Jumla ya pesa iliyopatikana kwa ajili ya kuchangia uanzishwaji wa Morning Star Televisheni mpaka sasa ni pesa za Kitanzania shilingi milioni 129 taslimu kati ya milioni 500 zinazohitajika
Mchakato wa matoleo hayo kutoka katika majimbo ya kanisa ni ufuatao
Jimbo la Kusini mwa Ziwa Victoria au South Nyanza Conference ni Sh.11,199,000.00
Jimbo la Mara au Mara Conference ni Sh.5,619,712.00
Jimbo la Magharibi au West Tanzania Field ni Sh.3,985,635.00
Jimbo la Nyanda za Juu Kusini au Southern Highlands Conference ni Sh.6,891,398.48
Jimbo la Kaskazini Mashariki au North Eastern Tanzania ni Sh.29,515,917.00
Jimbo la Mashariki mwa Tanzania au Eastern Tanzania Conference ni Sh.65,770,957.00
Wakati zilizokusanywa kupitia simu za mikononi ni Sh.5,300,000.00
Habari hii ni kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mawasiliano wa Kanisa la Waadventista Wasabato Tanzania Mchungaji Musa Mika.