote tulipata uzoefu wa kina Zaidi na Yesu kadri kulivyokusanyika pamoja katika maombi.

Muumini katika Asia:

Siku Kumi za Maombi zilipokuwa zikiendelea, niliomba kwa Baba yetu wa Mbinguni anipatie fursa ya kusambaza ujumbe wa Kiadventista… Baada ya kuomba katika Siku Kumi za Maombi, nilitoa ujumbe wa Kiadventista kwa kundi kubwa lisilokuwa na historia ya Ukristo, na wameukubali ujumbe. Nilipokea jibu kwa ombi langu. Ni ushuhuda wangu mkuu baada ya Siku hizi Kumi za Maombi. Bwana Asifiwe.

Mambo ya kawaida ya maombi katika siku kumi za maombi

Ukurasa wa Wazo la Kila Siku


Ukurasa wa wazo umeandaliwa kwa ajili ya kila siku katika siku hizi kumi. Hujumuisha fungu la Biblia, ushuhuda wa ibada, mafungu ya Biblia ya kuombea, mapendekezo ya maombi, na mapendekezo ya nyimbo. Tunapendekeza kwamba unatoe nakala ya kurasa za wazo kuu ili kila mshiriki aweze kuwa na nakala ya kufuatisha katika muda wa maombi. Kurasa zote za wazo la kila siku zinapatikana pia moja kwa moja kwa kompyuta au simu kwenye tovuti ya www.tendaysofprayer.org.

Makanisa ulimwenguni yataungana katika kuomba kuhusu wazo kuu la kila siku.  Ungana nao katika kuomba kupitia mafungu, nukuu, na maombi katika kila ukurasa wa wazo la siku husika. Mnaweza kugawanyika katika makundi madogo na kila kundi kuombea sehemu ya orodha.

Baadhi ya maombi huhusiana mahususi na Kanisa la Waadventista wa Sabato la Kiulimwengu. Ni muhimu kuomba pamoja kwa ajili ya familia ya kanisa letu, lakini unaweza kutumia muda wa maombi kwa kutumia maombi ya kawaida ikiwa kundi lako linajumuisha wageni kutoka kwenye jamii. Omba kuhusu namna unavyoweza kuwakaribisha wageni kwa ubora Zaidi na kuwafanya kujiskia kama sehemu ya kundi hilo.

Muda unaopendekezwa kwa ajili ya kila Kipengele cha Maombi

Kiasi cha muda utakaotumika katika kila kipengele cha maombi kwa hakika kitatofautiana kidogo kila wakati mtakapoomba pamoja. Dakika zifuatazo ni mapendekezo ya muda unaofaa zaidi: 

  1. Kukaribisha/Utangulizi – dakika 2 hadi 5

  2. Usomaji wa “Ushuhuda” (tazama ukurasa wa wazo la siku) – dakika 3 hadi 5

  3. Kuomba Kupitia “Mafungu ya Biblia ya Kuombea” (tazama ukurasa wa wazo la siku) – dakika 3 hadi 5

  4. Kipindi Cha Ibada Ya Kusifu Katika Maombi – dakika 10 

  5. Kipindi Cha Toba Na Kuungama Pamoja Na Kudai Ushindi Dhidi Ya Dhambi – dakika 3 hadi 5

  6. Kipindi cha kujitoa na kuingilia kati kwa maombi (tazama “Mapendekezo ya Maombi” katika ukurasa wa wazo la siku) – dakika 20 hadi 30

  7. Kipindi Cha Shukrani Katika Maombi – dakika 10

Kumsihi Mungu na kuomba kwa ajili ya Watu Saba Uliowachagua

Hamasisha kila mtu amwombe Mungu amwonyeshe watu saba atakaowaombea katika siku hizi kumi za maombi. Hawa wanaweza kuwa wanafamilia, marafiki, wafanyakazi, washiriki, n.k. Wahamasishe watu kumwomba Roho Mtakatifu awaongoze hawa saba anaowaombea wadumu katika Kristo. Wanakikundi pia wanapaswa kumwomba Mungu awaonyeshe namna wanavyoweza kuomba kwa ajili ya mahitaji mahususi na kuwafikia watu hao saba katika kipindi cha siku hizi kumi. Unaweza kutoa kadi au vikaratasi ambavyo watu watatumia kuandika majina saba watakayokuwa wakiombea.

Huduma ya Sabato katika Kipindi cha Siku Kumi za Maombi mwaka 2019

Maombi na yalenge katika kitu mahususi na mshiriki shuhuda mbali mbali jinsi Mungu alivyojibu maombi katika kipindi kile cha huduma za ibada Sabato zote mbili. Kuwa mbunifu – kuna namna nyingi za kushiriki pamoja na familia ya kanisa mambo yanayotokea watu wanapokutana katika maombi kila siku.

Sherehe za Sabato ya Kuhitimisha

Sabato ya mwisho, hasa, inapaswa kutayarishwa kama muda wa kufurahi sana kwa yale yote Mungu aliyotenda katika siku hizi kumi. Tenga muda wa kutosha kwa ajili ya shuhuda za maombi yaliyojibiwa, mafundisho, na mahubiri ya Biblia kuhusu maombi, na nyimbo. Ongoza kusanyiko katika muda wa maombi ili kwamba hata wale ambao hawakuhudhuria mikutano ya kila siku waweze kupata uzoefu wa furaha ya kuomba pamoja na wengine. Tafadhali tazama mwongozo wa Sherehe za Sabato kwa taarifa zaidi.

Kufuatilia kipindi hiki cha maombi ya siku kumi mwaka 2020

Omba kuhusu namna Mungu anavyotaka kanisa au kikundi chako kuendeleza kile Alichoanzisha katika kipindi cha Siku Kumi za Maombi za mwaka huu 2020. Pengine mtaendelea kukutana kila juma kwa ajili ya maombi. Au pengine Mungu anataka uanze huduma mpya ndani ya kanisa lako au ya kuifikia jamii. Kuwa muwazi na fuata kule Mungu anapoelekeza. Hakika utashangazwa kadiri unavyotembea pamoja naye. Tumejumuisha changamoto ya kuwafikia wengine walio nje, pamoja na mapendekezo mwishoni mwa Mwongozo huu wa Kiongozi.

Ushuhuda

Tafadhali shiriki visa vya namna Mungu alivyotenda kazi katika Siku Kumi za Maombi! Visa vyako vitakuwa msaada na hamasa kwa wengine wengi. Unaweza kutuma visa vya kwa stories@ministerialassociation.org au kutumwa mtandaoni kwenye tovuti ya www.tendaysofprayer.org. 

Vielekezi vya kuunganika katika maombi

Kubalianeni:

Mtu anapoombea hitaji fulani kwa Mungu, hakikisha kuwa wengine pia wanaombea hitaji hilo hilo na kukubaliana – kufanya hivi kuna nguvu! Usifikiri kwamba kwa sababu mtu mmoja ameomba kuhusu hitaji hilo, hakuna haja ya mwingine kuliombea. “Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni” (Mathayo 18:19). Inatia moyo kiasi gani kuinuliwa katika maombi!

Kudai Ahadi za Mungu

Utakuta ahadi za Biblia zinazohusiana na mada husika zimejumuishwa katika kila kitini. Himiza kikundi kudai ahadi za Mungu kadiri wanavyoomba. Ni rahisi sana kujielekeza katika matatizo yetu. Lakini tunapodai ahadi za Mungu, tunaongeza imani yetu na kujikumbusha kwamba hakuna kinachoshindikana kwa Mungu. Ahadi hizo hutusaidia kuondoa macho yetu kwenye madhaifu na magumu tunayokabiliana nayo, na kuyaelekeza kwa Yesu. Tunaweza kupata ahadi za Biblia za kudai kwa kila udhaifu na kila pambano. Himiza watu kutafuta ahadi nyingi zaidi iwezekanavyo na kuziandika ili kwamba waweze kuzidai wakati ujao.

Kufunga

Alika wale wanaoungana nawe katika Siku Kumi za Maombi kufikiria aina ya kufunga watakayopendelea, kwa mfano kufunga kutazama televisheni, muziki wa kidunia, filamu, mtandao, vitu vitamu vitamu kama vile pipi, au aina nyingine ya vyakula ambavyo ni vigumu kumeng’enywa. Kutumia muda wa ziada kuomba na kujifunza Biblia, ukimuomba Mungu akusaidie wewe na kusanyiko lako kudumu zaidi katika Kristo. Kwa kuchagua mlo mwepesi, tunaruhusu akili zetu kuwa sikivu zaidi kwa sauti ya Roho Mtakatifu.

Roho Mtakatifu

Hakikisha unamwomba Roho Mtakatifu akuonyeshe jambo la kuombea katika maisha ya mtu au katika hali fulani. Bibia inatuambia kwamba hatufahamu tuombee nini, na kwamba Roho Mtakatifu ndiye anayetuombea. “Hatupaswi kuomba tu kwa jina la Kristo, bali kwa uvuvio wa Roho Mtakatifu. Hii huelezea maana halisi tunaposema kuwa Roho “hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.” (Warumi 8:26). Mungu hufurahia kujibu ombi kama hilo. Tunapoomba kwa dhati na kwa nguvu tunaomba kwa jina la Kristo, katika nguvu hiyo kuna ahadi kutoka kwa Mungu kwamba anakaribia kujibu maombi yetu ‘zaidi ya tuyaombayo au tuyawazayo’ (Waefeso 3:20)” (Christ Object Lessons, uk. 147, msisitizo umeongezewa).

Kuwa pamoja Kimwili

Unapokuwa unaanza kipindi cha maombi ya pamoja, ni vema kualika kila mmoja asogee karibu. Watu wanaposogeleana na kutengeneza duara, inasaidia kukuza roho ya umoja, ambayo ni muhimu sana kwa maombi ya pamoja. Ni ngumu kusikia maombi anayoomba mwingine ikiwa watu wametawanyika sana kwenye chumba.

Kutunza Taarifa ya Maombi

Kutunza daftari la kumbukumbu ya maombi kwenye kipindi chote cha Siku Kumi za Maombi kunaweza kuwa njia bora ya washiriki kuweka moyoni wazo kuu la maombi ya kila siku, kufanya maagano thabiti na Mungu, na kutambua mibaraka yake kwao. Kuandika maombi yetu na kutunza kumbukumbu ya majibu ya Mungu ni njia iliyothibitishwa ya kutia moyo.

Ikiwa utapenda, utunzaji wa kumbukumbu unaweza kujumuishwa kwa namna mbalimbali katika Siku Kumi za Maombi. Unaweza kutenga muda wakati mnapokutanika kwa ajili ya maombi, ili watu wapate kuandika mwitikio wao kwa Mungu kwenye shajara zao binafsi za maombi. Au unaweza kutunza shajara ya kikundi ya maombi na majibu – inaweza kuwa ni daftari, au bango kubwa, au kutunzia mtandaoni. Njia rahisi ya kufanya hivi ni kuchora msitari katikati ya karatasi kubwa. Andika maombi kwenye upande wa kushoto na majibu upande wa kulia. Inafurahisha na pia inajenga imani unapotazama nyuma na kuona jinsi Mungu alivyojibu maombi!

Kicho

Himiza na kujenga mtazamo wa kicho na unyenyekevu. Tunakaribia chumba chenye kiti cha enzi cha Mfalme wa ulimwengu. Hebu tusitumie muda huu vibaya kwa mkao wetu na kwa mwenendo wetu na hata katika mazungumzo yetu. Hata hivyo, siyo lazima kila mmoja apige magoti muda wote. Unahitaji watu wawe huru kwa saa moja, hivyo wahamasishe watu kupiga magoti au kukaa au kusimama kadiri Mungu atakavyokuongoza na wanavyokuwa huru zaidi.

Maombi kwa Sentensi 

Maombi na yawe mafupi, na yaelekezwe moja kwa moja kwenye hitaji. Kufanya hivi kutawapatia wengine pia fursa ya kuomba. Jaribu kufupisha ombi lako kwa sentensi chache, kila mmoja anaweza kuomba mara kadhaa. Maombi mafupi yatafanya kipindi cha maombi kuwa cha kufurahisha na sio cha kuchosha huku mkimruhusu Roho Mtakatifu kugusa vikundi na kuwaongoza akiwaonesha namna ya kuomba. Sio lazima kuanza na kumaliza kwa maneno “Mungu wetu mpendwa” na “Amina” kwa sababu ni mawasiliano endelevu na Mungu.

Ukimya

Wewe kama kiongozi usitawale kipindi cha maombi. Lengo kubwa ni kuwawezesha wengine kuomba. Kipindi cha ukimya kina thamani kubwa ajabu, kwani kinampa Mungu muda wa kuzungumza na mioyo yetu. Ruhusu Roho Mtakatifu afanye kazi kwa kumpa kila mmoja muda wa kutosha wa kuomba.

Kuimba

Nyimbo za hapa na pale kutoka kwa vikundi zikichanganywa kwenye maombi, zinaongezea uzuri wa mkutano wa maombi. Nyimbo zinazofaa zimeorodheshwa mwisho wa kila ukurasa wa wazo la siku. Usihisi kwamba unahitaji kutumia nyimbo zote – haya ni mapendekezo tu. Kuimba pia ni njia nzuri ya kuhama kutoka kwenye kipindi kimoja kwenda kwenye kipindi kingine.

Kukusanya Mahitaji ya Kuombea

Usiulizie mahitaji ya kuombea kutoka kwenye kikundi. Badala yake, waambie watu wataje mahitaji yao katika maombi na kuwahimiza wengine kujiunga wakikubaliana nayo kwa kuungana katika maombi kimya kimya. Sababu kubwa ni kwamba, muda unaweza usitoshe kwa kuombea mahitaji ya mtu mmoja mmoja. Ukitaka kuzungumza kuhusu mahitaji ya kila mmoja unaweza kutumia muda wote wa maombi. Shetani anafurahi anapoona tunatumia muda wa maombi kuzungumza kuhusu matatizo yetu badala ya kuombea hayo matatizo. Wanakikundi wanaweza kuanza kushauriana na kupendekeza ufumbuzi. Uwezo unatoka kwa Mungu. Kadiri tunavyoongeza maombi ndivyo anavyoachia uwezo wake. 

Muda wako wa kila siku

Ni muhimu sana! Hakikisha wewe kama kiongozi unatumia muda wako mwingi miguun pa Yesu, ukizungumza naye na kusoma Neno lake. Ikiwa utafanya kumfahamu Mungu kuwa kipaumbele chako katika maisha, utafunguliwa uzoefu ulio mzuri wa ajabu. “Kutoka katika sehemu ya siri ya maombi ilitoka Nguvu ya ajabu iliyotikisha dunia na kuleta matengenezo makuu. Hapo, kwa utulivu mtakatifu, watumishi wa Bwana waliweka miguu yao katikka mwamba wa ahadi zake” (The Great Controversy, uk. 210)


Changamoto za Kuwafikia watu walio nje katika Siku Kumi za Maombi

Kila mmoja anaweza kufanya kitu ili kuharakisha ujio wa Yesu kupitia Kuhusishwa kwa Washiriki Wote (TMI) “Kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia” (Mathayo 25:35, 36).

Katika kitabu cha Huduma ya Uponyaji (The Ministry of Healing) tunasoma kuwa, “Tunapaswa kuishi maisha yenye sura mbili – maisha ya mawazo na matendo, na maisha ya maombi ya kimya na kazi inayofanywa kwa juhudi” (uk. 512). Ni faida kwetu kuwaonyesha wengine upendo wa Yesu. Tumepokea vitu vingi sana kutoka kwa Mwokozi wetu; hebu tusivitunze kwa ajili yetu wenyewe. Hebu tuwashirikishe watu wengine upendo wake.

Tunakuhimiza wewe na kanisa lako kumuuliza Mungu katika maombi namna unavyoweza kuwafikia wengine katika Siku hizi Kumi za Maombi. Chagua shughuli moja au shughuli kadhaa, na uchague siku, ili uwe mikono na miguu ya Yesu. Unapokuwa ukifanya kazi ya kupanga kila kitu, epuka kuruhusu shughuli hizi kukufanya ushindwe kuomba. “Unapoweka jitihada kwa ajili ya wengine, anza kwa maombi mengi ya siri; kwani ili kuelewa sayansi ya kuokoa roho unahitaji hekima kubwa. Kabla ya kuwasiliana na watu, wasiliana na Kristo. Pata maandalizi ya kuhudumia kwa watu kutoka katika kiti cha enzi cha neema ya kimbingu.” (Maombi, uk. 313).

Tumeandaa orodha ya njia unazoweza kutumia kusaidia wengine. Chagua njia yo yote utakayoona inakidhi mahitaji ya wale unaokwenda kuwahudumia. Kuwa huru kufanya kitu ambacho hakijaorodheshwa ikiwa utaona kinafaa zaidi.

  1. Mpikie mgonjwa chakula. 
  2. Mkaribishe jirani/mfanyakazi mwenzako kwenye kusanyiko la kijamii.
  3. Mpatie chakula mtu asiye na makazi. 
  4. Tafuta mzee mmoja. Mtembelee kila siku na umsaidie kazi, kununua mahitaji, kupika, au kazi za bustani. 
  5. Oka mkate na ushiriki huo mkate na jirani. 
  6. Saidia kwenye miradi katika maeneo yanayokuzunguka. 
  7. Jitolee kukaa na mgonjwa au mtu asiyejiweza ili wale wanaomhudumia waweze kufanya shughuli zingine. 
  8. Jitambulishe kwa jirani mpya aliyehamia maeneo yenu na kumpelekea chakula. Mfanye ajisikie kukaribishwa katika maeneo hayo. 
  9. Nunua mahitaji ya jikoni na uyapeleke kwenye familia yenye uhitaji. 
  10. Toa msaada miwani yako ya zamani.
  11. Jitolee kutoa masomo ya Biblia
  12. Tembelea watu katika sehemu za kutunzia watu.
  13. Mpatie mwanafunzi fedha ya “chakula.”
  14. Kusanya nguo kwa ajili ya wahitaji. Unaweza kuanzisha kabati la nguo kanisani kwako kwa ajili ya kushirki na wale walio na uhitaji.
  15. Toa msaada kompyuta yako au vifaa vingine vya kielektroniki.
  16. Toa msaada gari lako lililotumika.
  17. Andaa “Tamasha la Kupima Afya.”
  18. Tuma kadi kwa mtu aliyefungiwa ndani.
  19. Andaa mfululizo wa mambo ya uinjilisti.
  20. Mpatie mtu kitabu unachodhani angekipenda.
  21. Wapigie simu jirani zako na kuwajulia hali.
  22. Gawa vijarida na vijuzuu kwa watu. Vinapatiakana: www.glowonline.org/glow
  23. Mwalike mtu kumpokea Yesu.
  24. Endesha darasa la mapishi.
  25. Fanya “Mradi wa machapisho 28.” Katika Juma la kwanza, gawa kitabu kimoja. Juma la pili, gawa vitabu viwili. Juma la tatu, gawa vitabu vitatu. Endelea hadi utakapogawa vitabu vyote 28.
  26. Mpelekee chakula mtu aliyepoteza (aliyefiwa na) mpendwa wake.
  27. Mtembelee mtu hospitali ili kumtia moyo au kumsaidia kwa namna moja au nyingine.
  28. Msomee mzee kitabu.
  29. Tembelea makazi ya watoto na toa msaada kwa wafanyakazi wa hapo.
  30. Anza kundi la kushona/kufuma ili kutengeneza nguo kwa ajili ya wahitaji.
  31. Soma Biblia kwa sauti kwa ajili ya mtu asiyeona au asiyeweza kusoma. 
  32. Endesha usiku wa vijana nyumbani kwako.
  33. Toa makazi kwa watu walionyanyaswa.
  34. Gawa baadhi ya vitabu kwenye makazi ya watoto.
  35. Panga na kusimamia siku ya kufurahi kwa ajili ya watoto na wenye mahitaji maalumu pamoja na familia zao.
  36. Andaa siku ya kufanya usafi katika jamii.
  37. Anzisha chama cha afya katika kanisa lako. Alika marafiki na majirani.
  38. Muulize mtu kama angependa kuungana na wewe kutazama mkanda wenye ujumbe wa kiroho. Kadiri mnavyotazama pamoja, omba kwamba Roho Mtakatifu anene na moyo wa mtu huyo.
  39. Buni mradi wako mwenyewe. Kwa vitendea kazi zaidi juu ya ushuhudiaji, tembelea  www.revivalandreformation.org/resources/witnessing  


UTANGULIZI:

Karibu katika Siku Kumi za Maombi 2020! Tuna shukrani sana kwamba tunaweza kuanza mwaka huu kwa maombi. Mungu ametenda miujiza mingi katika miaka iliyopita kadri tulivyokuwa tukimtafuta katika maombi na kufunga. Roho Mtakatifu amewezesha uamsho, mabadiliko, hisia za uinjilisti zilizojengwa upya, na mahusiano yaliyoponywa. Kwa kweli, katika maombi ndipo mahali uamsho unapozaliwa!

Tunaamini kwamba maisha yako na ya wale unaowaombea, yatabadilishwa kadri unavyojumuika na washiriki wenzako katika maombi kwa ajili ya umwagwaji wa Roho Mtakatifu, ambaye Baba aliahidi kuwapatia wale watakaomuomba. Hapa kuna baadhi ya shuhuda tatu tu kutoka kwa wale walioshiriki katika Siku Kumi za Maombi za mwaka uliopita.

N.K. kutoka Zambia:

Katika siku ya tatu ya kipindi cha Siku Kumi za Maombi, nilikuwa nikiomba mbele ya kusanyiko nilipoombwa kuomba kwa ajili ya uingiliaji kati wa Mungu ulio mtakatifu. “Kuna mtu yupo katika mchakato wa kusitisha maisha yake,” niliomba. “Baba mpendwa, tafadhali usimruhusu kufanikiwa. Tafadhali ingilia kati.” Siku iliyofuata nilishtuka kugundua kwamba shangazi yangu alijaribu kujiua. Lakini kwa sababu ya maombi yetu, Mungu aliingilia kati na kuokoa maisha yake. Ninapoandika ushuhuda huu, shangazi yangu ni mzima na Mungu anatenda kazi katika maisha yake. Sote tunamsifu Bwana kwa jibu lake la kimuujiza kwa ombi letu.

J.J. kutoka North Carolina, Marekani:

Wakati wa Siku Kumi za Maombi mwaka 2018, rafiki yangu Alicia aliomba kwa ajili ya watu watano mahususi ili waje kwa Kristo. Mungu alijibu maombi yake mengi, lakini bado jina moja kwenye orodha yake, jina la dada yake, halikuitikia. Hata hivyo, mwaka huu katika Siku Kumi za Maombi, dada yake Alicia alikuja katika mikutano ya maombi na kujisalimisha kwa Yesu. Hivi sasa anajifunza Masomo ya Biblia na anajiandaa kwa ajili ya ubatizo. Pia, watu wengine wawili waliohudhuria katika mikutano ya Siku Kumi za Maombi wamejitoa kwa ajili ya ubatizo. Tunamsifu Mungu kwa kazi yake na kwa huduma ya Siku Kumi za Maombi. Kwa kweli sote tulipata uzoefu wa kina Zaidi na Yesu kadri kulivyokusanyika pamoja katika maombi.

Muumini katika Asia:

Siku Kumi za Maombi zilipokuwa zikiendelea, niliomba kwa Baba yetu wa Mbinguni anipatie fursa ya kusambaza ujumbe wa Kiadventista… Baada ya kuomba katika Siku Kumi za Maombi, nilitoa ujumbe wa Kiadventista kwa kundi kubwa lisilokuwa na historia ya Ukristo, na wameukubali ujumbe. Nilipokea jibu kwa ombi langu. Ni ushuhuda wangu mkuu baada ya Siku hizi Kumi za Maombi. Bwana Asifiwe.

Mada yetu ya Maombi:

Kutafuta Roho wa Mungu Katika Siku Kumi za Maombi mwaka huu 2020, tunakualika kupata uzoefu wa mibaraka iliyoahidiwa ya Roho Mtakatifu. Kabla ya Yesu kurudi mbinguni, alitupatia ahadi hii: “Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi” (Matendo 1:8).

“Ikiwa hii ndiyo njia tunayoweza kutumia kupata nguvu, kwa nini hatuoni njaa na kiu ya zawadi ya Roho? Kwa nini hatuizungumzii, hatuiombei, na hatuhubiri kuhusu zawadi hiyo? Bwana yu tayari zaidi kumtoa Roho Mtakatifu kwa wale wanaomtukimikia kuliko ilivyo kwa wazazi kutoa zawadi nzuri kwa watoto wao. Ili kupata ubatizo wa Roho wa kila siku, kila mtumishi anapaswa kuwasilisha ombi lake kwa Mungu” (Ellen White, The Acts of the Apostles, uk. 50).

Ungana nasi kadri tunapotafuta umwgwaji wa Roho Mtakatifu na kumruhusu Mungu kuzaa Matunda yake ndani ya maisha yetu! Mwongozo unaopendekezwa wakati wa maombi

  1. Jitahidi kufanya maombi yawe mafupi – sentensi moja au mbili kuhusu mada moja. Kisha waachie wengine. Unaweza kuomba mara nyingi kadiri unavyojisikia, kwa namna ile ile unayozungumza na rafiki.

  2. Msiogope kuwa kimya kwani kwa kufanya hivyo mtakuwa mnapata muda wa kumsikiliza Roho Mtakatifu.

  3. Imbeni nyimbo pamoja kadiri Roho Mtakatifu atakavyowaongoza, huo pia ni mbaraka mkubwa. Wala hamhitaji kinanda ili kuwaongoza, imbeni tu bila kinanda, inapendeza

  4. Badala ya kutumia muda wa thamani wa maombi ukizungumza kuhusu mahitaji yako ya kuombea, yaombee tu. Kasha wengine pia wanaweza kuombea mahitaji yako na kudai ahadi kwa ajili ya mahitaji yako. 


Kudai Ahadi: 

Mungu ametupatia ahadi nyingi katika Neno lake. Ni faida kwetu kudai ahadi hizo katika maombi. Maagizo yote ya Mungu na mashauri yake pia ni ahadi. Hawezi kudai jambo fulani kutoka kwetu ambalo hatuwezi kufanya kwa uweza wake.

Tunapoomba, ni rahisi kujielekeza katika mahitaji yetu, changamoto zetu au labda manung’uniko kuhusu hali fulani inayoweza kuwa imetokea. Hili silo kusudi la maombi, kusudi kubwa la maombi ni kuimarisha imani yetu. Ndiyo maana tunahimizwa kudai ahadi ambazo Mungu ametupatia katika maombi yetu. Hamisha macho yako kutoka katika mahitaji yako na changamoto zako na kuyaelekeza kwa Yesu Kristo. Ni kwa kumwangalia yeye ndipo tunapobadilishwa na kuchukua sura yake.

“Kila ahadi katika Neno la Mungu ni kwa ajili yetu. Ni katika maombi pekee ndipo tunapoweza kuwasilisha haja zetu, kwa kuonesha kwenye Neno la Yehova, na kwa imani kudai hizo ahadi. Neno lake linatupatia uhakika kwamba ukiomba kwa imani, utapokea mibaraka yote ya kiroho. Endelea kuomba nawe utapata zaidi ya kile ulichoomba.” (In Heavenly Places, uk. 71).

Ni kwa namna gani unaweza kudai hizo ahadi za Mungu? Kwa mfano, unapoomba kwa ajili ya amani, unaweza kudai Yohana 14:27 na kusema, “Bwana umetuambia katika Maandiko yako kwamba ‘Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.’ Ninakuomba unipatie amani uliyoahidi kutuachia.” Kisha mshukuru Bwana kwamba atakupatia hiyo amani hata kama haujisikii kuwa na amani wakati huo.

Kufunga: 

Tunakuhamasisha kufanya Mfungo wa Danieli katika Siku hizi Kumi. Kuanza mwaka kwa maombi na kufunga ni njia bora ya kuweka wakfu maisha yetu kwa Mungu kwa mwaka unaoanza. Ellen White anatuambia, “Sasa na kuendelea hata mwisho wa wakati watu wa Mungu wanapaswa kuwa na bidii zaidi, kuwa macho zaidi, kutokuamini hekima yao wenyewe, lakini kuamini hekima ya kiongozi wao. Wanapaswa kutenga siku kwa ajili ya kufunga na kuomba. Kujitenga kabisa na chakula kunaweza kusihitajike, lakini wanapaswa kula vyakula rahisi zaidi” (Counsels on Diet and Foods, uk. 188, 189).

Tunafahamu kuhusu Danieli, aliyekula matunda na mboga mboga kwa siku 10. Sisi pia tunakuhamasisha kuwa na mlo rahisi sana katika siku hizi kumi. Mlo rahisi unaoweka kando sukari, vyakula vilivyotengenezwa kiwandani, na soda huweza kutufaidisha kwa ngazi tofauti. Kwanza, kula chakula rahisi humaanisha muda mchache huhitajika kuandaa chakula na muda mwingi kutumika pamoja na Bwana. Pili, chakula chetu kinapokuwa rahisi zaidi, ndivyo inavyokuwa rahisi kwa tumbo kukimeng’enya, na akili zetu zitakua wazi zaidi. Sote tunafahamu kwamba sukari hufunika sehemu inayotawa kuwaza kwetu. Kama tunataka akili zilizo wazi zaidi ili kuisikia sauti ya Mungu, na kama tunataka kuwa karibu zaidi na Mungi, tunahitaji kuhakikisha kwamba chakula chetu hakiturudishi nyuma.

Kufunga si kujitenga tu na chakula. Tunakuhamasisha pia kufunga kutazama televisheni, filamu, michezo ya kompyuta, na hata Facebook na YouTube. Wakati mwingine vitu visivyo vibaya, kama Facebook na YouTube, huweza kutuchukulia muda mwingi sana. Weka kando kila kinachowezekana ili uwe na muda mwingi wa kukaa na Bwana. Kufunga si njia ya haraka ya kupata mibaraka kutoka kwa Mungu. Kufunga ni kujinyenyekeza wenyewe ili kwamba Mungu aweze kufanya kazi ndani yetu na kupitia kwetu. “Kwa baadhi ya mambo kufunga na kuomba hushauriwa na hufaa. Mikononi mwa Mungu, mambo hayo ni njia ya kusafisha moyo na kujenga akili ya usikivu. Tunapata majibu kwa maombi yetu kwa sababu tunanyenyekeza nafsi zetu mbele za Mungu” (Medical Ministry, uk. 283).

Hebu na tujinyenyekeze mbele za Mungu na kumtafuta kwa mioyo yetu yote, akili zetu, na nguvu zetu zote. Hebu na tusogee karibu naye kupitia maombi na kufunga, na atasogea karibu Zaidi nasi.

Roho Mtakatifu:

Hakikisha unamuomba Roho Mtakatifu akuonyeshe unachopaswa kuombea katika maisha ya mtu au katika hali fulani. Biblia inatuambia kwamba hatufahamu namna ya kuomba na kwamba Roho Mtakatifu ndiye anayetuombea.

“Hatupaswi kuomba tu kwa jina la Kristo, lakini kwa msukumo wa Roho Mtakatifu. Hii huelezea kinachomaanishwa inaposemwa kwamba Roho “hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa.” (Warumi 8:26). Ombi kama hilo Mungu hufurahia kulijibu. Tunapoomba kwa dhati na kwa nguvu tunaomba kwa jina la Kristo, katika nguvu hiyo kuna ahadi kutoka kwa Mungu kwamba anakaribia kujibu maombi yetu ‘zaidi ya tuyaombayo au tuyawazayo’ (Waefeso 3:20” (Christ Object Lessons, uk. 147).

Imani:

Tunasoma katika Roho ya Unabii kwamba “maombi na imani vitafanya kile ambacho hakuna nguvu duniani itaweza kufanya” (The Ministry of Healing, uk. 509).Tunahamasishwa pia kuomba na kuwa na imani kwamba Mungu amesikia na atajibu maombi yetu.

“Kristo anasema, ‘Ombeni nanyi mtapewa.’ Katika maneno haya, Kristo anatupatia mwongozo wa namna tunavyopaswa kuomba. Tunapaswa kuja kwa Baba yetu wa mbinguni tukiwa kama watoto, tukimuomba zawadi ya Roho Mtakatifu. Yesu anasema tena, ‘Muombapo, aminini kwamba mmepokea myaombayo, nayo yatakuwa yenu.’ Unapaswa kuja kwa Baba ukitubu na kuungama dhambi zako, ukisafisha nafsi na kila dhambi na uchafu, na ni heshima kwako kuthibitisha ahadi za Bwana… Tunapaswa kuamini neno la Mungu, kwani kwa kujijenga juu ya imani ya kitakatifu zaidi tunapata jaribio la tabia. Mungu anathibitishwa kwako kupitia Neno lake. Haupaswi kusubiri kuwa na hisia nzuri za ajabu kabla ya kuamini kwamba Mungu amekusikia; hisia hazipaswi kuwa kigezo chako, kwani hisia hubadilika kama mawingu… Kadiri tunapokuwa duniani, tunaweza kupata nguvu kutoka mbinguni… kwani nimemjaribu Mungu mara elfu. Nitatembea kwa imani, sitaacha kumheshimu Mwokozi wangu kwa kukosa imani” (Review and Herald, Oct. 11, 1892, aya ya 1, 3, 6).

Pia tunaambiwa kwamba “ahadi yo yote aliyoahidi, tunaweza kuiomba; kasha tunapaswa kuamini kwamba tumepokea, na kurudisha shukrani kwa Mungu kwamba tumepokea” (Education, uk. 258). Hivyo jenga tabia ya kumshukuru Mungu kabla kwa imani kwa kile atakachoenda kutenda na namna atakavyoenda kujibu maombi yako.

Ombea watu Saba:

Tunakuhamasisha kuombea kwa namna ya pekee watu saba katika siku hizi kumi ambao ungependa kuwaona wakipata “maisha yaliyojaa zaidi.” Wanaweza kuwa ndugu, marafiki, wafanyakazi wenzako, majirani, au hata watu unaowafahamu tu. Tenga muda na muulize Mungu angependa umuombee nani. Muombe pia akupatie mzigo halisi wa watu hawa. Andika majina yao kwenye karatasi na uitunze sehemu salama, kama kwenye Biblia yako. Kuna jambo lenye nguvu katika kuyaandika majina hayo, na utashangazwa namna Mungu anavyofanya kazi katika kujibu maombi yako! 

Changamoto za Kuwafikia watu walio nje katika Siku Kumi za Maombi 

Kila mmoja anaweza kufanya kitu ili kuharakisha ujio wa Yesu kupitia Kuhusishwa kwa Washiriki Wote (TMI)

“Kwa maana nalikuwa na njaa, mkanipa chakula; nalikuwa na kiu, mkaninywesha; nalikuwa mgeni, mkanikaribisha; nalikuwa uchi, mkanivika nalikuwa mgonjwa, mkaja kunitazama; nalikuwa kifungoni, mkanijia” (Mathayo 25:35, 36).

Katika kitabu cha Huduma ya Uponyaji (The Ministry of Healing) tunasoma kuwa, “Tunapaswa kuishi maisha yenye sura mbili – maisha ya mawazo na matendo, na maisha ya maombi ya kimya na kazi inayofanywa kwa juhudi” (uk. 512). Ni faida kwetu kuwaonyesha wengine upendo wa Yesu. Tumepokea vitu vingi sana kutoka kwa Mwokozi wetu; hebu tusivitunze kwa ajili yetu wenyewe. Hebu tuwashirikishe watu wengine upendo wake.

Tunakuhimiza wewe na kanisa lako kumuuliza Mungu katika maombi namna unavyoweza kuwafikia wengine katika Siku hizi Kumi za Maombi. Chagua shughuli moja au shughuli kadhaa, na uchague siku, ili uwe mikono na miguu ya Yesu. Unapokuwa ukifanya kazi ya kupanga kila kitu, epuka kuruhusu shughuli hizi kukufanya ushindwe kuomba. “Unapoweka jitihada kwa ajili ya wengine, anza kwa maombi mengi ya siri; kwani ili kuelewa sayansi ya kuokoa roho unahitaji hekima kubwa. Kabla ya kuwasiliana na watu, wasiliana na Kristo. Pata maandalizi ya kuhudumia kwa watu kutoka katika kiti cha enzi cha neema ya kimbingu.” (Maombi, uk. 313).

Katika vitendea kazi mtandaoni, utapata ukurasa maalumu wenye mapendekezo  ya kuifikia jamii yako kwa ajili ya Yesu. Pia kurasa za wazo la kila siku zinapatikana moja kwa moja kwa kompyuta au simu kwa tovuti ya www.tendaysofprayer.org 

USIKU WA MAOMBI:

Usiku wa Mkesha wa Hiari katika Siku 10 za Maombi

Fikiria kuandaa huduma ya maombi ya usiku kama sehemu ya Siku Kumi za Maombi. Kwa mfano, unaweza kuanza saa 12 jioni na kumaliza saa 12 asubuhi.

Kwa nini kuwa na Usiku wa Maombi?

Hakuna chochote “kitakatifu” katika kukesha na kuomba usiku kucha au sehemu ya usiku. Hata hivyo, usiku unaweza kuwa wakati wa pekee ambao watu hawana mambo mengi au haraka. Tunaamini kwamba lengo lako halipaswi kuwa kukaa usiku kucha, bali ni kuomba sana kadiri inavyohitajika hadi utakapokuwa umeombea vitu vyote unavyohisi kwamba Mungu anataka uombee.

Tunapendekeza kwamba baadhi ya watu waongoze usiku huo. Hakikisha kunakuwa na mapumziko. Kama kiongozi, unaweza kuona hali ilivyo na kufahamu wakati mapumziko yanapohitajika na wakati utakapoona unafaa kuhamia katika kipengele kinachofuata cha maombi. Unaweza pia kuingiza usomaji wa vifungu vya Biblia katika muda wako wa maombi. Unaweza kufanya mambo yote yaliyopendekezwa au baadhi yake, inategemea kile kilicho bora kwa kikundi chako. Kuwa huru kubadilisha mtiririko kadiri utakavyoona inafaa.

Mfano wa Ratiba kwa Saa moja ya kwanza

  1. 11:45 – Nyimbo za sifa

  2. 12:00 – Ukaribisho na utangulizi. Maelezo yawe mafupi lakini ya kirafiki.

  3. 12:05 – Maombi ya sifa kwa Mungu kwa vile alivyo (kusifu tabia yake).

  4. 12:10 – Kudai ahadi za Biblia (tazama “Ahadi za Kudai katika Maombi” katika vitendea kazi mtandaoni). 

  5. 12:15 – Maombi ya kuungama (Muda wa maombi ya kimya).

  6. 12:20 – Maombi ya mibaraka inayohitajika (kusihi)

  7. 12:25 – Maombi ya kimya.

  8. 12:30 – Maombi ya kuingilia kati kwa ajili ya wokovu wa roho katika jamii yako na eneo la kanisa.

  9. 12:35 – Maombi yanayoakisi katika maisha, kifo, na ufufuo wa Yesu.

  10. 12:40 – Kushukuru kwa kile Mungu alichotenda.

  11. 12:45 – Nyimbo za maombi na/au kusoma maneno kutoka kwenye kitabu cha nyimbo.

  12. 12:50 – Maombi ya kuomba uwepo na nguvu wa Roho Mtakatifu.

  13. 12:55 – Maombi zaidi ya sifa na kushukuru. 

Unaweza kuhitaji kurudia mfumo huo huo kwa kila saa usiku huo kwa sababu watu watakuwa wakija na kuondoka. Katika kipindi cha kusihi unaweza tamani kuombea “Mahitaji ya kuombea ya Kanisa la Kiulimwengu” (yamejumuishwa mwisho wa kipengele hiki). Hakikisha unatenga muda pia kwa ajili ya mahitaji ya kanisa mahalia na mambo ya kuombea.

Mguso mwingine ni kuwa na washiriki wenye karama kuwasilisha nyimbo au mashairi/maombi yaliyojengwa katika maombi. Unaweza kuweka pia dakika 3 hadi 5 za shuhuda.


Mahitaji ya Kuombea ya Kanisa la Kiulimwengu

  1. Tunaomba kwa ajili ya washiriki wa Kiadventista wanaopitia mateso au vifungo kwa sababu ya Imani yao.

  2. Tunaomba kwa ajili ya uamsho wa kiroho kati ya vijana Waadventista wa Sabato wanaohudhuria vyuo vya kiserikali ulimwenguni. Hebu na wawe mabalozi mashuhuri wa Kristo.

  3. Tunaomba kwa ajili ya asilimia 69 ya idadi ya watu duniani ambao hawajapokea habari zisizo na mawaa za Yesu.

  4. Tunaomba kwa ajili ya watu milioni 62 katika miji 28 ambayo haijafikiwa Zaidi katika unioni ya zamani ya Kirusi (Divisheni ya Ulaya na Asia).

  5. Tunaomba kwamba Mungu ainue wamisionari wenye hekima walio tayari kufanya kazi kati ya makundi 746 ya watu katika nchi 20 za Mashariki ya Kati.

  6. Tunaomba kwa ajili ya Harakati 1,000 za Kimisionari katika Divisheni ya Kaskazini mwa Asia-Pasifiki na Divisheni ya Kusini mwa Asia-Pasifiki. Kadri vijana hawa wanapohuduma katika nchi kama Taiwan, China, Urusi, na Burma, hebu na wabatizwe kwa Roho Mtakatifu na kutiwa nguvu kutenda kazi ya Mungu.

  7. Tunaomba kwa ajili ya mafuriko makuu ya Waadventista watakaomtumikia Mungu kwa kuwapenda wengine na kushiriki pamoja na watu kutoka katika tamaduni na dini nyingine.

  8. Tafadhali inua wanafuzi Wawaldensia wa siku za sasa, walio tayari kukutumikia katika maeneo magumu.

  9. Tunaomba kwa ajili ya watu milioni 202 katika miji 41 ambayo haijafikiwa Zaidi katika Divisheni ya Asia-Pasifiki waweze kumfahamu Yesu.

  10. Tunaomba kwa ajili ya Idara ya Shule ya Sabato na Idara ya Huduma binafsi ya kila kanisa mahalia kadri wanavyotafuta mpango wa Mungu na kuzifikia jamii zao kwa huduma za upendo, Kujifunza Biblia, na ushuhudiaji binafsi.

  11. Tunaomba kwa ajili ya shirika la ADRA (Adventist Development and Relief Agency) kadri wanavyofikia mahitaji mahususi duniani. 

  12. Tunaomba kwa ajili ya watu milioni 16 katika miji 6 ambayo haijafikiwa Zaidi ya Divisheni ya Kusini mwa Pasifiki. Tunaomba kwa ajili ya ubatizo wa kila siku wa Roho Mtakatifu kwa washiriki kadri wanavyowafikia kwa upendo wale ambao hawajafikiwa bado.

  13. Tunaomba kwamba Roho Mtakatifu atusaidia kufahamu namna ya kuwafikia watu milioni 406 katika miji 105 isiyofikiwa Zaidi ya Divisheni ya Kaskazini mwa Asia-Pasifiki.

  14. Bariki Huduma za Chaplensia za Kiadventista kadri zinavyosimamia chaplensia na washiriki wenye shauku katika kuhudumia wale walio katika magereza.

  15. Bwana, tunakumbuka waalimu wetu wa Shule ya Sabato. Tafadhali wasaidie kufahamu kazi yao ilivyo ya muhimu kwa watoto wetu.

  16. Bwana, tunatafuta uongozi wako katika Vituo vingi vya Vivutio, programu za afya na familia, na klabu za Watafuta Njia duniani.

  17. Tunaomba kwamba utusaidie kuwapenda na kuwatunza waumini wapya.

  18. Bwana, tafadhali tuonyeshe namna ya kutuma machapisho yaliyojazwa kweli (yaliyochapishwa na kielektroniki) katika jamii zetu. Tunaomba kwamba watu wayasome na Roho Mtakatifu awaonyeshe kweli ya Biblia.

  19. Bwana, tafadhali tunaomba ulinzi wako juu ya wamisionari wanaofanya kazi katika maeneo magumu.

  20. Tafadhali inua wainjilisti wa vitabu, wanafunzi wa kujitolea, waandishi, waliobobea katika masuala ya vyombo vya habari, na wategemezaji wa kifedha ili kusambaza maneno ya tumaini na uzima.

  21. Tunaomba kwa ajili ya shule 8,208 za Kiadventista zenye wanafunzi karibia milioni 2. Hebu shule hizi zifundishe daima kweli za Biblia na kuwaongoza vijana katika utume na huduma.

  22. Bwana, tupatie hekima ya kufikia tamaduni zisizo na dini ambazo hazina shauku katika dini. Mruhusu Roho wako Mtakatifu avunje kuta zinazoizunguka mioyo isiyokuwa na dini.

  23. Tunaomba kwa ajili ya makundi ya watu katika Asia ambayo hayana historia ya Ukristo. Tupatie hekima ya kuyafikia mahitaji yao.

  24. Bwana, tafadhali tia msukumo kwa Waadventista wa Sabato ulimwenguni wa kuomba kuliko ilivyowahi kutokea hapo kabla. Tusiadie kutsihi pamoja kwa ajili ya mvua ya masika ya Roho Mtakatifu. Tunaomba ukamilisho ulioahidiwa wa Yoeli 2, Hosea 6, na Matendo 2.

  25. Tunaomba kwa ajili ya makundi 541 ya watu katika nchi 18 za Divisheni ya Kusini mwa Afrika-Bahari ya Hindi. Tadhali wangoze katika kweli ya Kibiblia.  

  26. Tuonyeshe namna ya kufikia mahitaji ya kimwili na kiroho ya wakimbizi. Hebu kanisa letu na lifahamike kwa upendo wetu kwa watu wote, bila kujali walivyo au wanapotoka.

  27. Tunaomba kwa uaminifu na ukamilifu tutangaze Ujumbe wa Malaika Watatu wa Ufunuo 14. Tuweze kujenga mafundisho yetu yote katikaupendo na haki ya Kristo.

  28. Tunaomba uwainue wamisionari wa mijini ili kupanda makanisa kwa ajili ya makundi 806 ya watu katika nchi 20 za Divisheni ya Inter-Europe.

  29. Tafadhali inua jeshi la watenda kazi ili kusimamisha makanisa kwa ajili ya makundi 948 ya watu katika Divisheni ya Inter-America

  30. Tafadhali tufundishe namna ya kutangaza misingi yetu ya Imani kwa usawa, ubunifu, na uthibitisho wa kibliblia. Upendo wa Kristo na uwe kiini cha kila kitu tunachokiamini.

  31. Tunakuomba uandae vijana wa kuanzisha makanisa kwa ajili ya makundi 789 ya watu katika nchi 9 za Divisheni ya Kaskazini wa Amerika.

  32. Tunakuomba uandae watakaojitolea kuhudumu katika makundi 70 ya watu katika Fildi ya Israeli.

  33. Tunakuomba uinue wamisionari wa kitabibu ili kuanzisha makanisa kati ya makundi 830 ya watu katika nchi 11 za Divisheni ya Afrika Mashariki na Kati.

  34. Tunakuomba uinue mashujaa wa maombi ili kuomba kwa kuingilia kati kwa ajili ya makundi 2,568 ya watu katika nchi 4 za Divisheni ya Kusini mwa Asia. Tunakumbuka hasa kituo cha televisheni cha Hope Tv India na Shule ya Msaada kwa ajili ya vipofu.

  35. Tunaomba kwamba utende kama ulivyoahidi katika Zaburi 32:8, kwa kutuongoza na kutuelekeza kadri tunavyofanya Changamoto ya Kuwafikia Watu katika Siku Kumi za Maombi.

  36. Tafadhali ruhusu familia zetu kudhihirisha upendo wako katika nyumba zetu na jamii zetu. Tunakuomba ulete uelewano katika familia, ponya mahusiano yaliyovunjika, linda wenye hatari ya kukumbwa na unyanyasaji, na dhihirisha nguvu yako ya kutakaso katika hali zinazoonekana kutokuwa na tumaini.

  37. Tunaomba washiriki wa kanisa letu, wachungaji, na viongozi duniani wajilishe kwa Neno la Mungu kila siku. Tuweze pia kukutafuta kila siku katika maombi binafsi. Tukumbushe kwamba bila wewe, hatuwezi fanya lo lote.

  38. Tunakuomba uinue wauguzi na madaktari ili kuanzisha makanisa kati ya makundi 1,978 ya watu katika nchi 22 za Divisheni ya Afrika Magharibi na Kati.

  39. Tunaomba kwa ajili ya watu milioni 49 katika miji 19 ambayo haijafikiwa Zaidi ya Divisheni ya Tran-Europe. 

  40. Tunaomba kwa ajili ya watoto wetu. Tafadhali watie nguvu ili wasimame imara kwa ajili yako wanapokutana na vikwazo na misukumo. Wasaidie kufanya chaguzi sahihi na kusimamia ukweli.

  41. Tufundishe kufuata mfano wa Kristo wa kutojifikiria kwa kufikia mahitaji ya kila siku a watu walio karibu nasi. Tuandae kutumika kama wamisionari wa kitabibu, wanaojitolea kwa ajili ya jamii, na marafiki kwa wahitaji.

  42. Bwana, tunaomba uamsho mkuu wa utakatifu usafishe kanisa lako katika siku za mwisho. Tunaomba tusimamie ukweli hata mbingu zikianguka.

  43. Tafadhali bariki mamia ya maelfu ya shughuli za kuwafikia watu ulimwenguni kwa mwaka 2020. Tunaomba hasa kwa ajili ya efoti za uinjilisti za Uhusishwaji wa Kila Mshiriki huko Papua New Guinea mwezi Mei 2020.

  44. Tunaombea viongozi wa vijana ulimwenguni walio waaminifu katika kuhamisha hazina yetu katika kizazi kinachofuata: utambulisho katika Kristo, utume kama Waadventista wa Sabato, na uongozi katika kanisa mahalia.

  45. Tunaombea vijana wanaoishi kwa hatari kwa ajili ya Bwana kupitia Harakati ya OYiM (One Year in Mission) na harakati ya Mission Caleb.

  46. Tunaomba kwa ajili ya ubatizo wa Roho Mtakatifu kwa vijana wetu na viongozi vijana kama ilivyoahidiwa katika Matendo 1:8. Na tunaomba hasa kwa ajili ya mibaraka ya Mungu kwa vijana waliohusika katika shughuli ya “Give Him 20” (Mpatie 20) na mipango mingine ya maombi.

  47. Bwana, tafadhali tuonyeshe mkakati uliokubaliwa na Mungu wa kufikia Yeriko a dunia kwa Ujumbe wa Malaika Watatu na kuongoza akina Rahabu katika kila mji kwenye wokovu katika Kristo.

  48. Tunakuomba uinue viongozi wapya walio vijana na bariki semina za Uongozi wa Vijana Wakubwa (Senior Youth Leadership).

  49. Bwana, tafadhali saidia vijana wetu wasihubiri tu lakini pia waishi hubiri hilo. Tunamba Mungu abariki jitihada za Siku ya Vijana Ulimwenguni (Global Youth Day) na mikakati 100,000 ya uhusishwaji wa kila mshiriki (TMI)

  50. Bwana, tafadhali ongoza maamuzi ya kanisa katika Mkutano wa Uchaguzi wa Konferensi Kuu 2020 (Juni 25 – Julai 4). Tunaomba wajumbe, viongozi, na wageni wajazwe na roho ya uamsho na upendo.

  51. Tafadhali bariki siku 100 za Maombi (Machi 27 – Julai 4) kuelekea kwenye Mkutano wa Uchaguzi wa Konferensi Kuu. Mwaga Roho Wako Mtakatifu kadri tunavyoomba hekima na ujio wako ulio karibu.



Ahadi za Kudai kwenye Maombi


Mungu ametupatia ahadi nyingi sana katika Neno lake. Ni faida kwetu kuzidai ahadi hizo katika maombi haya. Amri zake zote na mashauri ni ahadi. Kamwe hawezi kututaka tufanye kitu ambacho hatuwezi kufanya kwa nguvu zake.

Ni rahisi sana kuweka umakini wetu katika mahitaji yetu, magumu yetu, changamoto zetu – na kuomboleza na kulalamika kuhusu hali zetu tunapoomba. Hili si lengo la maombi. Tunategemea kwamba maombi yataimarisha imani zetu. Ndiyo sababu tunakuhamasisha kudai ahadi za Mungu katika maombi yako. Acha kujitazama na kutazama madhaifu yako, bali mtazame Yesu. Kwa kumtazama, tunabadilishwa na kufanana nae.

“Kila ahadi katika Neno la Mungu ni kwa ajili yetu. Katika maombi yako, wasilisha neno lililoahidiwa la Yehova na kwa imani udai ahadi zake. Neno lake linatuhakikishia kwamba ukiomba kwa imani, utapokea mibaraka ya kiroho. Endelea kuomba, na utapokea zaidi ya yale uyaombayo au hata uyawazayo” (In Heavenly Places, uk. 71).

Unawezaje kudai ahadi zake? Kwa mfano, unapoombea amani, unaweza kudai Yohana 14:27 na kusema, “Bwana, umetuambia katika Neno lako kuwa, ‘Amani nawaachieni; amani yangu nawapa; niwapavyo mimi sivyo kama ulimwengu utoavyo. Msifadhaike mioyoni mwenu, wala msiwe na woga.’ Nipatie amani uliyoahidi kutuachia.” Mshukuru Bwana kwamba anakupatia amani, hata kama hutahisi kuipata wakati huo huo.


Ahadi za Roho Mtakatifu


  1. “Mwombeni Bwana mvua wakati wa masika, naam, Bwana afanyaye umeme, naye atawapa manyunyu ya mvua, kila mtu atapewa nyasi kondeni.” Zakaria 10:1
  2. “Basi, ikiwa ninyi mlio waovu mnajua kuwapa watoto wenu vipawa vyema, je! Baba aliye mbinguni hatazidi sana kuwapa Roho Mtakatifu hao wamwombao?” Luka 11:13
  3. “Lakini huyo Msaidizi, huyo Roho Mtakatifu, ambaye Baba atampeleka kwa jina langu, atawafundisha yote, na kuwakumbusha yote niliyowaambia… Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu.” Yohana 14:26; 16:8
  4. “Amin, amin, nawaambieni, Yeye aniaminiye mimi, kazi nizifanyazo mimi, yeye naye atazifanya; naam, na kubwa kuliko hizo atafanya, kwa kuwa mimi naenda kwa Baba. Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.” Yohana 14:12 – 14 
  5. “Akajibu akaniambia, akisema, Hili ndilo neno la Bwana kwa Zerubabeli, kusema, Si kwa uwezo, wala si kwa nguvu, bali ni kwa roho yangu, asema Bwana wa majeshi.” Zakaria 4:6



Ahadi kwamba Mungu Hujibu Maombi: 


  1. “Ninyi mkikaa ndani yangu, na maneno yangu yakikaa ndani yenu, ombeni mtakalo lote nanyi mtatendewa.” Yohana 15:7
  2. “Basi na tukikaribie kiti cha neema kwa ujasiri, ili tupewe rehema, na kupata neema ya kutusaidia wakati wa mahitaji.” Waebrania 4:16
  3. “Kwa sababu hiyo nawaambia, Yo yote myaombayo mkisali, aminini ya kwamba mnayapokea, nayo yatakuwa yenu.” Marko 11:24
  4. “Ukaniite siku ya mateso; Nitakuokoa, na wewe utanitukuza.” Zaburi 50:15
  5. “Tena nawaambia, ya kwamba wawili wenu watakapopatana duniani katika jambo lo lote watakaloliomba, watafanyiwa na Baba yangu aliye mbinguni.” Mathayo 18:19
  6. “Na yo yote mtakayoyaomba katika sala mkiamini, mtapokea.” Mathayo 21:22 
  7. “Nanyi mkiomba lo lote kwa jina langu, hilo nitalifanya, ili Baba atukuzwe ndani ya Mwana. Mkiniomba neno lo lote kwa jina langu, nitalifanya.” Yohana 14:13, 14
  8. “Tena siku ile hamtaniuliza neno lo lote. Amin, amin, nawaambia, Mkimwomba Baba neno lo lote atawapa kwa jina langu. Hata sasa hamkuomba neno kwa jina langu; ombeni, nanyi mtapata; furaha yenu iwe timilifu.” Yohana 16:23, 24
  9. “Na huu ndio ujasiri tulio nao kwake, ya kuwa, tukiomba kitu sawasawa na mapenzi yake, atusikia. Na kama tukijua kwamba atusikia, tuombacho chote, twajua kwamba tunazo zile haja tulizomwomba.” 1 Yohana 5:14, 15


Ahadi kuhusu Nguvu ya Mungu

  1. “Kuna neno gani lililo gumu la kumshinda Bwana? Kwa muhula wake nitakurudia, wakati huu huu mwakani, na Sara atapata mwana wa kiume.” Mwanzo 18:14
  2. “Bwana atawapigania ninyi, nanyi mtanyamaza kimya.” Kutoka 14:14
  3. “Yesu akawakazia macho, akasema, Kwa wanadamu haiwezekani, bali kwa Mungu sivyo; maana yote yawezekana kwa Mungu.” Marko 10:27
  4. “Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya.” 1 Wathesalonike 5:24 
  5. “Najua ya kuwa waweza kufanya mambo yote, Na ya kuwa makusudi yako hayawezi kuzuilika.” Ayubu 42:2
  6. “Basi, tuseme nini juu ya hayo? Mungu akiwapo upande wetu, ni nani aliye juu yetu? Yeye asiyemwachilia Mwana wake mwenyewe, bali alimtoa kwa ajili yetu sisi sote, atakosaje kutukirimia na mambo yote pamoja naye?” Warumi 8:31, 32
  7. “Mungu si mtu, aseme uongo; Wala si mwanadamu, ajute; Iwapo amesema, hatalitenda? Iwapo amenena, hatalifikiliza?” Hesabu 23:19
  8. “Je! Wewe hukujua? Hukusikia? Yeye Mungu wa milele, Bwana, Muumba miisho ya dunia, hazimii, wala hachoki; akili zake hazichunguziki. Huwapa nguvu wazimiao, humwongezea nguvu yeye asiyekuwa na uwezo. Hata vijana watazimia na kuchoka, na wanaume vijana wataanguka; bali wao wamngojeao Bwana watapata nguvu mpya; watapanda juu kwa mbawa kama tai; watapiga mbio, wala hawatachoka; watakwenda kwa miguu, wala hawatazimia.” Isaya 40:28 – 31 


Ahadi za Ulinzi wa Mungu

  1. “Je! Si mimi niliyekuamuru? Uwe hodari na moyo wa ushujaa; usiogope wala usifadhaike; kwa kuwa Bwana, Mungu wako, yu pamoja nawe kila uendako.” Yoshua 1:9 “Na tazama, mimi nipo pamoja nawe, nitakulinda kila uendako, nami nitakuleta tena mpaka nchi hii, kwa maana sitakuacha, hata nitakapokufanyia hayo niliyokuambia.” Mwanzo 28:15
  2. “Tazama, mimi namtuma malaika aende mbele yako, ili akulinde njiani na kukupeleka mpaka mahali pale nilipokutengezea.” Kutoka 23:20
  3. “Lakini huko, kama mkimtafuta Bwana, Mungu wako, utampata, ukimtafuta kwa moyo wako wote, na roho yako yote.” Torati 4:29
  4. “Niite, nami nitakuitikia, nami nitakuonyesha mambo makubwa, magumu usiyoyajua.” Yeremia 33:3
  5. “Kila bonde litainuliwa, Na kila mlima na kilima kitashushwa; Palipopotoka patakuwa pamenyoka, Na palipoparuza patasawazishwa; Na utukufu wa Bwana utafunuliwa, Na wote wenye mwili watauona pamoja; Kwa kuwa kinywa cha Bwana kimenena haya.” Isaya 40:4, 5
  6. “Nitakufundisha na kukuonyesha njia utakayoiendea; Nitakushauri, jicho langu likikutazama.” Zaburi 32:8
  7. “Naye Bwana, yeye ndiye atakayekutangulia, atakuwa pamoja nawe, hatakupungukia wala kukuacha; usiogope wala usifadhaike.” Torati 31:8
  8. “Ni nani amchaye Bwana? Atamfundisha katika njia anayoichagua.” Zaburi 25:12
  9. “Mtumaini Bwana kwa moyo wako wote, Wala usizitegemee akili zako mwenyewe; Katika njia zako zote mkiri yeye, Naye atayanyosha mapito yako.” Mithali 3:5, 6
  10. “Na kama ukimkunjulia mtu mwenye njaa nafsi yako, na kuishibisha nafsi iliyoteswa; ndipo nuru yako itakapopambazuka gizani; na kiwi chako kitakuwa kama adhuhuri. Naye Bwana atakuongoza daima, ataishibisha nafsi yako mahali pasipokuwa na maji, na kuitia nguvu mifupa yako; nawe utakuwa kama bustani iliyotiwa maji, na kama chemchemi ambayo maji yake hayapungui.” Isaya 58:10, 11
  11. “Nao watatoka nje na kuitazama mizoga ya watu walioniasi; maana funza wao hatakufa, wala moto wao hautazimika nao watakuwa chukizo machoni pa wote wenye mwili.” Isaya 65:24


Ahadi za Moyo Uliobadilishwa

  1. “Nami nitawapa moyo, wanijue ya kuwa mimi ni Bwana; nao watakuwa watu wangu, nami nitakuwa Mungu wao; kwa maana watanirudia kwa moyo wao wote.” Yeremia 24:7
  2. “Bwana, Mungu wako, atautahiri moyo wako, na moyo wa uzao wako, ili umpende Bwana, Mungu wako, kwa moyo wako wote, na kwa roho yako yote, upate kuwa hai.” Torati 30:6
  3. “Nami nitawapa ninyi moyo mpya, nami nitatia roho mpya ndani yenu, nami nitatoa moyo wa jiwe uliomo ndani ya mwili wenu, nami nitawapa moyo wa nyama.” Ezekieli 36:26
  4. “Nami niliaminilo ndilo hili, ya kwamba yeye aliyeanza kazi njema mioyoni mwenu ataimaliza hata siku ya Kristo Yesu;” Wafilipi 1:6
  5. “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya.” 1 Wakorintho 5:17
  6. “Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.” Wagalatia 2:20
  7. “Mungu wa amani mwenyewe awatakase kabisa; nanyi nafsi zenu na roho zenu na miili yenu mhifadhiwe mwe kamili, bila lawama, wakati wa kuja kwake Bwana wetu Yesu Kristo. Yeye ni mwaminifu ambaye awaita, naye atafanya.” 1 Wathesalonike 5:23, 24


Ahadi za Msamaha 

  1. “Ikiwa watu wangu, walioitwa kwa jina langu, watajinyenyekesha, na kuomba, na kunitafuta uso, na kuziacha njia zao mbaya; basi, nitasikia toka mbinguni, na kuwasamehe dhambi yao, na kuiponya nchi yao.” 1 Nyakati 7:14
  2. “Kwa maana Wewe, Bwana, U mwema, Umekuwa tayari kusamehe, Na mwingi wa fadhili, Kwa watu wote wakuitao.” Zaburi 86:5
  3. “Nanyi, kila msimamapo na kusali, sameheni, mkiwa na neno juu ya mtu; ili na Baba yenu aliye mbinguni awasamehe na ninyi makosa yenu.” Marko 11:25
  4. “Tena iweni wafadhili ninyi kwa ninyi, wenye huruma, mkasameheane kama na Mungu katika Kristo alivyowasamehe ninyi.” Waefeso 4:32
  5. “Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.” 1 Yohana 1:9
  6. “Haya, njoni, tusemezane, asema Bwana. Dhambi zenu zijapokuwa nyekundu sana, zitakuwa nyeupe kama theluji; zijapokuwa nyekundu kama bendera, zitakuwa kama sufu.” Isaya 1:8
  7. “Mimi, naam, mimi, ndimi niyafutaye makosa yako kwa ajili yangu mwenyewe, wala sitazikumbuka dhambi zako.” Isaya 43:25
  8. “Wala hawatamfundisha kila mtu jirani yake, na kila mtu ndugu yake, wakisema, Mjue Bwana; kwa maana watanijua wote, tangu mtu aliye mdogo miongoni mwao hata aliye mkubwa miongoni mwao, asema Bwana; maana nitausamehe uovu wao, wala dhambi yao sitaikumbuka tena.” Yeremia 31:34
  9. “Katika yeye huyo, kwa damu yake, tunao ukombozi wetu, masamaha ya dhambi, sawasawa na wingi wa neema yake.” Waefeso 1:7



Ahadi za Ushidi Dhidi ya Dhambi


  1. “Kwa maana kila kitu kilichozaliwa na Mungu huushinda ulimwengu; na huku ndiko kushinda kuushindako ulimwengu, hiyo imani yetu.” 1 Yohana 5:4 “Lakini katika mambo hayo yote tunashinda, na zaidi ya kushinda, kwa yeye aliyetupenda.” Warumi 8:37
  2. “Lakini Mungu na ashukuriwe atupaye kushinda kwa Bwana wetu Yesu Kristo.” 1 Wakorintho 15:57
  3. “Tazameni, Bwana Mungu atakuja kama shujaa, Na mkono wake ndio utakaomtawalia; Tazameni, thawabu yake i pamoja naye, Na ijara yake i mbele zake.” Isaya 40:10
  4. “Zaidi ya yote mkiitwaa ngao ya imani, ambayo kwa hiyo mtaweza kuizima mishale yote yenye moto ya yule mwovu.” Waefeso 6:16
  5. “Nimesulibiwa pamoja na Kristo; lakini ni hai; wala si mimi tena, bali Kristo yu hai ndani yangu; na uhai nilio nao sasa katika mwili, ninao katika imani ya Mwana wa Mungu, ambaye alinipenda, akajitoa nafsi yake kwa ajili yangu.” Wagalatia 2:20
  6. “Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.” Wafilipi 2:13
  7. “Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.” Wagalatia 5:16
  8. “Naye Mungu wa amani atamseta Shetani chini ya miguu yenu upesi. Neema ya Bwana wetu Yesu Kristo na iwe pamoja nanyi. Amina.” Warumi 16:20
  9. “Wala msiifuatishe namna ya dunia hii; bali mgeuzwe kwa kufanywa upya nia zenu, mpate kujua hakika mapenzi ya Mungu yaliyo mema, ya kumpendeza, na ukamilifu.” Warumi 12:2
  10. “Akafanya kikoto cha kambaa, akawatoa wote katika hekalu, na kondoo na ng'ombe; akamwaga fedha za wenye kuvunja fedha, akazipindua meza zao.” Yohana 2:15



Ahadi za Uponyaji


  1. “Akawaambia, Kwamba utaisikiza kwa bidii sauti ya Bwana, Mungu wako, na kuyafanya yaliyoelekea mbele zake, na kutega masikio usikie maagizo yake, na kuzishika amri zake, mimi sitatia juu yako maradhi yo yote niliyowatia Wamisri; kwa kuwa Mimi ndimi Bwana nikuponyaye.” Kutoka 15:20
  2. “Makomeo yako yatakuwa ya chuma na shaba; Na kadiri ya siku zako ndivyo zitakavyokuwa nguvu zako.” Torati 33:25
  3. “Ee nafsi yangu, umhimidi Bwana, Wala usizisahau fadhili zake zote. Akusamehe maovu yako yote, Akuponya magonjwa yako yote, Aukomboa uhai wako na kaburi, Akutia taji ya fadhili na rehema, Aushibisha mema uzee wako, Ujana wako ukarejezwa kama tai.” Zaburi 103:2 – 5
  4. “Usiwe mwenye hekima machoni pako; Mche Bwana, ukajiepushe na uovu. Itakuwa afya mwilini pako, Na mafuta mifupani mwako.” Mithali 3:7, 8
  5. “Alidharauliwa na kukataliwa na watu; Mtu wa huzuni nyingi, ajuaye sikitiko; Na kama mtu ambaye watu humficha nyuso zao, Alidharauliwa wala hatukumhesabu kuwa kitu. Hakika ameyachukua masikitiko yetu, Amejitwika huzuni zetu; Lakini tulimdhania ya kuwa amepigwa, Amepigwa na Mungu, na kuteswa. Bali alijeruhiwa kwa makosa yetu, Alichubuliwa kwa maovu yetu; Adhabu ya amani yetu ilikuwa juu yake, Na kwa kupigwa kwake sisi tumepona.” Isaya 53:3-5
  6. “Uniponye, Ee Bwana, nami nitaponyeka; uniokoe, nami nitaokoka; kwa maana wewe ndiwe uliye sifa zangu.” Yeremia 17:14
  7. “Maana nitakurudishia afya, nami nitakuponya jeraha zako, asema Bwana, kwa sababu wamekuita, mwenye kutupwa, wakisema, Ni Sayuni, ambao hapana mtu autakaye.” Yeremia 30:17
  8. “Tazama, nitauletea afya na kupona, nami nitawaponya; nami nitawafunulia wingi wa amani na kweli.” Yeremia 33:6
  9. “Lakini kwenu ninyi mnaolicha jina langu, jua la haki litawazukia, lenye kuponya katika mbawa zake; nanyi mtatoka nje, na kucheza-cheza kama ndama wa mazizini.” Malaki 4:2
  10. “Mtu wa kwenu amekuwa hawezi? Na awaite wazee wa kanisa; nao wamwombee, na kumpaka mafuta kwa jina la Bwana. Na kule kuomba kwa imani kutamwokoa mgonjwa yule, na Bwana atamwinua; hata ikiwa amefanya dhambi, atasamehewa.” Yakobo 5:14, 15



Ahadi kwa ajili ya Nguvu za Kufanya Mapenzi ya Mungu 


  1. “Umngoje Bwana, uwe hodari, Upige moyo konde, naam, umngoje Bwana.” Zaburi 27:14
  2. “Kwa hiyo hatulegei; bali ijapokuwa utu wetu wa nje unachakaa, lakini utu wetu wa ndani unafanywa upya siku kwa siku. Maana dhiki yetu nyepesi, iliyo ya muda wa kitambo tu, yatufanyia utukufu wa milele uzidio kuwa mwingi sana; tusiviangalie vinavyoonekana, bali visivyoonekana. Kwa maana vinavyoonekana ni vya muda tu; bali visivyoonekana ni vya milele.” 2 Wakorintho 4:16-18 
  3. “Tena tusichoke katika kutenda mema; maana tutavuna kwa wakati wake, tusipozimia roho.” Wagalatia 6:9 “Nayaweza mambo yote katika yeye anitiaye nguvu.” Wafilipi 4:13
  4. “Kwa maana ndiye Mungu atendaye kazi ndani yenu, kutaka kwenu na kutenda kwenu, kwa kulitimiza kusudi lake jema.” Wafilipi 2:13
  5. “Naye akaniambia, Neema yangu yakutosha; maana uweza wangu hutimilika katika udhaifu. Basi nitajisifia udhaifu wangu kwa furaha nyingi, ili uweza wa Kristo ukae juu yangu.” 2 Wakorintho 12:9



Ahadi Kuhusu Kuwa Mashahidi wa Mungu


  1. “Msiogope wala msifanye hofu; je! Sikukuhubiri haya zamani na kuyaonyesha? Na ninyi ni mashahidi wangu. Je! Yuko Mungu zaidi yangu mimi? Hakika hapana Mwamba; mimi sijui mwingine.” Isaya 44:8
  2. “Ondoka, uangaze; kwa kuwa nuru yako imekuja, Na utukufu wa Bwana umekuzukia.” Isaya 60:1 “Lakini vyote pia vyatokana na Mungu, aliyetupatanisha sisi na nafsi yake kwa Kristo, naye alitupa huduma ya upatanisho.” 2 Wakorintho 5:18
  3. “Lakini Bwana akaniambia, Usiseme, Mimi ni mtoto; maana utakwenda kwa kila mtu nitakayekutuma kwake, nawe utasema kila neno nitakalokuamuru.” Yeremia 1:7
  4. “Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.” Matendo 1:8
  5. “Bali ninyi ni mzao mteule, ukuhani wa kifalme, taifa takatifu, watu wa milki ya Mungu, mpate kuzitangaza fadhili zake yeye aliyewaita mtoke gizani mkaingie katika nuru yake ya ajabu.” 1 Petro 2:9
  6. “Mwe tayari siku zote kumjibu kila mtu awaulizaye habari za tumaini lililo ndani yenu; lakini kwa upole na kwa hofu.” 1 Petro 3:15 





Siku ya Kwanza - Jumatano - (08/01/2020) 



Hitaji Letu la Roho Mtakatifu



Fungu Elekezi:
“Lakini mtapokea nguvu, akiisha kuwajilia juu yenu Roho Mtakatifu; nanyi mtakuwa mashahidi wangu katika Yerusalemu, na katika Uyahudi wote, na Samaria, na hata mwisho wa nchi.” Matendo 1:8

Ushuhuda

“Ikiwa hii ndiyo njia tunayoweza kutumia kupata nguvu, kwa nini hatuoni njaa na kiu ya zawadi ya Roho? Kwa nini hatuizungumzii, hatuiombei, na hatuhubiri kuhusu zawadi hiyo? Bwana yu tayari zaidi kumtoa Roho Mtakatifu kwa wale wanaomtukimikia kuliko ilivyo kwa wazazi kutoa zawadi nzuri kwa watoto wao. Ili kupata ubatizo wa Roho kila siku, kila mtumishi anapaswa kuwasilisha ombi lake kwa Mungu” (Ellen White, The Acts of the Apostles, uk. 50).

Kabla tu ya kuhitimu chuo nikiwa na shahada ya theolojia, nilisoma kitabu kinaitwa They Found the Secret (Wameipata Siri) kilichoandikwa na V. Raymond Edman. Kitabu hiki hutueleza kuhusu wanaume na wanawake 20 waliofikia kipindi cha hatari ya kiroho katika maisha yao kilichopelekea uzoefu wa badiliko thabiti. Kitendo hiki kilifuatiwa na umwagwaji wa Roho Mtakatifu katika maisha yao. Wakawa watu waliobadilika na kuwa wapya – na kuongoza mamilioni kwa Kristo – kwa sababu walijazwa kwa Roho Mtakatifu. Ninapofikiria maisha yangu kama mume, baba mpya, na mchungaji mtarajiwa, niliandika dondoo katika kitabu hicho: “Ninamhitaji Roho Mtakatifu pia.” Tangu hapo nimefanya kipaumbele changu cha kwanza kuwa ni kudumisha uzoefu wangu wa badiliko na kutafuta ubatizo wa kibiblia wa Roho Mtakatifu kupitia kujifunza Biblia, utii, kushiriki na wengine, na maombi. Katika mwaka wangu wa kwanza wa uchungaji, niliitwa kumtembelea mhazini wa kanisa letu, aliyegunduliwa kuwa na kansa. Tuliomba na kumpaka mafuta kama Biblia inavyosema tufanye. Baada ya siku kadhaa, alishiriki kwa furaha kwamba aliponywa kabisa kansa yake! Ndipo nilifahamu kuwa Mungu alikuwa akisikia maombi yangu na kwamba alikubali jitihada zangu za kuyaishi maisha yangu kwa ajili yake. Vipi kuhusu wewe? Je, unamhitaji Roho Mtakatifu katika maisha yako?

Mafungu ya Biblia ya Kuombea

Siku moja Paulo aliuliza watu 12 kutoka Efeso, “Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini?” (Matendo 19:2). Je, wewe ungejibu vipi? Wale Waefeso walisema, “La, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia.” 

  1. Warumi 8:16 – Roho Mtakatifu atapokuja kati yetu, tutaungama dhambi zetu na kupokea zawadi ya wokovu kupitia kwa Yesu. Tutakuwa na uhakika wa wokovu kwa sababu sisi ni watoto wa Mungu.
  2. Ezekieli 36:25-27 – Uwepo wa Roho Mtakatifu utatupatia akili mpya na moyo mpya. Tutakuwa na ushindi dhidi ya dhambi zetu na kuona ukuaji halisi wa tabia.
  3. Yohana 7:38, 39 na Wagalatia 5:22, 23 – Tunapojazwa kwa Roho Mtakatifu, tunda la Roho – tabia ya Mungu – itatiririka kutoka kwetu kama mito ya maji ya uzima.
  4. Matendo 4:13, 31 – Uwepo wa kudumu wa Roho Mtakatifu utatuhamasisha na kututia nguvu kushiriki injili na watu wengi kadri iwezekanavyo.
  5. Yohana 16:13 – Kadri Roho anavyoishi ndani yetu, tutakuwa na njaa na upendo kwa Biblia, na atatuongoza katika kweli yote. Kweli hii si uelewa tu wa mambo lakini tabia halisi ya Kristo, ambaye ndiye kweli.
  6. Warumi 8:26, 27 – Kadri tunavyoomba katika Roho Mtakatifu, tutakuwa na nguvu katika maombi yetu na tutaona majibu mengi ya miujiza kwa maombi yetu.

Yesu alisema kwamba kutakuwa na makundi mawili ya Wakristo kabla tu ya kurudi kwake (Mathayo 25). “Ndipo ufalme wa mbinguni utakapofanana na wanawali kumi, waliotwaa taa zao, wakatoka kwenda kumlaki bwana arusi” (Mathayo 25:1). Wanawali watano walikuwa wapumbavu na hawakuwa na mafuta (uwepo wa Roho Mtakatifu; tazama Zakaria 4:1-6) katika akiba. Hawa huwakilisha wale wanaoonekana kumfuata Yesu lakini hawatendi hivyo. Wana dini bali si wa kiroho. Hivyo Yesu aliwaambia, “Siwajui ninyi!” Wanawali watano werevu walikuwa na mafuta ya kutosha. Walijazwa kwa Roho Mtakatifu na walikuwa na uhusiano halisi na Yesu.

Baada ya kupaa kwa Kristo, kama utii kwa agizo lake, wanafunzi wake walibaki Yerusalemu. “Nao walikuwa daima ndani ya hekalu, wakimsifu Mungu” (Luka 24:53). Wakati ambao hawakuwepo hekaluni, walikuwa katika chumba cha juu. “Hawa wote walikuwa wakidumu kwa moyo mmoja katika kusali, pamoja nao wanawake, na Mariamu mama yake Yesu, na ndugu zake” (Matend 1:14). Siku kumi baadae wote walibatizwa katika nguvu ya Roho Mtakatifu (Matendo 2), na watu 3,000 walibadilishwa ndani ya siku moja katiku sehemu ile moja!

Mapendekezo ya Maombi

  1. Tunakuja katika uwepo wako tukiwa na shukrani, na tunaingia katika nyumba yako tukiwa na sifa. Hatuna maneno yanayoweza kueleza kwa ufasaha namna tunavyokushukuru wewe na yale uliyotutendea. Kwa furaha na unyenyekevu tunaongeza sifa zetu za kibinadamu kwa zile sifa za malaika wasio na dhambi, ambao hufurahia daima kukuabudu!
  2. Tafadhali badilisha moyo wangu, Ee Mungu, uufanye mpya daima. Nisasishe kutoka kwenye dhambi na niandae kumpokea Roho Wako (Zaburi 51:7, 10).
  3. Bwana, tafadhali tuma uamsho wa kweli kati ya watu wako, wanaotambulika kwa tunda la Roho Mtakatifu (Wagalatia 5: 22, 23).
  4. Tubatize kwa Roho Mtakatifu na tupatie nguvu ya kutangaza injili kwa dunia iliyopotea katika giza (Matendo 1:5-8).
  5. Ee Bwana, naomba urehemu familia yangu, marafiki, wafanyakazi, na wanafunzi wenzangu. Waokowe, na naomba niwe msaidizi wako upande huu (Mathayo 28:19, 20). 
  6. Wabariki wachungaji, waalimu, wainjilisti, watendakazi wa Biblia, na watendakazi wa kanisa letu kwa nguvu ya Roho Mtakatifu (1 Timotheo 2:1-4).
  7. Ee Bwana, tafadhali warehemu walionyanyaswa na kuteswa na wapatie ulinzi wako na ukombozi kutoka kwa mikono ya wale wanaotafuta kuwaumiza (Zaburi 91).
  8. Tafadhali bariki mamia ya maelfu ya shughuli za kuwafikia watu ulimwenguni kwa mwaka 2020. Tunaomba hasa kwa ajili ya efoti za uinjilisti za Uhusishwaji wa Kila Mshiriki huko Papua New Guinea mwezi Mei 2020.
  9. Tunaomba kwa ajili ya uamsho wa kiroho kati ya vijana Waadventista wa Sabato wanaohudhuria vyuo vya kiserikali ulimwenguni. Hebu na wawe mabalozi mashuhuri wa Kristo.
  10. Tunaomba kwa ajili ya asilimia 69 ya idadi ya watu duniani ambao hawajapokea habari zisizo na mawaa za Yesu.
  11. Tunaomba kwa ajili ya watu milioni 62 katika miji 28 ambayo haijafikiwa Zaidi katika unioni ya zamani ya Kirusi (Divisheni ya Ulaya na Asia).
Nyimbo Zinazopendekezwa
  1. Nijaze Sasa #40,
  2. Moyo Safi #116
  3. Nakupenda Zaidi #48
   


Siku ya Pili - Alhamisi- (09/01/2020)

Ushuhuda wa Roho Mtakatifu

Fungu Elekezi: “Naye akiisha kuja, huyo atauhakikisha ulimwengu kwa habari ya dhambi, na haki, na hukumu.” Yohana 16:8

Ushuhuda 

“Roho Mtakatifu ni nafsi, kwani hushudia pamoja na nafsi zetu kwamba sisi ni watoto wa Mungu. Ushuhuda huu unaposhuhudiwa, hubeba pamoja nao uthibitisho wake. Katika nyakati kama hizi tunaamini na kuwa na uhakika kwamba sisi ni watoto wa Mungu” (Ellen White, Evangelism, uk. 616).

Roho Mtakatifu hutenda kazi katika maisha yetu kwa hatua tatu (Yohana 16:8-11). Kwanza, hutuonyesha dhambi zetu tunazopaswa kuleta kwa Yesu. Pili, hutuonyesha haki ya Kristo, itoshayo kutuokoa. Tatu, humuondoa Shetani na dhambi kutoka katika maisha yetu (Yohana 16:11).

Wazazi wangu walilea watoto wao sita (mimi ni wa tano) kumuamini Mungu na Biblia. Tulijifunza kwamba kulikuwa na mbingu ya kushinda na jehanamu ya kuepuka. Hata hivyo, hatukutafuta uhusiano na Mungu au kumuamini. Kaka wa mama yangu, mjomba wangu, alioa Mwadventista wa Sabato. Siku moja mjomba wangu Harold alimwambia mkewe angemthibitishia kutoka kwenye Biblia kwamba hakupaswa kuitunza Sabato (Jumamosi). Hata hivyo, baada ya kujifuna sana, aligundua kwamba Sabato ya kweli ya Biblia kwa hakika ilikuwa Jumamosi. Baadaye Harold alibatizwa na kuwa Mwandventista wa Sabato.

Baada ya muda mchache Harold alishiriki Imani yake na familia yetu, na kwa kadri nilivyojitahidi, sikuweza kupata njia ya kukanusha mafundisho ya Biblia kuhusu Sabato. Sikutaka kuitunza Sabato. Ilikuwa ni usumbufu katika mipango yangu. Baada ya muda udhihirisho wa Roho Mtakatifu kwamba nilikuwa mdhambi niliyestahili uharibifu ulijikita ndani ya akili na moyo wangu. Nilifahamu kuwa sikuwa nikimfuata Mungu, na nilifahamu kuwa sitaokolewa. Wakati huo barua ilifika kutoka kwa mjomba wangu Harold, na alielezea vile Mbingu itakavyokuwa kupitia Biblia kama mamlaka yake. Kadri nilivyosikiliza maelezo ya Mbingu, nilihisi shauku kubwa ya kutoa maisha yangu kwa Mungu. Kisha nikasikia sauti ya Mungu ndani ya moyo wangu kwa uwazi kama vile ni mtu alikuwa ameketi kando yangu. “Ni utoe maisha yako kwangu sasa, au hutayatoa kamwe.” Ghafla nilihisi wasiwasi mkuu. Nilikuwa nikiacha Mbingu kwa vitu vya dunia hii. Niliinuka kutoka kwenye kiti changu, nikaelekea chumbani kwangu, na kufunga mlango. Nilipiga magoti kando ya kitanda changu na kuomba kwa mara ya kwanza kutoka moyoni mwangu. Nilipambana kufahamu hasa cha kusema, lakini hatimaye niliomba, “Yesu mpendwa, ninatakuwa kuwa vile unahitaji niwe. Ninataka kutenda vile utakavyo nitende, na ninataka kwenda pale utakapo niende.”

Dakika niliyosema ombi hilo, nilihisi badiliko likipita katika mwili wangu. Hasira na ukorofi wangu wa awali uliachiliwa, na upendo, Amani, na furaha ya Mungu iliujaza moyo wangu. Nilifahamu kwamba Mungu alisikia ombi langu, na nilifahamu nilichopaswa kutenda. Niliinuka magotini na kwenda kumueleza mama yangu habari zile njema – kwamba sasa ningeishi kwa ajili ya Yesu na kuanza kuitunza Sabato. Machozi ya furaha yalitiririka usoni mwake. Ndani ya siku kadhaa nilanza kuachia kila kifungo cha dhambi kilichoniunganisha na dunia. Baadhi ya watu hawakuelewa uamuzi wangu, na njia mbele yangu haikuwa wazi kabisa, bali dhamiri yangu ilikuwa wazi, na furaha iliujaza moyo wangu! Baadae nilijifunza pamoja na Mchungaji wa Kiadventista na kuanza kuelewa Zaidi kuhusu nia ya Mungu kwa maisha yangu. Hatimaye nilibatizwa na kuwa mshiriki wa Kanisa la Waadventista wa Sabato. Ni uamuzi bora Zaidi niliowahi kufanya! 

Mafungu ya Biblia ya Kuombea Siku moja

Paulo aliuliza watu 12 kutoka Efeso, “Je! Mlipokea Roho Mtakatifu mlipoamini?” (Matendo 19:2). Je, wewe ungejibu vipi? Wale Waefeso walisema, “La, hata kusikia kwamba kuna Roho Mtakatifu hatukusikia.”

  1. Yohana 16:8-11 – Ni kazi ya Roho Mtakatifu kutuhakikishia dhambi zetu na kutuongoza kwa Yesu.
  2. Warumi 3:10, 23 – Hakuna mwenye haki, kwani wote tumetenda dhambi na kupungukiwa na utukufu wa Mungu.
  3. Warumi 6:23 – Mshahara wa dhambi ni mauti, bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu.
  4. Yohana 3:16 – Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa mwanawe wa pekee, ili kila amuaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele.
  5. Waefeso 2:8, 9 – Tunaokolewa kwa neema kwa njia ya Imani, wala si kwa wema wetu. Ni kipawa cha Mungu, si matendo yetu.
  6. 1 Yohana 5:11-13 – Ikiwa tumekubali Yesu kwa Imani, tunafahamu kuwa tuna uzima wa milele.
  7. Warumi 8:16 – Roho mwenyewe hushuhudia, na tunafahamu kuwa sisi ni wana na binti za Mungu.
  8. Kila siku, kadri tunavyomgeukia Yesu na kuomba, tunapokea msahama na neema. Kama watoto wa Israeli walivyotoka kila siku kupokea mana kutoka mbinguni, vivyo hivyo kila siku tunafanya upya uhusiano wetu na Yesu, Mkate wa Uzima (Yohana 6:58). Kupitia uwepo wa Roho Mtakatifu unaozunguka katika maisha yetu, tunaungama dhambi zetu kwa Mungu, na kukubali haki ya Kristo kwa niaba yetu, na tunaweza kushinda majaribu ya shetani (Wagalatia 5:16). Mapendekezo ya Maombi
  9. Mpendwa Baba wa mbinguni, ninafahamu kuwa mimi ni mwenye dhambi. Tafadhali nisamehe dhambi zangu zote kama ulivyoahidi kutenda (1 Yohana 1:9). Asante! Pia uliahidi kunipatia uzima wa milele ikiwa nitamkubali Yesu kama Mwokozi wangu. Leo ninamchagua Yesu. Ninasubiri kwa hamu ujio wa Yesu!
  10. Mpendwa Yesu, ninataka kutembea na wewe daima katika uwepo wa Roho Mtakatifu ili niweze kuhisi ujio wa Shetani na malaika zake waovu. Nipatie nguvu zako ili niweze kutambua na kushinda majaribu (Yakobo 4:7)
  11. Sasa ninakuamini, Bwana, kwa ajili ya wokovu wangu. Naomba niwe na uhakika wa furaha na kamilifu ili kwamba maisha yangu yaweze kuvuta roho zilizopotea kuja kwako.
  12. Mpendwa Baba, watu wengi katika makanisa ya ulimwengu huu wana dini tu. Hawamfahamu Yesu na neema yake iokoayo. Tafadhali mtume Roho wako Mtakatifu awadhihirishie dhambi zao na kuwaongoza kwa Yesu. Wafanye waogope sherehe za kawaida. Wawe na njaa ya uwepo halisi wa Mungu katika maisha yao.
  13. Bwana, tunaomba kwa ajili ya wale walio katika vifungo vya kiroho na kiakili waweze kuwekwa huru kutoka kwenye hatia na vifungo vingine.
  14. Tafadhali inua wanafuzi Wawaldensia wa siku za sasa, walio tayari kukutumikia katika maeneo magumu.
  15. Tunaomba kwamba Mungu ainue wamisionari wenye hekima walio tayari kufanya kazi kati ya makundi 746 ya watu katika nchi 20 za Mashariki ya Kati.
  16. Tunaomba kwa ajili ya Harakati 1,000 za Kimisionari katika Divisheni ya Kaskazini mwa Asia-Pasifiki na Divisheni ya Kusini mwa Asia-Pasifiki. Tunaomba vijana hawa watiwe nguvu kutenda kazi ya Mungu.
  17. Tunaomba kwa ajili ya watu milioni 202 katika miji 41 ambayo haijafikiwa Zaidi katika Divisheni ya Asia-Pasifiki waweze kumfahamu Yesu.
  18. Tunaombea vijana wanaoishi kwa hatari kwa ajili ya Bwana kupitia Harakati ya OYiM (One Year in Mission) na harakati ya Mission Caleb. 
  19. Pia tunaomba kwa ajili ya orodha zetu za watu saba au Zaidi [taja majina kama inawezekana]
  20. Mahitaji ya kuombea ya kanisa mahalia:

Nyimbo Zinazopendekezwa: 

  1. Kuwa na Yesu Mwokozi #51, 
  2. Roho Mtakatifu #41
  3. Taamini Nitii Pia #128 




Siku ya Tatu - Ijumaa - (10/01/2020)



Ushindi Kupitia kwa Roho Mtakatifu


Fungu Elekezi: “Basi nasema, Enendeni kwa Roho, wala hamtazitimiza kamwe tamaa za mwili.” Wagalatia 5:16.

Ushuhuda 

“Hakuna kitu ndani yake [Yesu] kilichoitikia madanganyo ya Shetani. Hakuridhia dhambi. Hakujitoa kwa dhambi hata kwa wazo tu. Hivyo inaweza kuwa kwetu. Ubinadamu wa Kristo uliunganishwa na uungu; Roho Mtakatifu aliyeishi ndani yake alimuandaa kwa ajili ya pambano. Na alikuja kutufanya kuwa washiriki wa asili ya uungu. Tutakapoungana naye kwa Imani, dhambi haitakuwa na nguvu dhidi yetu. Mungu huushikilia mkono wa Imani ndaniyetu ili auongoze kushikilia kwa haraka utakatifu wa Kristo, ili tuweze kupata ukamilifu wa tabia” (Ellen White, The Desire of Ages, uk. 123).

Jerry alikuwa mfanyakazi mwenye bidii. Alitumia muda mwingi wa utu uzima wake kama mfanyakazi wa vifaa vya chuma akijenga madaraja na magorofa. Alikuwa ni mtu aliyepanda mamia ya futi juu ya nchi kwenye chuma nyembamba na kuichomelea kwenye chuma nyingine. Ingawa Jerry alikuwa na kipaji sana na mtenda kazi mashuhuri, aliharibu mwili wake kwa pombe, tumbaku, madawa, wanawake, na maisha yasiyofaa. Wakati wo wote Mkristo alipokuja kazini, Jerry alimtesa kwa maneno na kihisia, akitegemea kumfanya aiache kazi hiyo. Jerry alichukia Ukristo na Wakristo.

Kadri Jerry alivyokaribia miaka 50, alianza kupata msongo. Siku moja aliamua kusitisha maisha yake. Kadri alivyokuwa akiendesha kuelekea nyumbani ili kujiua, aliona kibao cha Kanisa la Waadventista wa Sabato barbarani. Roho Mtakatifu aliweka wazo akilini mwake: “Pengine wanaweza kunisaidia.” Hivyo Jerry aliegesha gari sehemu sahihi mara tu shule ya kansia ilipokuwa ikimaliza ratiba zake kwa siku hiyo, alimkaribia mkuu wa shule, na kunong’oneza kitu kuhusiana na kuhitaji msaada. Mkuu alimpatia Jerry namba yangu ya simu na kumwambia, “Hii ni namba ya mchungaji wetu. Tafadhali mpigie.” Jerry alipopiga usiku ule, alinieleza kwamba aikuwa kwenye matatizo na akauliza kama naweza kumsaidia. Nilimpigia mzee wa kanisa, na pamoja tulienda nyumbani kwa Jerry. 

Jerry alitueleza kila kitu na kuongeza, “Siamini kwamba nimeanguka sana kiasi cha kuwa na mchungaji nyumbani kwangu.” Alisema alijaribu kila kitu dunia iliweza kutoa bila kupata suluhisho, hivyo aliamua kusitisha maisha yake. Nikasema, “Jerry haujajaribu kila kitu kwa sababu haujamjaribu Yesu.” “Upo sahihi,” alihamaki, “Sijamjaribu Yesu. Hivyo, ninapaswa kufanya nini kumjaribu Yesu?” nilishiriki ujumbe rahisi wa injili na kumuliza, “Je, kuna sababu yo yote ya kukufanya usitake kumpokea Yesu katika maisha yako?” Jerry alisema, “Hapana, kwa sababu asipotenda kitu kwa ajili yangu usiku wa le, nitasitisha maisha yangu.”

Huku nikimualika Jerry kupiga magoti pamoja nasi, nilimuomba arudie ombi baada yangu. Baada tu ya sisi kusema “Amina,” Jerry alishika mkono wangu na kusema, “Umeona?” “Nimeona nini?” niliuliza. “Niliposema tu ‘Amina,’ nilifungua macho yangu na kuona mtu akipita juu ya kichwa changu akiwa na uso wa ukali, na kasha akapotelea kwenye dari. Unapaswa kuniamini!” “Ninakuamini, Jerry,” nilisema. “Unajisikiaje sasa?”Baada ya muda wa kutafakari alisema, “Ninajisikia vizuri, vizuri sana. Sijajisikia vizuri hivi kwa muda mrefu sana, kama nilishawahi. Nini kimenitokea?” Nilimueleza, “Jerry, umemuomba Yesu aingie katika maisha yako na kukusamehe dhambi zako. Sasa anaishi ndani yako. Roho ya uovu uliyoiona ilikuwa ikijaribu kukufanya usitishe maisha yako, lakini Yesu ameiondoa.”

Furaha kuu ilijaa nyumbani kwa Jerry usiku ule, furaha nyingi kiasi cha Jerry kushindwa kulala. Alizunguka nyumbani kwake akiondoa pombe, madawa, magazeti, na vitu vingine vyote ambavyo aliona ni vyenye dhambi. Aliweka vitu vyote katika mfuko wa plastiki na kuvizika futi sita kwenda chini katika shamba lake. Siku iliyofuata aliendesha gari kuelekea kwenye duka la mimea na kununua mti ili kuupanda sehemu alipozika vitu vyote vile. Nilipomtembelea tena alinionyesha mti ule na kusema, “Mchungaji, shimo hilo na mti huo unawakilisha maisha yangu. Jerry wa zamani amezikwa hapo chini na mti huo mpya wa matunda unawakilisha Jerry mpya kwa sababu sasa ninaishi maisha mapya.”

Mafungu ya Biblia ya Kuombea
  1. Yohana 16:8-11 – Ni kazi ya Roho Mtakatifu kutuhakikisha kwa dhambi zetu na kutuongoza kwa Yesu.
  2. Ezekieli 36:25, 26 – Tumeahidiwa moyo mpya, akili mpya, na maisha mapya.
  3. 2 Wakorintho 5:17 – Mtu ye yote akiwa ndani ya Kristo, amekuwa kiumbe kipya. Ya kale yamepita. 
  4. Yohana 8:36 – Unaweza kuwa huru kwelikweli kupitia kwa Yesu Kristo.
  5. 1 Wathesalonike 4:3 – Ni nia ya Mungu kwamba wewe uingie katika ushindi dhidi ya dhambi. 
  6. Warumi 6:14 – Dhambi haitakutawala tena.
  7. Mathayo 5:29, 30 – Jitenge kutoka kwa mtu au kitu cho chote kinachokushawishi kuingia dhambini.
  8. Warumi 12:21 – Weka watu  na vitu chanya badala ya watu na vitu hasi
  9. Wagalatia 5:19-26 – Tamaa za mwili zilizo za uovu zinaweza kufunikwa kwa tunda la Roho. 
Kila siku, kadri tunavyomgeukia Yesu na kuomba, tunapokea msahama na neema. Kama watoto wa Israeli walivyotoka kila siku kupokea mana kutoka mbinguni, vivyo hivyo kila siku tunafanya upya uhusiano wetu na Yesu, Mkate wa Uzima (Yohana 6:58). Kupitia uwepo wa Roho Mtakatifu unaozunguka katika maisha yetu, tunaungama dhambi zetu kwa Mungu, na kukubali haki ya Kristo kwa niaba yetu, na tunaweza kushinda majaribu ya shetani (Wagalatia 5:16).

Mapendekezo ya Maombi

  1. Mpendwa Bwana, ninafahamu kwamba ni mapenzi yako mimi kushinda dhambi kwa nguvu zako. Tafadhali nijaze kwa Roho wako Mtakatifu na niongoze katika kweli yote (Yohana 16:13).
  2. Katika jina la Yesu na kupitia kwa damu yake, ninamkemea Shetani na roho zake za uovu katika maisha yangu. Tafadhali, Bwana, muondoe muovu ndani ya maisha yangu na nyumba yangu. Ruhusu kweli na haki pekee zikae ndani yangu.
  3. Mpendwa Bwana, jaza maisha yangu kwa uwepo wa Roho Mtakatifu. Naomba nguvu zake zitiririke kupitia kwangu na kuhudumu kwa wale ambao bado wamefungwa katika dhambi. Walete kwa Yesu ili vifungo vyao viweze kuvunjwa.
  4. Bwana, tusaidie kuwa na uvumilivu na upendo, tukionyesha upendo na huruma yako kwa wale wanaotukasirisha au kutushutumu.
  5. Tunaomba kwa ajili ya wale wanaohudumia wazee wao wanafamilia wagonjwa. Wapatie uvumilivu, nguvu, na upendo.
  6. Bwana, tafadhali punguza wasiwasi wa wale wanaopitia magonjwa yasiyotibika. Wapatie ujasiri na Amani ya Yesu.
  7. Tunaomba kwa ajili ya Idara ya Shule ya Sabato na Idara ya Huduma binafsi ya kila kanisa mahalia kadri wanavyotafuta mpango wa Mungu na kuzifikia jamii zao kwa huduma za upendo, Kujifunza Biblia, na ushuhudiaji binafsi.
  8. Tunaomba kwa ajili ya ubatizo wa Roho Mtakatifu kwa vijana wetu na viongozi vijana kama ilivyoahidiwa katika Matendo 1:8. Na tunaomba hasa kwa ajili ya mibaraka ya Mungu kwa vijana waliohusika katika shughuli ya “Give Him 20” (Mpatie 20) na mipango mingine ya maombi. 
  9. Bwana, tafadhali tuonyeshe mkakati uliokubaliwa na Mungu wa kufikia Yeriko a dunia kwa Ujumbe wa Malaika Watatu na kuongoza akina Rahabu katika kila mji kwenye wokovu katika Kristo.
  10. Tafadhali bariki siku 100 za Maombi (Machi 27 – Julai 4) kuelekea kwenye Mkutano wa Uchaguzi wa Konferensi Kuu. Mwaga Roho Wako Mtakatifu kadri tunavyoomba hekima na ujio wako ulio karibu.
  11. Pia tunaomba wka ajili ya orodha yetu ya watu saba au Zaidi [taja majina kama inawezekana]

Mahitaji ya kuombea ya kanisa mahalia:


Nyimbo Zinazopendekezwa
  • Yesu Unipendaye #30,
  • Yesu Nataka Kutakaswa Sana #114
  • Twae Wangu Uzima #146



Siku ya Nne - Jumamosi - (11/01/2020)

Ubatizo wa Roho Mtakatifu

Fungu Elekezi: “Hata alipokuwa amekutana nao aliwaagiza wasitoke Yerusalemu, bali waingoje ahadi ya Baba, ambayo mlisikia habari zake kwangu; ya kwamba Yohana alibatiza kwa maji, bali ninyi mtabatizwa katika Roho Mtakatifu baada ya siku hizi chache.” Matendo 1:4, 5.

Ushuhuda 

“Unapokuwa umepokea ubatizo wa Roho Mtakatifu, utaelewa zaidi furaha za wokovu kuliko ulivyokuwa ukifahamu maisha yako yote” (Ellen White, Manuscript Releases, vol 5, uk. 231).

Nilimtembelea mtu aliyekuwa akikaribia kufariki kwa ugonjwa usiotibika. Niliomba na kujaribu kumtia moyo kwa upendo na rehema za Mungu, lakini nilipoondoka nyumbani kwake, nilikumbwa na namna nilivyokuwa nikihisi kutokuwa na nguvu katika hali ile – na namna Wakristo wengi wanaonekana kutokuwa na nguvu. Kadri nilivyolinganisha maisha yangu na maisha ya Wakristo wngine pamoja na maisha ya Wakristo wa Agano Jipya, tofauti ilikuwa ikishangaza. Kama matokeo ya ugeni ule, niliamua kujifunza kwa kina somo la Roho Mtakatifu katika Biblia. Hatimaye nilijifunza mafungu 273 katika lugha za asili ambayo huzungumza moja kwa moja katika kazi ya Roho Mtakatifu, na niligundua zaidi ya nukuu za pekee 2,000 za maandiko ya Ellen White juu ya mada hii.

Katika kujifunza kwangu Biblia niligundua ubatizo wa Roho Mtakatifu. Uzoefu ule ulibalisha maisha ya Petro, Paulo, na kila mmoja aliyepokea Roho wa Mungu kwa ukamilifu. Hata Yesu alijazwa na Roho Mtakatifu, kwani kabla ya Roho Mtakatifu kushuka kwake kwa mfano wa hua, alidumu kuwa katika karakana ya seremala. Baada ya Roho kushuka juu yake, Yesu alitenda kazi ya Masihi.

Katika visa vya Biblia, daima tunapata uthibitisho unaoonyesha kwamba nguvu ya Roho Mtakatifu imetolewa. Usiku wa siku ya Ijumaa majira ya saa 4, binti yetu mwenye umri wa miaka 8 alimuita Mama yake. Mke wangu alipokuwa akimuendea, niliamua kwenda ofisini kwangu na kuomba. Nilipokuwa nikiomba, nilihisi uwepo mtakatifu wa Yesu ukiingia kwenye chumba kile. Nilianza kunena na Bwana kwa hamasa kuu na njaa ya uwepo wa Roho wake katika maisha yangu. Ghafla nilimuona Yesu katika mlango wa kanisa langu kwa upendo akiweka mkono wake wenye alama za misumari kwenye mabega ya kila mshiriki akiwa na mtazamo wa neema na ukaribisho. Yesu aliniuliza, “Je, unawapenda watu wangu?” ningeweza kusema niliwapenda, lakini ilinibidi kukubali kwamba baadhi yao ilikuwa vigumu kuwapenda. Machozi yalianza kunitiririka kadri nilivyoungama dhambi yangu. Kisha niliona miguu iliyokuwa na alama za misumari ikisimama kwenye mimbara ambayo nilihubiri kila juma. Yesu alisema, “Nilikufa ili nisamehe na kuokoa watu wa dunia hii. Je, unahubiri injili kila siku kwa shauku kwa ajili ya nafsi zilizopotea?” ningeweza kusema ilikuwa shauku yangu kuhubiri injili kwa uharaka wa kuokoa waliopotea, lakini nilijihisi kutostahili katika uwepo wake. Machozi yalitirirka kadri nilivyoungama dhambi zangu kwa Yesu. Kasha niliona taji ya miba ikilazimishwa katika kichwa chake. Nilimsikia Yesu akisema, “Nilijinyenyekeza hata mauti ya msalaba. Je, unatafuta sifa kutoka kwa wanadamu?” ningeweza kusema sikutaka sifa za wanadamu, lakini kwa machozi nilikubali kuwa nilipambana na kiburi. Nilijihisi kutostahili na kutokukubalika katika uwepo wake, na mahozi yalinitiririka ziadi. Ghafla Yesu alivua kando vazi lake, na nikaona upande ambapo mkuki ulimchoma. Alisema, “Wale wanaonijia sitawatupa kamwe.”

Kisha nilihisi upendo kamili na ukubali wa Bwana kuliko nilivyowahi kuhisi hapo kabla. Nilifahamu kuwa dhambi zangu zilisamehewa, na nilifahamu kuwa alinikubali. Nilizama katika ufunuo huo wakati nilipomsikia mke wangu akishuka ngazi. Nilitazama saa; ilikuwa ni saa 6 usiku. Masaa mawili yalionekana kama dakika chache tu. Sikuwa tayari kuzungumza kuhusu kilichotokea, hivyo nilirudi kitandani na kugeuza mgongo wangu mlangoni ili mke wangu asione kama nilikuwa macho. Alipoingia chumbani, aliuliza, “Nini kimekutokea?” Nilisema, “Unamaanisha nini?” Alisema, “Ninafahamu kuna kitu kimekutokea. Ninaona. Nini kimetokea?” Hivyo nilimweleza kila kitu, na wakati huo huo mke wangu alitoka kuelekea sebuleni na kuomba mwenyewe. Niliweza kumsikia akimuita Mungu aweze kubarikiwa pia.

Siku iliyofuata, Sabato, nilihisi nguvu ya Mungu kadri nilipohubiri somo langu. Baadhi ya watu walifanya maamuzi kwa ajili ya Kristo siku ile. Baadaye mtu mmoja aliuliza, “Mchungaji, kuna kitu kilikutokea jana usiku?” Nikiwa nimeshangaa, nilisema, “Kwa nini unauliza?” Alisema, “Ninafahamu kuna kitu kitakuwa kimekutoka jana usiku. Wakati wote ulipokuwa ukihubiri, niliona mng’ao katika uso wako.” Niliposhiriki kilichotokea, alisema, “Kwa hakika Bwana amekutembelea.” Mwaka ule watu 37 walitoa maisha yao kwa Yesu. Katika miaka iliyofuata baada ya usiku ule, mamia ya watu wamefanya maamuzi kwa ajili ya Kristo. Bwana Yesu asifiwe milele!

Mafungu ya Biblia ya Kuombea.
  1. Luka 3:21, 22 - Baada ya ubatizo wake, Yesu aliomba Roho Mtakatifu aje juu yake. 
  2. Matendo 1:5-8 – Utapokea nguvu akisha kukujilia Roho Mtakatifu. x Matendo 2:1-4 – Na wote wakajazwa Roho Mtakatifu na kuanza kunena kwa lugha mbalimbali.
  3. Matendo 4:31 – Kanisa la awali lilipokea nguvu kadri lilivyoomba kwa ajili ya Roho wa Mungu kuja juu yao.
  4. Matendo 8:15-17 – Walibatizwa kwa maji katika jina la Yesu, bali walihitaji Roho Mtakatifu.
  5. Luka 11:11-13 – Ubatizo wa Roho Mtakatifu unatolewa kwa wale wanaomtafuta kupitia maombi.
  6. Matendo 5:31, 32 – Roho Mtakatifu atatolewa kwa wale walio tayari kutii. Mapendekezo ya Maombi
  7. Mpendwa Baba, tafadhali nibatize katika Roho Mtakatifu ili niweze kuishi na kukupenda kwa mafanikio.
  8. Ni shauku yangu kuu, Bwana Yesu, kwamba nikuwakilishe vyema kwa ulimwengu. Tafadhali andaa moyo wangu kumpokea Roho Mtakatifu na kushiriki upendo wako na watu wengine katika maisha yangu.
  9. Tafadhali niongoze katika kweli yote ili daima niweze kutenda yale yapendezayo machoni pako. Mruhusu Roho wako Mtakatifu adhihirishe kwangu kile unachotaka nifahamu na unachotaka nishiriki na wengine. Naomba misimamo na mizigo yangu itoke moyoni mwako na si kutoka kwenye matendo yangu ya ubinafsi.
  10. Tunamba kwamba wapendwa wetu walioiacha Imani wakumbuke inavyokuwa wakiwa katika ushirika na wewe na kutamani kuunganika tena na wewe. Wasaidie kuhisi na kukubali upendo na msamaha wako.
  11. Bwana, tunaomba ulinzi wako kwa wamisionari wanaofanya kazi katika maeneo hatarishi.
  12. Tunaomba kwa ajili ya watu milioni 16 katika miji 6 ambayo haijafikiwa Zaidi ya Divisheni ya Kusini mwa Pasifiki. Tunaomba kwa ajili ya ubatizo wa kila siku wa Roho Mtakatifu kwa washiriki kadri wanavyowafikia kwa upendo wale ambao hawajafikiwa bado.
  13. Tunaomba kwamba Roho Mtakatifu atusaidia kufahamu namna ya kuwafikia watu milioni 406 katika miji 105 isiyofikiwa Zaidi ya Divisheni ya Kaskazini mwa Asia-Pasifiki.
  14. Tafadhali bariki Huduma za Chaplensia za Kiadventista kadri zinavyosimamia chaplensia na washiriki wenye shauku katika kuhudumia wale walio katika magereza. 
  15. Pia tunaomba kwa ajili ya orodha yetu ya watu saba au Zaidi [taja majina kama inawezekana]
  16. Mahitaji ya kuombea ya kanisa mahalia:

Nyimbo Zinazopendekezwa

  1. Tubatize Upya #189, 
  2. Ati Kuna Mvua Njema #39
  3. Roho Yangu Amka Sasa #66 



Siku ya Tano - Jumapili - (12/01/2020)


Tunda la Roho Mtakatifu


Fungu Elekezi: “Lakini tunda la Roho ni upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi; juu ya mambo kama hayo hakuna sheria.” Wagalatia 5:22, 23.

Ushuhuda 

“Kweli inapopendwa na kuthaminiwa, na kuchukuliwa kama mali takatifu, ni wazi kwamba Roho Mtakatifu ndiye ameipanda ndani ya moyo. Kisha upendo utatiririka ndani ya moyo kama kijito cha maji ya uzima, kinachotiririsha uzima wa milele. Upendo huu unapokuwa ndani ya moyo, mtendakazi hataona uchovu katika kazi ya Kristo” (Ellen White, Review and Herald, vol. 3, uk. 121, Feb. 13, 1894).

Shemasi mmoja, aliyefahamika kama mtu mwenye msaada na mvuto, alikuwa na tatizo kubwa la tabia ambalo mkewe na watoto pekee ndiyo walifahamu. Kazini au katika maburudisho yake na wengine, alikuwa mtu wa kirafiki sana unayeweza kutamani kukutana naye. Nyumbani, mara nyingi alikuwa mtu asiyevumilika. Anaweza kuwa na badiliko la tabia na mwenye kukasirisha. Nyakati nyingine hasira ilitawala, na alikuwa akiwatesa kihisia na kuwaadhibu sana watoto wake.

Shemasi huyo alifahamu hitaji lake. Alijichukia kwa kulipuka nyumbani. Alitambua kwamba alionyesha kitu kimoja mbele za watu na kuishi maisha tofauti nyumbani. Nyakati nyingine alitambua kwamba alipaswa kuhudhuria madarasa ya kutawala hasira, lakini aliogopa matokeo ya kukubali tatizo lake kanisani. Pia alifahamu kwamba alipaswa kupata ushauri, lakini alikatishwa tamaa na wazo la kumlipa mtu ili amsikilize. Kiburi chake kilimtenga na msaada aliohitaji. Alikuwa mtu wa dini bali si mtu wa kiroho – alihitaji kubadilishwa na kuwa na uwepo wa kudumu wa Roho Mtakatifu katika maisha yake.

Majira fulani ya mwaka, alikuja mhubiri katika mji wao na kuendesha mfululizo wa mikutano ya uamsho. Kwa sababu ya cheo chake kanisani, shemasi yule alihudhuria kila mkutano, japokuwa moyo wake ulikuwa kama jiwe. Maombi mengi yalitendeka katika mikutano hii, na Roho Mtakatifu alikuwa akitenda kwa njia za kimiujiza. Binti mmoja alifanya upya uhusiano wake na Yesu na kufanya ungamo la hadhara la dhambi zake, akiomba maombi na msaada wa kusanyiko lile. Mwanamke asiyekuwa Mkristo aliyehudhuria pamoja na rafiki aliyatoa maisha yake kwa Yesu. Maisha yalibadilika kadri watu walivyosogea mbele wakati wa wito kila usiku. 

Usiku mmoja, karibia na miisho ya mikutano hiyo, wito ulipotolewa shemasi yule aliinuka na kwenda mimbarani. Akiwa na machozi usoni mwake, alielekea mbele pamoja na wengine walioitikia wito wa Mungu mioyoni mwao. Pale mbele ya kanisa, alianguka magotini, akainua mikono yake, na kusema kwa sauti, “Mungu, nisamehe mimi, mdhambi!” watu waliomfahamu shemasi yule walishangazwa kumsikia akiomba ombi lile mbele za watu, lakini hiyo haikuwa mwisho. Shemasi yule aliinuka, akageukia mkutano, na kusema, “Nina tatizo baya sana la hasira. Mimi si mume na baba ninayepaswa kuwa. Ninahitaji kuungama dhambi zangu, kutafuta msaada, na nyumbani kwangu kuwa mwanaume ambaye wote mnamfahamu hadharani.” Muda huu mke na watoto wake walikuwa wamemzunguka huku wakilia na kumkaribia mume na baba yao. Washiriki wa kanisa nao walimzunguka, mchungaji aliweka mikono yake juu ya baba yule, na walikuwa na kipindi cha maombi cha ajabu usiku ule!

Shemasi yule alikuwa muaminifu kwa neno lake. Kwa msaada wa Mchungaji alipata mshauri, na pia alianza kuhudhuria madarasa ya kutawala hasira. Muhimu aidi, alianza masomo ya Biblia ya kila juma pamoja na mchungaji – si kuelewa mafundisho bali kutafuta uhusiano halisi na Yesu. Roho Mtakatifu alimbariki shemasi yule na alianza kumjaza kwa tunda la Roho. Si mke na watoto wake tu walioona badiliko bali washirki wa kanisa na jamii iliweza kuona pia. Shemasi alikuwa na Amani. Alikuwa mtu mwema Zaidi. Wema na upendo wake, hasa kwa mke na watoto wake, ulikuwa wazi kwa kila mtu. Furaha na mibaraka ya Yesu, kupitia kwa Roho Mtakatifu aliyedumu ndani yake, ilibadilisha nyumba ya shemasi yule kuwa mfano mdogo wa mbingu duniani.

Mafungu ya Biblia ya kuombea
  1. Wagalatia 5:19-23 – Kazi za mwili huondolewa kwa tunda la Roho Mtakatifu: upendo, furaha, amani, uvumilivu, utu wema, fadhili, uaminifu, upole, kiasi.
  2. Yohana 13:35 – Watu watatufahamu kuwa ni Wakristo wa kweli kupitia upendo tunaouonyesha.
  3. 1 Petro 1:8 – Tutakuwa na furaha isiyoelezeka.
  4. Wafilipi 4:7 – Amani ya Mungu italinda mioyo na akili zetu.
  5. 2 Wakorintho 3:18 – Kwa nguvu ya Roho Mtatifu tunabadilishwa na kuwa na sura ya Yesu.
  6. Yohana 7:38 – Mito ya maji ya uzima itatiririka kutoka mioyoni mwetu. 
Mapendekezo ya Maombi
  1. Mpendwa Yesu, ninataka kuakisi tabia yako kwa kila mtu ninayemfahamu na kwa wote ninaokutana nao. Nijaze kwa Roho wako Mtakatifu, na ruhusu tunda la roho ling’ae kutoka moyoni mwangu.
  2. Tafadhali nisaidie kuwa Mkristo halisi Zaidi nyumbani kuliko sehemu nyingine. Naomba wale wanaonifahamu vema waweze kukuona wewe Zaidi ndani yangu.
  3. Nifanye niwe mto wa mibaraka kadri ninavyoshiriki upendo, furaha, na Amani yako pamoja na dunia ninapoishi.
  4. Kadri ninavyotumia muda katika maombi na kujifunza Biblia, tafadhali nibatize Zaidi na Zaidi kwa Roho wako Mtakatifu. Naomba neema isiyo na kikomo itiririke kupitia kwangu na kuuendea ulimwengu unaoumia.
  5. Msifu Mungu, Ee moyo wangu, na liabudu jina lake takatifu. Furaha yake na ijaze nafsi yangu!
  6. Bwana, tafadhali safisha mioyo ya wale walio katika huduma wenye wasiwasi. Wakumbushe kwamba wanatenda mapenzi yako. Tafadhali waruhusu waone matunda ya kazi yao, hata ikiwa ni nafsi moja tu.
  7. Bwana, tunakumbuka waalimu wetu wa Shule ya Sabato. Tafadhali wasaidie kufahamu kazi yao ilivyo ya muhimu kwa watoto wetu.
  8. Bwana, tunaomba uongozi wako katika Vituo vingi vya Vivutio, programu za afya na familia, na klabu za Watafuta Njia duniani.
  9. Bwana, tafadhali tuonyeshe namna ya kutuma machapisho yaliyojazwa kweli (yaliyochapishwa na kielektroniki) katika jamii zetu. Tunaomba kwamba watu wayasome na Roho Mtakatifu awaonyeshe kweli ya Biblia.
  10. Tafadhali inua wainjilisti wa vitabu, wanafunzi wa kujitolea, waandishi, waliobobea katika masuala ya vyombo vya habari, na wategemezaji wa kifedha ili kusambaza maneno ya tumaini na uzima.
  11. Pia tunaomba wka ajili ya orodha yetu ya watu saba au Zaidi [taja majina kama inawezekana]
  12. Mahitaji ya kuombea ya kanisa mahalia:
Nyimbo Zinazopendekezwa: 
  1. Kumtegemea Mwokozi #129,
  2. Yesu Nakupenda #29
  3. Mishale ya Nuru #164



Siku ya Sita - Jumatatu - (13/01/2020)


Zawadi za Roho Mtakatifu


Fungu Elekezi: “Basi pana tofauti za karama; bali Roho ni yeye yule. Tena pana tofauti za huduma, na Bwana ni yeye yule. Kisha pana tofauti za kutenda kazi, bali Mungu ni yeye yule azitendaye kazi zote katika wote. Lakini kila mmoja hupewa ufunuo wa Roho kwa kufaidiana.” 1 Wakorintho 12:4-7.

Ushuhuda 

“Ni usaidizi wa Roho Mtakatifu wa Mungu ndio unaoandaa watendakazi, wanaume na wanawake, kuwa wachungaji kwa watu wa Mungu… wale walio na Imani katika mtumishi wa kimbingu [Roho Mtakatifu] wataendelea. Watazawadiwa nguvu ya kuvita ujumbe wa kweli kwa uzuri mtakatifu” (Ellen White, Gospel Workers, aya. 96, 97).

Simu iliita ofisini kwangu mjini Albany, Oregon. “Je, huyu ni mchungaji wa Kanisa la Waadventista wa Sabato?” sauti ya kike iliuliza. “Ndiyo.” Nilijibu. “Unapaswa kuja hospitali sasa hivi. Tuna mgonjwa hapa mwenye matatizo ya mapigo ya moyo. Tunadhani anaweza kufa, lakini hataki kuturuhusu kufanya cho chote hadi mchungaji kutoka kwenye Kanisa la Waadventista amuombee. Anaendelea kusisitiza kwamba mchungaji kutoka Kanisa la Waadventista akimuombea, atapona. Tafadhali njoo haraka!”

Nikiwa naendesha gari kuelekea hospitali, niliomba, “Bwana, nina wasiwasi kidogo kuhusu ugeni huu. Binti huyu anaendelea kuwaeleza watu kwamba mchungaji wa Kanisa la Waadventista akimuombea, atapona. Sote, wewe na mimi tunafahamu kwamba si kila muda unachagua kumponya mtu. Wauguzi na madaktari wale watasema nini ikiwa hutamponya Binti huyu?” Ilionekana kama bwana alijibu kwa kusema, “Unahofia nini?” “Ninahofia sifa yako njema,” nilisema. “Sasa, ngoja niweke hili sawa, “Bwana alionekana kunena. “Unahofia sifa yangu njema?” “SAWA,” niliendea, “Ninatambua hilo linaonekana jambo la kipuuzi kidogo, lakini watu watasema nini – binti yule atasema nini – ikiwa hutamponya?” Bwana alinena moyoni mwangu, “Ni wajibu wako kuwa mtii. Ni wajibu wangu kushughulikia sifa yangu njema.” “Upo sahihi,” nilisema. “Nitakuamini na kukuacha utende unachoona ni bora.”

Pale hospitalini nilikutana na wauguzi wanne nje ya chumba cha mgonjwa yule. “Je, wewe ndiye mchungaji wa Kiadventista?” muuguzi mmoja aliuza. “Harakisha uingie na kuomba ili tuweze kufanya kitu!” nilikwisha kufahamu kutokana na jina la binti huyu nililopewa na muuguzi kwamba si muumini wa kanisa langu au kanisa la karibu. Nilijiuliza kwa nini alisisitiza kuombewa na mchungaji wa Kiadventista, lakini huu haukuwa muda wa kuanzisha mazungumzo. Mashine ya kuendeshe moyo wake ilionyesha mapigo ya moyo yanayobadilika badilika. Nilifahamu kwamba alikuwa katika matatizo. Nitembea kuelekea kando ya kitanda chake na kuushika mkono wake wa kuume. Aligeuka kidogo, akafumbua macho, na kuuliza, “Je, wewe ndiye mchungaji wa Kiadventista?” “Ndiyo,” nilisema. “Ukiniombea, ninafahamu kuwa nitaponywa,” alisema.

Huu haukuwa muda wa hubiri au kujifunza Biblia juu ya maombi kwa ajili ya wagonjwa. Kwa urahisi nilimuuliza, “Dada, upo tayari kumruhusu Yesu aamue kitakachotendeka leo hapa?” “Oh, ndiyo, mchungaji,” alisema, “lakini ninafahamu kwamba ukiniombea, nitaponywa!” Hivyo nilifumba macho yangu na kumuomba Mungu wa mbinguni kuonyesha nguvu zake na neema zake kwa binti huyu. Nilimuomba alitukuze jina lake mbele ya wauguzi na madaktari katika hospitali ile, na kwamba uponyaji wa binti huyu uwe ushuhuda kwa watu wengi. Nilimuomba Mungu amponye kama ndiyo yalikuwa mapenzi yake, kama kumponya kutaleta utukufu kwa jina lake, na kama ilikuwa kwa nia njema kwake. Nilimaliza ombi langu kwa jina la Yesu na kusema “Amina.” Nilipofumbua macho yangu, nilitazama mashine, na ilionyesha mtiririko thabiti wa mapigo ya moyo! Binti yule alishika mkono wangu kwa furaha na kusema, “Ninajisikia vizuri. Nimeponywa! Nilijua kwamba kama mchungaji wa Kiadventista akiniombewa, ningeponywa!”

Nilikumbuka namna Yesu alishughulika na hali kama hizi katika maisha yake, hivyo nilisema, “Dada, Imani yak imekuponya!” Nilimshukuru Mungu na kutoka katika chumba kile. Muuguzi alisema, “Tunaweza kuingia sasa?” Nilijibu, “Ndiyo, lakini sidhani kama anawahitaji tena.” Macho yao yalifumbuka Zaidi kwa mshangao, na wakakimbia kuingia kwenye chumba kile. Siwezi kukueleza kilichotokea tena baada ya pale kwani niliondoka. Sikutaka wauguzi au binti yule kunitazama kama mimi ndiye niliyemponya. Ilikuwa ni karama ya uponyaji iliyotolewa na Roho Mtakatifu kwa ajili ya binti yule kwa wakati ule.

Mafungu ya Biblia ya Kuombea:
  1. 1 Wakorintho 12:9 – Karama ya uponyaji imetajwa. Bwana ana njia nyingi za kuponya watu, na anataka kudhihirisha nguvu yake ya uponyaji kupitia watu wake.
  2. Waefeso 4:11-13 – Roho Mtakatifu anataka kutoa karama nyingi kwa watu wake. Mungu ana mpango kwa ajili yako pia.
  3. Luka 5:17 – Nguvu ya Bwana ipo ili iponye. 
  4. 1 Wakorintho 14:1, 13 – Tamani karama za roho na omba kwamba uzipokee.
  5. Ufunuo 1:10 – Roho Mtakatifu anapokuja juu yetu, tunaweza kumsikia Mungu kwa njia mpya na yenye nguvu.
Mapendekezo ya Maombi
  1. Nipo hapa, Bwana, nitumie katika huduma kila. Nijaze kwa Roho yako na kunijaza karama zako.
  2. Mpendwa Yesu, ninataka kufanya badiliko kwa ajili yako katika dunia hii. Sifurahishwi na kukaa tu kanisani. Nipatie nguvu ya Roho wako kupitia karama unazonichagulia ili niweze kushinda nguvu za dhambi katika dunia hii.
  3. Bwana, ongeza karama zetu kwa elimu, semina, uzoefu, na maombi. Tunaweka wakfu talanta zetu kwako na kwa unyenyekevu tunaomba kwamba uongeze mibaraka yako isiyo ya kibinadamu ili kwamba injili isonge mbele kwa nguvu.
  4. Tunaomba kwa ajili ya shule 8,208 za Kiadventista zenye wanafunzi karibia milioni 2. Hebu shule hizi zifundishe daima kweli za Biblia na kuwaongoza vijana katika utume na huduma.
  5. Bwana, tupatie hekima ya kufikia tamaduni zisizo na dini ambazo hazina shauku katika dini. Mruhusu Roho wako Mtakatifu avunje kuta zinazoizunguka mioyo isiyokuwa na dini.
  6. Tunaomba kwa ajili ya makundi ya watu katika Asia ambayo hayana historia ya Ukristo. Tupatie hekima ya kuyafikia mahitaji yao.
  7. Bwana, tafadhali tia msukumo kwa Waadventista wa Sabato ulimwenguni wa kuomba kuliko ilivyowahi kutokea hapo kabla. Tusiadie kutsihi pamoja kwa ajili ya mvua ya masika ya Roho Mtakatifu. Tunaomba ukamilisho ulioahidiwa wa Yoeli 2, Hosea 6, na Matendo 2.
  8. Tunaomba kwa ajili ya makundi 541 ya watu katika nchi 18 za Divisheni ya Kusini mwa Afrika-Bahari ya Hindi. Tadhali wangoze katika kweli ya Kibiblia.
  9. Pia tunaomba wka ajili ya orodha yetu ya watu saba au Zaidi [taja majina kama inawezekana]
  10. Mahitaji ya kuombea ya kanisa mahalia:

Nyimbo Zinazopendekezwa

  1. Tupe Moto wa Uhai #81,
  2. Nijaze Sasa #40
  3. Ninaye Rafiki #49




Siku ya Saba - Jumanne - (14/01/2020)



Kuomba katika Roho Mtakatifu



Fungu Elekezi:
“Kwa sala zote na maombi mkisali kila wakati katika Roho, mkikesha kwa jambo hilo na kudumu katika kuwaombea watakatifu wote.” Waefeso 6:18

Ushuhuda 

“Kristo, Mpatanishi wetu, na Roho Mtakatifu huomba na kusihi daima kwa niaba ya wanadamu, bali Roho hatuombei kama atuombeavyo Kristo anayewasilisha damu yake, iliyomwagwa tangu misingi ya dunia; Roho hutenda kazi katika mioyo yetu, akitoa maombi na hatia ya dhambi, sifa na shukrani. Shukrani zitiririkazo kutoka kwenye vinywa vyetu ni matokeo ya Roho akigusa nyuzi za nafsi katika kumbukumbu takatifu, akiamsha muziki wa moyo” (Ellen White, SDA Bible Commentary, vol 6, aya 1077-78).

Maombi yanaleta changamoto. Hatuwezi kumuona Mungu, na kwa wengi wetu ni mara chache sana, kama imeshatokea, humsikia Mungu. Hatuwezi kumgusa, na nyakati nyingine huonekana kama vigumu kwa majibu kutokea. Pia tuna maswali mengi sana kuhusu namna maombi yanavyotenda kazi, au kwa nini yanaonekana kutotenda kazi.

Ninakumbuka nilivyoomba kama kijana mdogo na kuwa na hali ya kukata tamaa. Mara nyingi nilisinzia (nikiomba huku nimeinamisha kichwa na kufumba macho), na mara kadhaa akili yangu iliwaza orodha ya mambo niliyohitaji kutenda badala ya kuzungumza na Bwana. Nyimbo kama “Saa heri ya Maombi” zilikuwa ni fumbo kwangu. “Ni kwa namna gani mtu anaweza kuomba kwa lisaa lizima? Ni vigumu kwangu kuomba kwa dakika 15 tu.” Hata hivyo, utafiti mmoja huonyesha kwamba muda wa wastani ambao wachungaji hutumia katika maombi ni dakika 7 hadi 10 kila siku! Ninahisi hatia. Kwa mambo yote ambayo mchungaji anapaswa kuyatenda kwa moyo, maombi ndilo jambo la muhimu Zaidi ya yote.

Nilipokuwa nikijifunza kwa undani mada ya Roho Mtakatifu, nilikutana na fungu hili: “Kadhalika Roho naye hutusaidia udhaifu wetu, kwa maana hatujui kuomba jinsi itupasavyo, lakini Roho mwenyewe hutuombea kwa kuugua kusikoweza kutamkwa” (Warumi 8:26). Sikuelewa kwa ukamilifu fungu hili kwa wakati ule, lakini ilikuwa wazi kwamba Roho Mtakatifu angenisaidia katika maombi. Wazo hilo moja lilianza kubadilisha maisha yangu ya maombi. Mungu ameahidi kunisaidia kuomba, hivyo nilianza kudai ahadi hiyo kwa moyo wangu wote. Niliposinzia, nilidai ahadi hiyo.

Akili yangu ilipoanza kuwaza mengine, nilidai ahadi hiyo. Baada ya muda thamani cha maombi yangu na muda niliotumia katika maombi viliongezeka. Pia, nilitumia muda mwingi Zaidi katika maombi, changamoto binafsi zilitatulika au ziliondoka, na miujiza ilianza kutendeka. Siwezi kuelezea ni kwa nini, lakini inaonekana kuwa ni kweli: muda unaotumika katika maombi ni muhimu kama thamani ya kile tunachokinena.

Japokuwa nyakati nyingine maombi bado ni changamoto, huwa ninaona kama muda unasonga haraka, na sina matatizo katika usingizi au kuwaza mambo mengine. Ninafahamu Mungu husikia maombi yangu, na ninafahamu kwamba atajibu kwa wakati na njia yake mwenyewe. Hivyo, tukizungumza kibiblia, kuomba katika Roho humaanisha kufanya jitihada za kibinadamu katika kuboresha muda wetu katika maombi huku tukimuamini Roho Mtakatifu kutuvuvia na kututia nguvu.

Baadhi ya mawazo ya kuboresha katika maisha yako ya maombi: 
  1. Omba kupitia maandiko. Soma fungu na muombe Bwana kuhusu jambo ulilolisoma.
  2. Tumia muziki. Kitabu cha nyimbo za Kristo na vitabu vingine vya nyimbo huwa na maombi mengi sana. Tumia maombi hayo kukusaidia kufahamu unachohitaji kunena. Kuimba ni namna nyingine ya kuomba.
  3. Omba katika eneo lenye hewa safi na mbali na masumbufu.
  4. Andika maombi yako. Watu wengi hufurahia kuandika maombi ya kugundua kwamba huwasaidia kuweka sawa mawazo yao na kujieleza kwa ufasaha Zaidi.
  5. Tafuta mwenzi wa maombi unayeweza kuomba naye ana kwa ana au kupitia simu.
  6. Hudhuria mikutano ya maombi (kanisani au nyumbani) au anzisha mkutano wa maombi.
  7. Andaa orodha ya mambo unayohitaji kuzungumza na Mungu.

Mafungu ya Biblia ya Kuombea

  1. Yuda 20 – Tunajenga Imani yetu kwa kuomba katika Roho Mtakatifu.
  2. Waefeso 6:18 – Omba katika Roho ukiwa na maombi ya aina yo yote.
  3. Luka 6:12 – Yesu alikesha katika maombi.
  4. Luka 11:11-13 – Roho Mtakatifu hutujia kama majibu kwa maombi yetu.
  5. 1 Timotheo 2:1 – Maombi ni jambo la muhimu zaidi tunaloweza kutenda.
  6. Luka 22:43 – Msaada wa kimbingu utasaidia kuimarisha maombi yetu, kama ulivyofanya kwa Yesu. 
  7. Mwanzo 32:24 – Yakobo alipambana na Mungu. Nyakati nyingine maombi huonekana kama kazi ngumu.
  8. Luka 18:1 – Tutabarikiwa ikiwa tutadumu katika maombi bila kufa moyo.
  9. Zakaria 12:10 – Roho ya neema na maombi itamwagwa kwetu na kwa familia zetu.
Mapendekezo ya Maombi

  1. Mpendwa Baba, nifanye kuwa mtu wa maombi na nitumie kuwabariki watu katika maisha yangu. Tafadhali nimwagie Roho wako Mtakatifu na nipatie nguvu.
  2. Bwana, tafadhali kemea Shetani na roho zake za uovu zinazotaka kuniweka kifungoni. Nipatie ushindi dhidi ya dhambi zangu kupitia nguvu ya damu yako. 
  3. Tafadhali okoa watoto na wajukuu wetu. Tuma kila malaika mbingu inayoweza kumtoa ili awaongoze katika uzma wa milele. Vunja nguvu za Shetani dhidi yao, wasaidie waweze kuuona wema wako, na wapatia roho ya kuungama.
  4. Wabariki wachungaji wetu, waalimu, wainjilisti, na washiriki duniani kote kwa roho ya maombi. Tunaomba kwamba sauti ya umoja ya watu wako ifike mbinguni katika wimbo mkuu wa sifa na kusihi.
  5. Bwana, tunaomba ulinzi wako wa watoto na vijana walio katika hatari. Tunaomba uwalinde dhidi ya wale wanaotafuta kuwaharibu.
  6. Tunaomba uwainue wamisionari wa mijini ili kupanda makanisa kwa ajili ya makundi 806 ya watu katika nchi 20 za Divisheni ya Inter-Europe.
  7. Tafadhali inua jeshi la watenda kazi ili kusimamisha makanisa kwa ajili ya makundi 948 ya watu katika Divisheni ya Inter-America
  8. Bwana, tafadhali ongoza maamuzi ya kanisa katika Mkutano wa Uchaguzi wa Konferensi Kuu 2020 (Juni 25 – Julai 4). Tunaomba wajumbe, viongozi, na wageni wajazwe na roho ya uamsho na upendo.
  9. Tunainua majina ya watu saba tuliyoyaandika katika karatasi zetu. Wavute watu hao karibu na wewe.
  10. Mahitaji ya kuombea ya kanisa mahalia:

Nyimbo Zinazopendekezwa

  1. Saa Heri ya Sala #137
  2. Saa Heri ya Maombi #135
  3. Mungu Atukuzwe #3




Siku ya Nane - Jumatano - (15/01/2020)



Kujisalimisha kwa Roho Mtakatifu



Fungu Elekezi:
“Kwa sababu hiyo nawaambia, Kila dhambi na kila neno la kufuru watasamehewa wanadamu, ila kwa kumkufuru Roho hawatasamehewa.” Mathayo 12:32.

Ushuhuda 

“Hakuna mtu anapaswa kuitazama dhambi dhidi ya Roho Mtakatifu kama kitu cha ajabo na kisichoelezeka. Dhambi dhidi ya Roho Mtakatifu ni dhambi ya kudumu kukata kuitikia wito wa kutubu” (Ellen White, SDA Bible Commentary, vol 5, uk. 1093).

Kila mtu aliyejazwa roho hutenda makosa nyakati zingine. Ibrahimu, Musa, Daudi, na Petro wote walikuwa na matatizo katika tabia na kushindwa mara kwa mara katika saa ya majaribu. Hata Yesu alijaribiwa (Mathayo 4), japo hakukubali kujaribiwa. Hivyo, kwa sababu tu tunatembea katika Roho kwa wakati huu haimaanishi kwamba tumevuka nafasi ya kuweza kutenda makosa, na kosa si sawa na kufanya mioyo yetu kuwa migumu katika dhambi.

Mwanamke mmoja katika miaka yake ya mwisho alikuwa mtu asiyejali, aliyekata tamaa, na mwenye hasira. Alikuwa na uvumilivu kidogo kwa wengiine isipokuwa marafiki zake wa karibu kwa miaka hiyo. Wageni walipokuja kanisani, mara nyingi alitoa maneno ya kashfa kuhusiana na watoto wao, mavazi yao, au kitu kingine. Washiriki wapya waliokuwa wamebatizwa na watu wengine walikasirishwa kwa maneno yake ya kashfa na kukosoa. Baadhi walikatishwa tamaa kiasi cha kuwafanya kutokuhudhuria tena kanisani. Wakati wote sikuwa nikifahamu jambo hili hadi kwenye kikao kimoja cha wazee. Niliwauliza wazee kama walifahamu kwa nini watu hawakuwa wakirudi kanisani. Baadhi walinyamaza. Hatimaye mzee mmoja alizungumza: “Mchungaji, tuna mwanamke katika kusanyiko letu asiyeweza kutawala mdomo wake. Husengenya na kukosoa karibu kila mtu. Hii ndiyo sababu watu hawatarudi katika kanisa letu.” “Jambo hili limeendelea kwa muda gani?” niliuliza. “Kwa miaka mingi,” lilikuwa ndilo jibu. “Ni kwa nini hakuna aliyefanya lo lote kuhusu jambohili?” niliendelea. “Baadhi ya wachungaji wamejaribu, lakini hakujawahi kuwa na badiliko.” “Jambo hili haliwezi kuendelea,” nilisema, “hivyo, hili ndilo ninalopendekeza. Nitakwenda kumtembelea mwanamke huyu na kumuomba abadilishe tabia yake ndani ya majuma mawili. Akiwa tayari kubadilika, jina lake litaletwa katika baraza lijalo kwa ajili ya kunidhamishwa. Je, nyinyi wazee mtaniunga mkono katika hili?” Wazee walikubali kuunga mkono mpango huu. 

Nilifanya mipango ya kumtembelea mwanamke huyu kwa ajili ya kumhoji. “Ninafahamu ni kwa nini upo hapa,” alisema mara tu nilipoketi sebuleni kwake. “Unafahamu?” nilijibu. “Ndiyo,” aliendelea kusema, “umekuja hapa kuzungumza kuhusu sababu ya ninavyozungumza na watu.” “Hilo ni sahihi kabisa,” nilisema, “lakini ni kwa namna gani umefahamu hilo?” “Kwa sababu wachungaji wengine wawili wamekuja nyumbani kwangu kuzungumzia suala hilo hilo.” “Kulikuwa na badiliko?” niliuliza. “Hapana, hakuna.” “Kwa nini?” niliuliza. “Kwa sababu nina haki ya kuzungumza ninachoona ni chema, na watu ni wepesi kuhisi tofauti. wanavaa hisia ao katika nguo zao.”

Nilijadili kuhusu tabia ya Mkristo kutumia mafungu kama Waefeso 4:29-31, lakini mwanamke yule bado hakuwa tayari kubadilika. Huku nikiomba moyoni mwangu, nilisema, “Una majuma mawili ya kubadilisha tabia yako, au nitalazimika kupeleka jina lako katika baraza la kanisa kwa ajili ya kunidhamishwa, na nina utegmezi wa wazee wote katika hili.” “Hutafanya hivyo!” alihamaki. “Oh, ndiyo, nitafanya hivyo usipoamua kubadili namna unavyozungumza na watu.” “Siamini kama wazee watakuunga mkono katika hili,” alisema. “Wamekwisha fanya hivyo, na unaweza kuwauliza kama utapenda, lakini hivi ndivyo ilivyo,” nilisema. Udhihirisho huu ulimfanya mwanamke yule atulie na kuwaza kwa ukimya. Kwa upole nilisema, “Sote tunakupenda na tunataka uwe sehemu ya kusanyiko letu, lakini tabia hii inahitaji kubadilika.”

Sabato iliyofuata hakuhudhuria kanisani. Marafiki zake walinikwepa. Nilifahamu kwamba walikuwa wakipambana na hali ile. Sabato iliyofua, kabla tu ya majuma yake mawili kuisha, alikuja kanisani. Nilitembea na kwenda kumsalimu. Uso wake ulikuwa na huzuni, lakini alinishika mkono kwa nguvu. “Mchungaji,” alisema, “Nimefikiria sana ulichosema. Ninataka ufahamu kwamba sasa ninaona kwa uwzi kwamba nimekuwa nikikosea kwa miaka yote hii. Ninatumaini utanisamehe, na nimepanga kuomba msamaha kwa wazee na kanisa zima. Kwa msaada wa Mungu, nitakuwa mwanamke tofauti.” Macho yake yalijawa machozi kwa ukubali huu, na ninafuraha kusema kwamba alikuwa mwaminifu katika ahadi yake. Watu walianza kurejea kanisani, na kusanyiko lilikua kwa haraka.

Mafungu ya Biblia ya Kuombea

  1. Mathayo 12:31, 32 – Kukufuru ni kupuuzia dhambi na kuchukua nafasi ya Mungu (Marko 2:7-11; Yohana 10:33).
  2. Waebrania 6:4-6 – Watu waliobadilishwa kweli wana uwezo wa kugeuka kutoka kwa Yesu.
  3. Waebrania 4:7 – Muda sahihi wa kutii sauti ya Roho Mtakatifu ni mara ya kwanza yeye kunena nawe. 
  4. Matendo 7:51 – Usikatae uongozi na maonyo ya Roho Mtakatifu.
  5. Luka 13:34 – Mpatie Yesu maisha yako kabla haujachelewa, kama ilivyokuwa kwa Yerusalemu

Mapendekezo ya Maombi

  1. Mpendwa Baba, naomba niisikilize sauti yako daima. Nisamehe pale nilipokuwa msumbufu. Fungua macho na masikio yangu ili nisikilize nia yako na nipatie ujasiri wa kutii.
  2. Mpendwa Yesu, nisamehe kwa maumivu niliyokusababishia pale ambapo sikuwa tayari kuachia dhambi zangu. Tafadhali usimuondoe Roho wako Mtakatifu kutoka kwangu na naomba ulainishe moyo wangu ili nipokee maelekezo yako.
  3. Tafadhali samehe kanisa letu pale ambapo hatukuisikiliza sauti yako katika Biblia. Tusaidie sisi kama kusanyiko kujisafisha dhambi na rejesha uwepo wa Roho wako kati yetu.
  4. Fanya ndani yetu moyo safi, Ee Mungu, na uifanye upya roho sahihi ndani yetu. Usituondoe mbali na uwepo wako na usituondolee Roho wako Mtakatifu. Jeresha kwetu furaha ya wokovu wako. Kisha tutawafundisha waovu njia zako, na watabadilishwa na kurejea kwako (Zaburi 51).
  5. Baba, tunaingilia kati kwa ajili ya wale wanaoweza kuwa wahanga wa hali fulani au huongozwa na mazoea mabaya. Tafadhali vunja vifungo vinavyowafunga! Tunaomba tuweze kuwarudisha kwako kupitia upendo na kujali kwetu.
  6. Tafadhali tufundishe namna ya kutangaza misingi yetu ya Imani kwa usawa, ubunifu, na uthibitisho wa kibliblia. Upendo wa Kristo na uwe kiini cha kila kitu tunachokiamini.
  7. Tunakuomba uandae vijana wa kuanzisha makanisa kwa ajili ya makundi 789 ya watu katika nchi 9 za Divisheni ya Kaskazini wa Amerika.
  8. Tunakuomba uinue wamisionari wa kitabibu ili kuanzisha makanisa kati ya makundi 830 ya watu katika nchi 11 za Divisheni ya Afrika Mashariki na Kati.
  9. Tunakuomba uinue mashujaa wa maombi ili kuomba kwa kuingilia kati kwa ajili ya makundi 2,568 ya watu katika nchi 4 za Divisheni ya Kusini mwa Asia.  
  10. Tunakuomba uinue viongozi wapya walio vijana na bariki semina za Uongozi wa Vijana Wakubwa (Senior Youth Leadership).
  11. Asante, Baba, kwa kumtuma Roho Mtakatifu kuwabadilisha watu saba katika orodha zetu za maombi.
  12. Mahitaji ya kuombea ya kanisa mahalia: 



Siku ya Tisa - Alhamisi - (16/01/2020)


Kazi ya Roho Mtakatifu



Fungu Elekezi:
“Baada ya hayo naliona malaika mwingine, akishuka kutoka mbinguni, mwenye mamlaka kuu; na nchi ikaangazwa kwa utukufu wake… Kisha nikasikia sauti nyingine kutoka mbinguni, ikisema, Tokeni kwake, enyi watu wangu, msishiriki dhambi zake, wala msipokee mapigo yake.” Ufunuo 18:1, 4.

Ushuhuda 

“Huduma ya Roho Mtakatifu ya kutenda kazi ndani yetu ndilo hitaji letu kuu. Roho ni mtakatifu katika kazi na udhihirisho wake. Mungu anataka uwe na ujazo wa kiroho; ndipo utafanya kazi kwa nguvu ambayo hukuwahi kuifahamu hapo kabla. Upendo na Imani na tumaini vitadumu. Unaweza kuendelea katika Imani, ukiamini kwamba Roho Mtakatifu yupo pamoja nawe” (Ellen White, Evangelism, uk. 299).

Siku moja kutatokea uamsho mkubwa kati ya watu wa Mungu walio wa kweli duniani. Roho Mtakatifu atashuka kwa nguvu kuu. Ushukaji huu wa Roho Mtakatifu ulifananishwa na mvua ya masika katika nyakati za Biblia, ambayo ingenyesha katika Mashariki ya Kati, ikikomaza mazao na kuandaa mavuno (Zakaria 10:1). Siku moja watu wa Mungu watatoka na kushiriki Imani yao kwa njia yo yote ile iwezekanayo. Miujiza itatendeka kupitia kwa Kristo. Maelfu, pengine mamilioni, wataokolewa. Kazi ya Roho Mtakatifu ni kuokoa waliopotea, na hakuna furaha kuu zaidi kuliko kushiriki katika kazi hiyo.

Katika Sabato moja, Lance na mke wake, Ranea, walikuja katika kanisa letu la Waadventista wa Sabato. Kuna mtu aliacha kitabu kiitwacho Bible Readings for the Home (Masomo ya Biblia kwa ajili ya nyumbani) mlangoni mwa nyumba yao. Kwa sababu ya hali fulani katika maisha yao, Lance na Renae waliamua kuangalie kile kitabu kilisema nini. Wakikiangalia kitabu, waligundua mada ya Sabato, ambayo kwa hakika ilivuta hamasa yao. Walijifunza kwa kina kipande hivyo na walidhihirishiwa kwamba walihitaji kutafuta kanisa lililochapisha kitabu hicho. Baada ya kugundua kwamba kilichapishwa na Waadventista wa Sabato, walitafuta kanisa letu na kuhudhuria Sabato iliyofuata. Lance alishikilia kitabu hicho na kuuliza, “Je, kanisa lako linachapisha kitabu hiki?” “Ndiyo, tunafanya hivyo!” nilijibu. “Vema,” Lance aliendelea, “Tuna maswali mengi. Kuna uwezekano wa wewe kuja nyumbani kwetu kutupatia mafundisho ya Biblia?” Hakika, niliwahakikishia kwamba ningefurahi kufanya hivyo. 

Nilipowatembelea, niligundua kwaba Lane na Renae na vijana wao wa kiume wwili walitamani mabadiliko makubwa katika maisha yao. Walikuwa ni wahanga wa pombe na mambo ya kuharibu, na ndoa yao ilikuwa ikiteseka sana. Nilifahamu kwamba walihitaji nguvu ya Yesu. Kadri niliposhiriki injili, huku nikidumu msaada wa Mungu moyoni mwangu, niliweza kuona Roho Mtakatifu alikuwa akinena nao ndani sana. Nilimaliza uwasilishaji wa injili na kuuliza, “Je, kuna sababu yo yote ya kuwafanya msitoe maisha yenu kwa Yesu?” Walijibu kwamba wangefurahia msamaha na wokovu wa Yesu. Saa ile ile tulipiga magoti na kuomba, na niliwaongoza katika ombi la kuungama na kumkubali Yesu kama Bwana na Mwokozi. Huku wakitokwa machozi walirudia ombi lililosema, na tuliinuka magotini tukiwa na furaha. Nguvu ya muujiza ya Roho Mtakatifu ilikuwa dhahiri. Sasa walizaliwa kama watoto wa Mungu.

Nilipowasili kwa ajili ya kipindi chetu kilichofuata kwa juma, kabla sijamaliza hatua tatu kuelekea sebuleni, Lance aliuliza, “Mchungaji, unafikiri nini juu ya uvutaji wa sigara? Unafikiri ni jambo Mkristo anapaswa kufanya?” Nilipendekeza tujifunze mada ya maisha yenye afya usiku ule, ambayo tulijifunza. Kama matokeo ya kipindi kile ha kujifunza Biblia na siku zilizofuata za mimi kuwatembelea, Lance na Renae walikuwa huru kutoka kwenye vifungo vyote ambavyo Shetani aliwafunga navyo. Na karibuni walibatizwa na wote wakawa wasaidizi wenye nguvu katika shauri la Kristo, wakishiriki shuhuda zao na kutoa masomo ya Biblia kwa wanafamilia na marafiki. Wao pia walianza kushiriki katika kazi ya Roho Mtakatifu kwa kusambaza injili kwa wote waliowazunguka. Ni muujiza wa ajabu kiasi gani!


Mafungu ya Biblia ya Kuombea

  1. Mathayo 28:19, 20 – Kila mfuasi wa Kristo anapaswa kutenda awezalo kutenda ili kusambaza injili ya wokovu.
  2. Yohana 16:13 – Roho Mtakatifu anapotenda kazi, watu watavutwa katika kweli ya Neno la Mungu.
  3. Matendo 4:29-31 – Kanisa la awali lilimuomba Mungu awajaze kwa Roho Mtakatifu ili waweze kutangaza Neno la Mungu kwa ujasiri.
  4. Waefeso 4:11, 12 – Karama za Roho Mtakatifu ni kwa ajili ya kuwaandaa Wakristo kwa ajili ya kazi ya utume na kulijenga kanisa la Mungu.
  5. Matendo 9:36-42 – Kusudi la miujiza ni kwamba watu wawe na ushahidi unaoweza kuwafanya wamuamini Yesu.
  6. Marko 16:15-18 – Enendeni ulimwenguni, ponyeni wagonjwa, hubirini injili, dhihirisheni tabia ya Mungu kwa kila mtu.
  7. Isaya 6:8 – Mimi hapa, Bwana. Nitume mimi. 

Mapendekezo ya Maombi

  1. Mpendwa Baba wa mbinguni, nifanye kuwa mtumishi wako na nisaidie kushiriki ujumbe wa upendo na wokovu wako.
  2. Kwa neema yako, Bwana, ninajitoa kufundishwa na kuandaliwa kushiriki injili kwa namna utakayonichagulia.
  3. Nibatize kwa Roho wako Mtakatifu ili niongozwe kutoka ndani kuweza kushinda vikwazo na hofu. Nifanye niwe mfereji wa nguvu yako na ujumbe unaookoa wa Kristo aliyesulubishwa na kufufuka.
  4. Bariki jitihada za wachungaji, watendakazi wa Biblia, waalimu, na wainjilisti ulimwenguni. Wajaze kwa nguvu kuu na mamlaka. Tunaomba mamilioni ya watoto wako waokolewe kila mwaka!
  5. Tafadhali ruhusu familia zetu kudhihirisha upendo wako katika nyumba zetu na jamii zetu. Tunakuomba ulete uelewano katika familia, ponya mahusiano yaliyovunjika, linda wenye hatari ya kukumbwa na unyanyasaji, na dhihirisha nguvu yako ya kutakaso katika hali zinazoonekana kutokuwa na tumaini.
  6. Tunaomba washiriki wa kanisa letu, wachungaji, na viongozi duniani wajilishe kwa Neno la Mungu kila siku. Tuweze pia kukutafuta kila siku katika maombi binafsi. Tukumbushe kwamba bila wewe, hatuwezi fanya lo lote.
  7. Tunakuomba uinue wauguzi na madaktari ili kuanzisha makanisa kati ya makundi 1,978 ya watu katika nchi 22 za Divisheni ya Afrika Magharibi na Kati.
  8. Tunaomba kwa ajili ya watu milioni 49 katika miji 19 ambayo haijafikiwa Zaidi ya Divisheni ya Tran-Europe
  9. Bwana, tafadhali saidia vijana wetu wasihubiri tu lakini pia waishi hubiri hilo. Tunamba Mungu abariki jitihada za Siku ya Vijana Ulimwenguni (Global Youth Day) na mikakati 100,000 ya uhusishwaji wa kila mshiriki (TMI)
  10. Tunaombea watu saba katika orodha zetu za maombi. Wapatie mioyo ya kukufahamu kama Neno lako linavyosema katika Yeremia 24:7.
  11. Mahitaji ya kuombea ya kanisa mahalia:

Nyimbo Zinazopendekezwa

  1. Nipo Bwana Nitume #107
  2. Sauti Yake Mchungaji #193
  3. Nasikia Sauti Yako #142




Siku ya Kumi - Ijumaa - (17/01/2020)



Kudumu katika Roho Mtakatifu



Fungu Elekezi:
“Nami nitamwomba Baba, naye atawapa Msaidizi mwingine, ili akae nanyi hata milele… Sitawaacha ninyi yatima; naja kwenu… Mtu akinipenda, atalishika neno langu; na Baba yangu atampenda; nasi tutakuja kwake, na kufanya makao kwake.” Yohana 14:16, 18, 23.

Ushuhuda 

“Unapoamka asubuhi, huwa unahisi hali yako ya kukosa msaada, na hitaji lako la nguvu kutoka kwa Mungu? Na huwa unaeleza mahitaji yako kwa unyenyekevu, na kwa moyo kwa Baba yako wa Mbinguni? Kama ndivyo, malaika huweka alama maombiyako, na ikiwa maombi haya hayakutoka kwenye midogo isiyo kusudia, unapokuwa katika hatari ya kutenda kinyume bila kutambua, na kuweka mvuto utakaowaongoza wengine kutenda kinyume, malaika wako wa ulinzi atakuwa kando yako, akikusihi kuwa bora Zaidi, akikuchagulia maneno, na kutia mvuto katika matendo yako” (Ellen White, Messages to Young People, uk. 90).

Sabato moja, nilikuwa nimesimama sehemu ya kuoshea vyombo katika ukumbi wa mikutano yetu ya ushirika nikiwa naosha vyombo baada ya kutumia vyakula tulivyobeba. Mwanafunzi mdogo kutoka Urusi alikuwa akikausha vyombo. Nilifahamu hakuwa Mkristo, hivyo niliomba kwa ukimya kuhusu namna ninavyoweza kutumia muda huu tunaoosha vyombo pamoja. “Nina swali kwako, ikiwa hutojali,” nilisema. “Sawa, ni nini?” alijibu. “Ni kwa nini watu wengi Urusi si Wakristo?” niliuliza. “Unaweza pia kuniuliza kwa nini mimi si Mkristo,” alisema akiwa na tabasamu dogo. “Sawa,” nilisema kwa sauti ya upole, “ni kwa nini wewe si Mkristo?” “Sina tu uthibitisho wa uwepo wa Mungu,” alisema. Kasha aliuliza, “Kwa nini wewe ni Mkristo?” “Kwa sababu nina ushahidi wa kutosha!” nilijibu. Alicheka na kusema, “Sawa, ushahidi wako ni upi?” Kisha nilimpatia ushuhuda wangu wa yale Mungu aliyonitendea.

“Nina uchunguzi, ikiwa utapenda kujaribu,” nilisema. “Ninaamini ukifanya uchunguzi huu utapata ushahidi wa Mungu. Ningependa utumia muda mchache kwa siku 30 zinazofuat kusoma kutoka kwenye kitabu cha Yohana. Ukimaliza kabla siku 30 hazijaisha, anza tena. Pia ningependa uomba Mungu wakati mtu mwingine ye yote hafahamu. Zungumza naye kuhusu mambo ambayo wewe pekee ndiye unayafahamu, na muombe kitu ambacho wewe pekee ndiye unafahamu, kasha uone kitakachotokea.” “Sawa,” alisema, “hilo linaonekana jambo rahisi sana. Utakua uzoefu wa kuvutia.”

Kama mwanafunzi wa kubadilisha mazingira alipaswa kwenda po pote familia yake iliyompokea itakapokwenda ili aweze kuonja ladha ya tamaduni. Hivyo, kila juma alihudhuria kanisani kwa sababu hilo ndilo familia iliyomhifadhi kwa muda ilitenda. Majuma mawili baada ya kuanza utafiti huo, nilihudhuria kanisani kwake na kumuuliza, “Unaendeleaje na utafiti?” Alikuwa makini lakini mwenye kufurhi na alisema, “Sielewi kinachotokea. Bado nina juma moja, lakini sina uhakika kwamba naweza tena kusema hakuna Mungu.” “Hilo ni jambo jema kwako,” nilijibu. “Endelea. Nina uhakika utapata ushahidi ziadi wa Mungu ikiwa utafungua akili yako.” Alitabasamu na kunishukuru alipoondoka siku ile. Alirudi kwao Urusi kabla ya siku 30 kuisha, lakini ninafahamu alikua akiunganika Zaidi na Mungu!

Ni kwa namna gani tunadumu katika uwepo wa Baba, Mwana, na Roho Mtakatifu? 
1. Kwa kutumia muda katika kujifunza Biblia kwa moyo na akili zilizo wazi. Yesu ndiye Neno (Yohana 1:14; 14:6-9), na ikiwa tumemuona, tumemuona Baba. Pia, Roho Mtakatifu ndiye alivuvia Neno la Mung (2 Petro 1:21). Hivyo, kadri tunavyosoma Biblia na kuamini mafundisho na ahadi zake, tunabadilishwa na kuwa katika mfano wa Kristo (2 Wakorintho 3:18).
2. Pili, tunapoomba kwa Mungu, tukifungua mioyo yetu kwake kama tufanyavyo kwa Rafiki, Roho Mtakatifu husogea karibu, mioyo yetu hulainishwa, na tunaweza kushinda majaribu yake kwa nguvu za Mungu.
3. Mwisho, tunapotii Biblia na kushiriki na wengine, tunavutwa karibu na moyo wa Mungu, na utu wetu wa ndani huwa na Amani (Mathayo 11:28-30).

Mafungu ya Biblia ya Kuombea
  1. 2 Petro 1:21 – Roho Mtakatifu alivuvia Biblia. Tunapoisoma na kuikubali, tunadumu katika uwepo wake na wa Yesu na wa Baba (Yohana 14:23).
  2. Luka 11:11-13 – Tunapoomba uwepo wa Mungu tunazidsha nguvu ya Roho Mtakatifu ndani yetu na kutuzunguka.
  3. Matendo 2:1-4 – Roho Mtakatifu anatutaka tushiriki kile alichotufundisha Mungu na namna alivyotubariki. Anataka watu wote kila mahali waokolewe.
  4. 1 Timotheo 2:1-4 – Tunapoomba, Roho Mtakatifu hubariki dunia kutuzunguka na huwaongoza watu katika wokovu.
  5. Matendo 5:31, 32 – Tunapotii kile alichotuambia tutende, tunaongeza uwepo wa Rooho Mtakatifu na mibaraka katika maisha yetu.
  6. Warumi 8:26 – Roho Mtakatifu anataka kutusaidia kuwa watu wa maombi. Hakika mibaraka itafuata (2 Nyakati 7:14). 
Mapendekezo ya Maombi
  1. Mpendwa Baba wa mbinguni, nipatie njaa ya neon lako ili nifurahie kutumia muda pamoja nawe. Ninaposoma Biblia, nipatie uelewa wa wazi wa tabia yako na nia yako katika maisha yangu.
  2. Yesu, tafadhali tuma Roho Mtakatifu katika maisha yangu na nifanye kuwa mtu wa maombi. Nibadilishe na kuwa mwanamaombi mwenye nguvu ili wengi waweze kuokolewa na kuwekwa huru kutoka kwenye vifungo vya giza ya Shetani.
  3. Naomba akili na moyo wangu viwe makini kwa nia yako. Nifanye nitembee katika utii kamili wa amri zako na Neno lako lote.
  4. “Nipokee, Ee Bwana, kwa utakatifu wako, ninaweka mipango yangu yote miguuni pako. Nitumie leo katika huduma yako. Kaa pamoja name, na ruhusu kazi zangu zote kujengwa kwako” (Ellen White, Steps to Christ, uk. 70). 
  5. Bwana, tunawainua viongozi wetu wa kanisa duniani. Tafadhali wapatie hekima kadri wanavyofanya maamuzi na kuwaongoza watu wako.
  6. Tunaomba kwa ajili ya watoto wetu. Tafadhali watie nguvu ili wasimame imara kwa ajili yako wanapokutana na vikwazo na misukumo. Wasaidie kufanya chaguzi sahihi na kusimamia ukweli.
  7. Tunaomba kwa ajili ya familia ambazo mazingira yao yamejazwa vurugu, huzuni, na kuchanganyikiwa.
  8. Bwana, tunaomba uamsho mkuu wa utakatifu usafishe kanisa lako katika siku za mwisho. Tunaomba tusimamie ukweli hata mbingu zikianguka.
  9. Tunaomba kwa ajili ya majina saba katika orodha zetu. Tafadhali muonyeshe kila mmoja namna Yesu anavyompenda.
  10. Mahitaji ya kuombea ya kanisa mahalia:
Nyimbo Zinazopendekezwa
  1. Karibu na Wewe Mungu Wangu #152  
  2. Univute Karibu Baba #148
  3. Asubuhi #89
  4. Tumesikia Mbiu #108 



Sherehe ya Siku ya Sabato ya Mwisho - Jumamosi (18/01/2020)


Kutafuta Roho wa Mungu



Mfumo uliopendekezwa kwa Sabato ya Mwisho

Sabato hii ya mwisho inapaswa kuwa muda wa kufurahi sana katika yale yote Mungu aliyotenda kwa ajili yako na kanisa lako kwa kipindi cha Siku hizi Kumi za Maombi. Buni siku yako kwa ajili ya kusherehekea wema wa Mungu na nguvu yake kuu. Fikiria namna ulivyopata uzoefu wa umwagwaji wa Roho Mtakatifu katika siku hizi kumi zilizopita. Sabato hii ni fursa ya kusherehekea kwa yale aliyotenda, anayotenda, na atakayotenda.

Mahitaji ya kusanyiko yanatofautiana, hivyo tafadhali fanya kazi pamoja na viongozi wa kanisa mahalia ili kueandaa mpango mahususi kwa ajili ya kanisa lako. Hapa kuna baadhi ya mambo ya kujumuisha katika ibada ya kanisa lako katika Sabato ya Mwisho.

Mapendekezo ya Ratiba ya Ibada

  1. 04:30 Nyimbo za kusanyiko.
  2. 04:45 Ukaribisho, matangazo, na maelezo ya matukio.
  3. 05:00 Wimbo wa Sifa (mapendekezo: “Mungu Atukuzwe #3”). Watu wasimame. 05:05 Usomaji kwa kuitikia. Watu wasimame.
  4. 05:10 Maombi ya kusanyiko. Yakiongozwa na mchungaji au mzee wa kanisa. Hili ni ombi la sifa, si kwa ajili ya mahitaji au ombi la kusihi. Watu wapige magoti.
  5. 05:15 Maombi ya kuungama. Watu wakidumu kupiga magoti. Kusanyiko liombe kwa ukimya, kisha kiongozi wa maombi amshukuru Mungu kwa kusikia maombi yetu na kutusamehe dhambi zetu kulingana na 1 Yohana 1:9. Baada ya maombi, watu wanaweza kuketi.
  6. 05:20 Wito na ukusanyaji wa matoleo, ikifuatiwa na ombi la kumshukuru Mungu kwa mahitaji anayotupatia na kumuomba abariki zaka na sadaka hizo.
  7. 05:25 Wimbo maalumu. Chagua wimbo unaoendana na wazo kuu la maombi. 05:30 Mchungaji au kiongozi mwingine atoe ujumbe mfupi kuhusu umuhimu wa maombi katika maisha yetu.
  8. 05:40 Mchungaji au kiongozi mwingine aite watu wasogee mbele ikiwa wana maombi ya mizigo maalumu. Toa muda kwa ajili ya watu kushiriki ikiwa watapenda. Kisha mtu aongoze ombi la kusihi, akiwasilisha maombi kwa Mungu. Watu wanaweza kurudi na kuketi baada ya hapo.
  9. 05:55 Maombi kwa ajili ya huduma mahususi. Mfano: maombi kwa ajili ya jamii, kwa ajili ya watu wanaomhitaji Yesu, kwa ajili ya shule mahalia ya Kikristo na huduma za vijana, kwa ajili ya konferensi na kanisa la kiulimwengu, kwa ajili ya ndoa na familia. Kila kipengele kinaweza kuongozwa na mtu anayehusika na huduma husika; mfano, mwanafunzi anaweza kuombea shule.
  10. 06:10 Wimbo wa kufunga wa kuweka wakfu (Mapendekezo: “Uniongoze Yehova #156; Huniongoza Mwokozi #151”).
  11. 06:15 Maombi na mibaraka ya mwisho. 

Programu za nyongeza kama utapenda

  1. Shuhuda kwa maombi yaliyojibiwa
  2. Muda wa maombi ya makundi madogo
  3. Matangazo ya shughuli za maombi zijazo
  4. Visa vya watoto kuhusu maombi
  5. Vipindi vinavyowasilishwa na vijana